CRDB WAKALA MKOMBOZI WA AJIRA KWA VIJANA

 

Hamad Masoud Meneja wa Benki ya CRDB Mpanda akitoa neno wakati wa semina maalumu kwa Mawakala wa utoji wa Huduma za kifedha kwa mkoa wa katavi ikiwa ni sehemu ya kuadhimisha miaka 10 ya huduma ya CRDB wakala.

Na Paul Mathias 

Katavi,

Vijana katika Mkoa wa Katavi wameaswa kuchangamkia fursa ya utoaji wa  huduma za kifedha za Kibenki kwanjia ya uwakala Kupitia Benki ya CRDB benki ikiwa ni sehemu ya kukabiliana na tatizo la ajira kwa vijana hapa nchini.

Msitahiki meya wa Manispaa ya Mpanda Haidary Sumry akifungua semina ya siku moja kwa watoa huduma za kibenki wa CRDB katika mkoa wa Katavi ikiwa ni sehemu ya kuadhimisha miaka 10 ya huduma ya CRDB Wakala tangu ianze mwaka 2013
Vijana katika Mkoa wa Katavi wameaswa kuchangamkia fursa ya kutoa huduma za kifedha za Kibenki kwanjia ya uwakala Kupitia Benki ya CRDB benki ikiwa ni sehemu ya kukabiliana na tatizo la ajira kwa vijana hapa nchini.

Wito huo umetolewa na Msitahiki meya wa Manispaa ya Mpanda Haidary Sumry wakati akifungua semina maalumu kwa watoa huduma za kifedha katika mkoa wa Katavi wanaotoa huduma za kifedha kwanjia ya uwakala ikiwa ni sehemu ya kufikisha miaka 10 kwa huduma hiyo kuazishwa katika Benki ya CRDB kote nchini.

Haidary amesema kuwa Vijana wa Mkoa wa katavi hawana budi kuchangamkia fursa ya kuwa sehemu ya kutoa huduma za kifedha kwa kuwa Mawakala ikiwa ni sehemu inayotolewa na Benki ya CRDB Benki kama sehemu ya kukabiliana na changamoto ya ajira kwa vijana.

Baadhi ya mawakala wa utoaji wa huduma za kifedha kupitia uwakala wa Benki ya CRDB katika mkoa wa katavi wakiwa katika picha ya pamoja na  wametunukiwa vyeti kwakuwa mawakala walionza kufanya kazi tangu huduma ya CRDB wakala ilipoanza Mwaka 2013 kwa mkoa wa katavi

‘’nimeambiwa hapa kwa Nchi nchi nzima CRDB benki mnamawakala zaidi ya elfu 25000 nchi nzima na hapa katavi kuna mawakala zaidi ya  60 kwahiyo kati ya hao elfu 25000 na vijana wa katavi wamo hii ni fursa kubwa ambayo mmepewa na Benki ya CRDB benki itumieni vizuri kwa kukuza uchumi wa taifa na uchumi wenu kwa ujumla’’

Amesema huduma hizo za kifedha kupitia Mawakala wa kifedha wa CRDB Benki imelahisisha katika malipo mbalimbali ya kiserikali pamoja na ada za shule kwa wazazi na walezi kupitia huduma zinazo tolewa na Benki ya CRDB benki kwa mawakala wao kwenye maeneo mbalimbali ya mkoa wa katavi.

Haidary amesema kuwa CRDB benki kwa nchi nzima imeweza kutoa ajira zaidi ya Elf 35000 nchinzima hatua hiyo ni sehemu ya kukabiliana na tatizo la ajira kwa vijana hapa nchini.

Amefafanua kuwa Katika kukuza uchumi wa taifa ‘’Benki ya CRDB benki kwa mwaka hufanya miala milioni Miamoja yenye thamani ya Shilingi Trion 50  ambapo kati ya hizo Trioni 1.3 nimapato ya serikali kwa kazi hii mnayoifanya mawakala mnaisadia sana serikali katika ukusanyaji wa mapato’’

Meneja wa Benki ya CRDB Mpanda Hamad Masoud [Kushoto] akimkabidhi cheti moja ya washiriki wa semina ya kuadhimisha miaka 10 tangu huduma ya CRDB wakala ilipoanza kufanya kazi hapa nchini.

Hamad Masoud Meneja wa Benki ya CRDB Benki  tawi la Mpanda amesema kuwa tangu huduma hiyo ya utoaji wa huduma za kifedha kwa mawakala umekuwa na msaada mkubwa kwa wananchi kwa kuepusha Gharama na usumbufu ambao ulikuwa unapatikana katika malipo mbalmbali ya fedha kiserikali na mtu mmoja mmoja.

‘’tunajivunia huduma hii ya CRDB wakala kwa kipindi cha miaka 10 tumekuwa karibu zaidi na wateja wetu kupitia Mawakala hawa ndio maana tunasema CRDB benki ulipotupo’’ amesema Hamad

Baadhi ya watoa huduma za uwakala wa Benki ya CRDB benki katika mkoa wa katavi wakiwa semina maalumu ya kujengewa uwezo juu ya utoaji wa huduma hiyo kwa wateja ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 10 tangu huduma ya CRDB Wakala ianze rasmi.
Nao baadhi ya washiriki wa semina hiyo wamesema wanaishukuru benki ya CRDB benki kwa kuwaamini kwakuwa mawakala wa utoaji wa huduma za kifedha kwani kupitia kazi hiyo wanaendesha maisha yao ya kila siku kwa kufanya shughuli za maendeleo

Mafunzo hayo yamefanyika katika ukumbi wa mikutano wa Katavi Resort Mjini Mpanda kwa kuwa husisha zaidi ya mawakala 60 wa huduma za kibenki kutoka Benki ya CRDB Benki  kutoka sehemu mbalimblali katika mkoa wa katavi.

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages