N. C. O KATAVI YAJITOSA UTUNZAJI MAZINGIRA

 

Na Paul Mathias 

Katavi,

Mkuu wa mkoa wa Katavi mwanamvua Mrindoko ameziagiza taasisi za serikali kujiwekea mikakati ya kupanda miti Milioni moja kwa kila taasisi ikiwa nisehemu ya mwendelezo wa upandaji miti katika kukabiliana na Mabadiliko ya Tabia nchi.

Mkuu wa mkoa wa Katavi ,Mwanamvua Mrindoko Mwenye Kilemba [Katikati] akifurahia jambo na viongozi wa NCO Mwakilishi wa mkuu wa wilaya ya Mpanda pamoja na wanafunzi baada ya kukabidhiwa miti 1000 na Shirika la Nilinde Community Organization
Mkuu wa mkoa wa Katavi mwanamvua Mrindoko ameziagiza taasisi za serikali kujiwekea mikakati ya kupanda miti Milioni moja kwa kila taasisi ikiwa nisehemu ya mwendelezo wa upandaji miti katika kukabikaina na Mabadiliko ya Tabia nchi.

Ameyasema hayo wakati akikabidhiwa miti 1000 na Shirika lilisilokuwa la kiserikali Nilinde Community Organization kwaajili ya kupadwa katika taasisi Mbambali mbali za umma.

Mrindoko amesema ‘’nitoemaelekezo kwa taasisi za serikali kuhakikiasha mnajiwekea lengo la kupanda miti million Moja kwa kila taasisi kama sehemu ya mwendelezo wa zoezi la upandaji miti kwenye taasisi zenu kama wewe ni mkuu wa taasisi na upo hapa kafanye hivyo ili uendelee kuitwa mkuu wa taasisi hiyo ‘’

Amesema kuwa kwakuwa suala la upandaji miti nia agenda ya kitaifa hivyo kila mwanachi katika mkoa wa Katavi anaowajibu wa kushiriki katika zoezi la upandaji miti kwa lengo kuhifadhi mazingira.

Mkuu wa mkoa wa Katavi,Mwanamvua Mrindoko [katikati ya waliosimama] kulia kwake ni Mkurugenzi wa Shirika la Nilinde Community Organization na kushoto kwake Mboninpambaye Nkolonko Mwakilishi wa mkuu wa wilaya ya Mpanda wakiwa na wanafunzi baada ya kukabidhiwa Miti na shirika la Nilinde Organization.   

Ameeleza kuwa miti hiyo iliyotolewa na taasisi ya Nilinde Community Organization ikapadwe katika shule za msingi na sekondari kulingana na mahitaji ya shule husika katika maeneo yao ili kuunga mkono juhudi za serikali katika suala la utunzaji wa Mazingira.

‘’niombe walimu mliopo hapa hakikisheni Miti hii tuliyopatiwa leo mnakwenda kuisimamia ipandwe vizuri kwenye maeneo yenu ya shule na muisimamie ukue na isitwi’’

Katika hatua nyingine mkuu huyo wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko ameipongeza taasisi ya Nilinde Community Organization kwa kuona umuhimu wa kushiriki katika utunzaji wa mazingira kwa kuotesha miche ya miti na kuigawa kwa serikali.

Awali akitoa taarifa kwa mkuu wa mkoa Mkurugenzi wa Shirika la Nilinde Organization Alinanuswe Edward amesema kuwa Shirika hilo limekuwa likitoa Miti ya Matunda  kwa taasisi mbalmbali zikiwemo shule za msingi na sekondari katika mkoa wa Katavi.

Alinanuswe ‘’anasema Mwaka 2022 mwanzoni shirika lilitoa miti ya Matunda 1200 kwa shule za msingi na sekondari mkoani hapa kwaajili ya kuunga mkono juhudi za mkoa katika kukabiliana na lishe duni hali inayopelekea udumavu’’

Katika kulinda vyanzo vya maji shirika hilo kwa mwaka 2022 liliweza kupanda miti ipatayo 650 katika chanzo cha Maji cha bwawa la Milala na mwaka jana shirika hilo lilikabidhi miti 400 kwa afisa mazingira Manispaa ya Mpanda.

‘’katika kuunga mkono juhudi za mkuu wa mkoa wa Katavi kuifanya Katavi iwe ya kijani mwaka jana shirika lilitoa Miti 450 na kukabidhi kwa Afisa mazingira wa Manispaa ya Mpanda’’ amesema Alinanuswe

Amesema lengo la shirika nikuhahakisha mazingira yanatuzwa kwa kizazi cha sasa na kijacho ndio maana wameamua kakabidhi miti 1000 kati ya 6000 mbayo wameamua kuitoa kwa serikali katika mkoa wa Katavi.

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages