RC: KATAVI TUULINDE MUUNGANO WETU KWA VITENDO.

 

Mkuu wa Mkoa wa Katavi,Mwanamvua Mrindoko akiwahutubia wananchi wa mkoa wa katavi kwenye kumbukizi ya Miaka 59 ya muungano wa Tangayika na zanzibar yaliyofanyika kimkoa katika viwanja vya Sharp Rangers Usevya halmashauri ya Mpibwe wilaya ya Mlele

Na Paul Mathias

Katavi,

Wananchi katika mkoa wa Katavi wameaswa kuendelea kulinda Tunu za muungano wa Tanganyika na Zanzibari ulio asisiwa na Viongozi wazalendo wa Taifa la Tanganyika na zanzibari Hayati Abeid Aman Karume na Julias Kambarage Nyerere Mnamo 26/4/1964.

viongozi mbalimbali wa Halmashauri na wilaya wakiwa katika maadhimisho ya miaka 59 ya muungano wa Tanganyika na Zanzibar yaliyofanyika kimkoa katika Halmashauri ya Mpimbwe eneo la Usevya.

Wananchi katika mkoa wa Katavi wameaswa kuendelea kulinda Tunu za muungano wa Tanganyika na Zanzibari ulio asisiwa na Viongozi wazalendo wa Taifa la Tanganyika na zanzibari Hayati Abeid Aman Karume na Julias Kambarage Nyerere Mnamo 26/4/1964.

Akiwa hutubia wanachi wa mkoa wa Katavi katika maadhimisho ya kumbukizi ya miaka 59 ya muungano wa Tanganyika na Zanzibar yaliyofanyika kimkoa katika halmashauri ya Mpibwe Eneo la viwanja vya Sharp Rangers Usevya.

 Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Hoza Mrindoko amesema muungano huo ishala ya umoja na mshikamano kwa wanachi wa Tanzania Bara na Tanzania Visiwani.

Amesema kuwa kupitia muungano huu Wananchi wamepewa uhuru wa kuchagua mahali pakuishi bila kizuizi chochote kwa kuzingatia kanuni taratibu za nchi ndani ya jamuhuri ya muungano wa Tanzania na Visiwa vya Zanzibari

Mrindoko ameeleza kuwa muungano umeweza kukuza uchumi kwa wanachi kwakuwa wananchi kutoka Tanzania Bara na wananchi kutoka visiwani Zanziba wanao uhuru wa kufanya shughuli za kiuchumi pasipo na kikwazo chochote hali ambayo huimalisha uchumi kwa wananchi kupitia shughuli za kiuchumi.

Katika hatua nyingine Mrindoko ameeleza kuwa kuna faida kubwa ya muungano hasa katika eneo la ulinzi na usalama wa mipaka ya Jamuhuri ya muungano wa Tanzania hali hii husaidia katika kuendeleza Amani na utulivu katika kulinda Rasilimali za nchi kwa manufaa ya wananchi na maendeleo kwa wananchi.

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko[ aliyeketi katikati] akiwa na mkuu wa Wilaya ya Mlele Alhaji Majid Mwanga [watatu kutoka kulia] pamoja na Katibu wa itikadi na uenezi wa chama cha Mapinduzi CCM Mkoa wa Katavi Joseph Lwamba

Amesema katika kuendelea kuenzi Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ni muda muafaka sasa kwa wazazi na walezi kuendelea kuwaelimisha watoto juu ya umuhimu wa muungano wa Tanganyika na Zanzibari ili kuwa na kizazi kitakachokuwa na uelewa kuhusu muungano huu adhimu kwenyye Jamuhuri ya muungano wa Tanzani.

Ikumbukwe kuwa Muungano huu wa Tanganyika na Zanzibar umebaki kuwa muungano imala hali ambayo inatimiza ndoto za viongozi waasisi wa  Mataifa ya Afrika akiwemo hayati  Mwalimu Julius Kambarage Nyerere pamoja na baadhi ya viongozi waasisi wa Mataifa ya Afrika kama Kwame Nkrumah wa Ghana pamoja na viongozi wengi wa afrika amabao walitamani afrika iungune ndoto ambazo hazikufanikiwa kutokana na changamoto mbalimbali ikiwemo mifumo tofauti ya kiutwala iliyokuwa chini ya ukoloni kwenye Mataifa yao.

Maadhimisho hayo yameenda sambamba na kauli mbiu inayosema MIAKA 59 YA MUUNGANO NDIYO NGUZO YA KUKUZA UCHUMI WETU, Kwa sisi wazalendo wa Taifa hili sote tuseme udumu Muungano wa Tangayika na Zanzibar.

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages