M-MAMA MKOMBOZI KWA WANAWAKE NA WATOTO

 

Mkuu wa wilaya ya Tanganyika Onesmo Buswelu akitoa hotuba ya ufunguzi katika uzinduzi wa Huduma ya M-MAMA kwa niaba ya mkuu wa mkoa wa katavi.

Na Walter Mguluchuma

Katavi.

Mkoa wa Katavi umezindua  mpango    wa kuwasafirisha  kwa wadharula  wajawazito  waliojifungua na watoto wadogo  kutoka kituo kimoja kwenda kwenye kituo kingine  baada ya kupata uzazi  nje ya kituo cha kutolea huduma  ili kuweza kupunguza vifo vya mama na mtoto kwa kushitikisha jamii.


Wadau mbalimbali wa sekta ya afya katika mkoa wa Katavi wakiwa katika uzinduzi wa huduma ya M-MAMA

Mkoa wa Katavi umezindua  mpango    wa kuwasafirisha  kwa wadharula  wajawazito  waliojifungua na watoto wadogo  kutoka kituo kimoja kwenda kwenye kituo kingine  baada ya kupata uzazi  nje ya kituo cha kutolea huduma  ili kuweza kupunguza vifo vya mama na mtoto kwa kushitikisha jamii.

Uzinduzi huo wa Mradi umezinduliwa na Mkuu wa Mkoa wa Katavi ambae aliwakilishwa  kwa niaba yake na Mkuu wa Wilaya ya Tanganyika Onesmo Buswelu uzinduzi ambao uliudhuriwa na viongozi mbalimbali kutoka  Halmashauri zote za Mkoa wa Katavi pamoja na wataalamu kutoka Wizara ya Afya .

Mganga Mkuu wa Mkoa wa Katavi DKT  jonathan  Budenu  amesema kuwa lengo la mradi  huu ni  kushirikisha jamii kusafirisha  wajawazito   wanaojifungua na watoto wachanga  ili kuwasafirisha  kutoka kituo kimoja kwenda kwenye kituo kingine pindi wanapokuwa wamejifungua nje ya kituo ili kuokoa vifo vya mama  na mtoto  vinavyosababishwa na watu kukosa usafiri wa kuwafikisha kwenye vituo vya kutolea huduma za afya .

Amebainisha kuwa   wanajua kwamba  moja ya  masuala  wanayohitaji kuyafanyia kazi  ni rufaa kati ya  vituo vya kutolea huduma  za afya  ,afya  hasa  upatikanaji  wa usafiri wa dharula  kutoka kituo kimoja  hadi kituokingine  kinachoweza kutoa  huduma kwa kiwango cha juu na pia  ukosefu  wa usafiri  wa dharula  kutoka  kwenye jamii hadi kwenye vituo vya kutolea huduma .

 Mradi huu wa M- MAMA  utasaidia sana  kwani kwa sasa Mkoa wa Katavi  unajumla ya magari sita tuu ya kubebea wagonjwa kwa Mkoa mzima  yanayofanya kazi  ya kutowa huduma  za dharula  kwa wagonjwa  kwenye vituo vya kutolea  huduma  za afya .

Msitahiki meya wa Manispaa ya Mpanda Haidary Sumry akitoa katika uzinduzi huo kwa kuwa hakikishia wananchi wa manispaa ya Mpanda kuwa mpango huo utatekelezwa kwa malengo yaliyo kusudiwa
Magari hayo yanatosheleza  asilimia 46 ya usafiri  wa dharula  hivyo bado kuna  upungufu mkubwa   kwenye usafiri wa dharula ,na jambo hili  ni moja  ya vipaumbele  katika  kuokoa  maisha ya wajawazito  na  watoto  wachanga  wanapokuwa na dharula  kiafya kwa asilimia  54.

 Katika hotuba ya Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoka  kwenye uzinduzi wa mradi huu uliyosomwa kwa niaba yake na mwakilishi wake ambae ni Mkuu wa Wilaya ya Tanganyika Onesmo Buswelu  amesema  Mkoa sasa unauhakika  changamoto  hiyo iliyokuwepo itatatuliwa  na mfumo huu wa usafirishaji  wa dharula .

Ambao Serikali  imefanya kazi  na wadau  mbambali wa maendeleo  VODA COM/VODA FONE   na washirika wake  ambao  ni Touch  Found ation   na Pathfinder   International  katika uzinduzi huu  wameweza kupata  maelekezo  juu ya ufanyaji kazi  wa mfumo huu ili viongozi wa ngazi mbalimbali  wawe sehemu ya utekelezaji  wa mpango  kwa kutambua wajibu  na   majukumu yao  katika kutekeleza mpango  husika .

Amesema  mfumo huu   huu wa M- MAMA  utahakikisha  kuwa  vituo   vya kutolea huduma  za afya  ngazi ya chini  zanahati na vituo vya Afya  na wale  wenye dharula  walipo kwenye jamii wanapata usafiri  wa dharula   utaopatikana muda wote  .

Kwa kuwa magari ya kubeba wagonjwa  yapo machache  kwa mfumo huu  watachagua magari machache ya watu binafsi  watakayoyachagua  na kuwatambua  wamiliki  wa magari  katika kila Kata  na kuingia nao mikataba  kupitia Halmashauri  na   madreva wa magari yatakayokuwa yamechaguliwa  wataingizwa kwenye mfumo wa M- MAMA  ambao unaendeshwa na serikali kwa kushirikiana na wadau wengine .

Wadau watahusika  kutowa huduma za usafiri  wa dharula  pale tuu magari  ya serikali  ya ubeba  wagonjwa yanapokuwa yamekosekana  kwa sababu  mbalimbali  zinazo eleweka  muhimu  ni kuhakikisha  kila  mama  mwenye  dharula  anafikishwa  sehemu  stahiki  ili aweze  kupata huduma bora  kwa  wakati .

Meya wa Manispaa ya Mpanda Haidari Sumry amesema kuwa Manispaa ya Mpanda itahakikisha inatowa  ushirikiano wa kutosha kwenye mlagi huu kwa kuwa ni mradi muhimu na unalenga kuokoa vifo vya akina mama na watoto

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages