BARAZA LA MADIWANI WAOMBA MAMBA WAVUNWE


Madiwani katika halmashauri ya Nsimbo mkoa wa katavi wakiwa katika kikao cha Balaza la Madiwani
Na Paul Mathias-Nsimbo

Baraza la Madiwani katika Halmashauri yaNsimbo mkoa wa Katavi wameiomba serikali kupitia wizara ya Mali asili na utalii kuja na Mpango maalumu wa kuwavuna wanyama aina ya Mamba kwenye Mto Ugalla kwani wamekuwa wakisabisha vifo kwa wananchi na wanafunzi wanapo kwenda kuteka maji kwenye mto huo.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Nsimbo katikati Charles Halawa pamoja na mkurugenzi wa halmashauri ya Nsimbo Mohamed Ramadhan wa Kwanza kulia na Adam Chalamila Makamu mwenyekiti kwenye kikao hicho

Balaza la Madiwani katika halmashauri yaNsimbo mkoa wa Katavi wameiomba serikali kupitia wizara ya Mali asili na utalii kuja na Mpango maalumu wa kuwavuna wanyama aina ya Mamba kwenye Mto Ugalla kwani wamekuwa wakisabisha vifo kwa wananchi na wanafunzi wanapo kwenda kuteka maji kwenye mto huo.

Elieza Fyula Diwani wa kata ya Mtapenda amiibua hoja hiyo wakati akichangia hoja za kamati kwenye baraza hilo amesema katika kipindi cha nyuma waliomba ushauri huo wa kuwavuna Mamba hao kwenye Mto Ugalla.

Fyula anasema ‘’huko nyuma Mamba waliua watu wengi sana Ugalla na tulishauri ipelekwe kampuni na kupewa zabuni kwaajili ya kuwinda wale wanyama wakapungua na maisha ya watu yakasalimika sasa hii hali imejirudia labda Mamba wamezaana sana’’

Amesema nivyema hatua zikachukuliwa haraka ili maiasha ya wananchi yaendelee kama kawaida.

Baadhi ya Madiwani katika Halmashauri ya Nsimbo mkoa wa Katavi wakiwa katika kikao cha Baraza la Madiwani
Michael Kasanga Diwani wa Kata ya Nsimbo amesema hali hiyo inatokana na wananchi hususani wa maeneo ya vijiji vya katambike kutegemea Maji ya Mto Ugalla kwenye shughuli zao na hupatwa na madhila ya kutafunwa na Mamba wakati wakienda kuteka maji kwenye Mto huo.

Kasanga ‘’anasema Chanzo cha kuliwa wananchi na Mamba nipamoja na uhaba wa Maji wanaenda kufata maji kwenye sehemu ambayo Mamba wapo na mamba wanakaa pale kwa kuwasubili ‘’

Amesema tayari Serikali imeleta fedha kwaajili ya ujenzi wa Mradi wa Maji ambapo zaidi ya shilingi milioni 700 zimeletwa hatua ambayo itapunguza tatizo hilo pindi utakapo kamilika kwa wananchi wa maeneo ya katambike ambao wameonekana kuwa wahanga wa kutafunwa na Mamba hao.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Nsimbo Charles Halawa ambae pia ni Diwani wa Kata ya Ugalla amesema tatizo hilo kwenye Kata ya ugalla lipo na hatua lazima zichuliwe

‘’Hao wanachi wanaozungumnzwa wapo kwenye Kata yangu juzi tumempoteza Mtoto aitwae Mrisho Msombola mwenye miaka 14 alikuwa mwanafunzi wa Darasa la Saba ameondoka na mamba kwahiyo lipozungumziwa suala la Mamba tuwesiliazi kidogo’’ amesema Halawa

Akjibu hoja hiyo Mkurugenzi wa Halmashauri ya Nsimbo Mohamed Ramadhani amesema tayari wameshaandika Barua kwenda Mali asili na utalii kwaajili ya kuomba kibali cha uvunaji wa Mamba hao.

‘’tulifanya jukumu la kuandika Barua wizara ya mali asili kwaajili ya kuomba sasa kibali cha kununwa na mpaka sasa bado hatujapokea majibu yeyote ya kukubaliwa kibali hicho au la ‘’amesema Ramadhani

Jonas Mathas Afisa afisa mali asili Halmashauri ya Nsimbo amesema tayari wameanza kuchukua hatua kwa kuweka alama ambazo Mamba hao wameonekana wakionekana mara kwa mara 

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages