DAMU CHAFU 15 MIKONONI MWAPOLISI KATAVI


Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoa wa Katavi ACP Ali Makame Hamad akitoa taarifa mbalimbali za utendaji kazi wa Jeshi hilo Mbele ya waandishi wa Habari ofisi kwake.

Na Paul Mathias.-Katavi

Jeshi la polisi mkoa wa limewakamata watoto 15 wanaojihusisha na makundi ya uharifu katika umri Mdogo ambayo yamekuwa yakijukiana kwa majina ya Damu chafu na Manyigu.

Vitu mbambali vilivyokamatwa na polisi vinavyosadikiwa kuwa nivyawizi 

Jeshi la polisi mkoa wa limewakamata watoto 15 wanaojihusisha na makundi ya uharifu katika umri Mdogo ambayo yamekuwa yakijukiana kwa majina ya Damu chafu na Manyigu.

Akitoa taarifa mbele ya waandishi ya utendaji kazi ya Jeshi la Polisi Mkoa wa Katavi Kamanda wa Polisi mkoa wa Katavi Ali Hamad Makame amesema jeshi hilo kupitia misako mbalimbali limeweza kuwa kamata watoto hao pamoja na wazazi wao na kufikishwa mahakamani na kulipa faini ya Shilingi 50000/=.

Kamanda Makame amewaonya  vikali wazazi na walezi amabao wamekuwa wakiwatumikisha watoto wao kwa kufanya shuguli za kiuchumi kwa kuuza baiashara ndogo ndogo mitaani badala ya kuwapeleka watoto hao shule na kusisaitiza kuwa jeshi hilo halitakuwa na simile kwa mzazi au mlezi wa mtoto ambae atabainika kumtumikisha mtoto wake katika biashara ndogo ndogo mtaani.

Ameeleza kuwa Mpaka sasa kuna msako mkali unaendelea kufanyika katika maeneo mbalimbali ya mkoa wa Katavi ya kuhakikisha watoto wadogo hawajihusishi na Biashara muda wa Masomo  huku baadhi yao kujiingiza katika vikundi vya kiharifu.

‘’Tunaendelea kufanya Msako wa kuwakamata watoto wadogo wanaofanya baiashara ndogo ndogo na katika hili hatutakamata mtoto pekee tutamkamata hadi Mzazi wake ili atuambie kwanini mtoto anampa majukumu ya kutunza familia wakati mzazi na mlezi upo’’

Vitu mbambali vilivyokamatwa na jeshi la polisi ambavyo vinasadikiwa ni mali za wizi

Katika hatua nyingine makame amewaomba wazazi kuzingatia malezi ya watoto kwakuzingatia maadili ya utanzania na kuwalea watoto katika misingi ya hofu ya mungu ili kutengeneza kizazi ambacho hakina tabia za uharifu katika siku za usoni.

‘’tusemetu kwamba  suala hili la malezi ya Watoto linaumuhimu wa kipekee kwa watoto waliochini ya umri wa miaka 18 hawa wanatajwa kwamba wanakianzana na sheria maana yake bado wazazi wanalojukumu la kuhakikisha kwamba wanawasimamaia vyema watoto wao kwani umri huo niwawatoto kwenda shule lakini wanaachiwa mitaani na hatimae kuingia katika wimbi la uharifu sisi kama jeshi tutaendelea kutekeleza wajibu wetu na sisi kama jeshi la Polisi  tutakamata mtoto na mzazi wake ambae atakwenda kinyume kwa kuwatumikisha watoto au mtoto wa mazazi fulani kujiingiza katika makundi ya uharifu’’

Jamii kwa ujumla lazima iwe sehemu ya kuhakikisha watoto wanalelewa katika misingi ya malezi bora na maadili kuanzia ngazi ya familia ili kuepuka wimbi la mmomonyoko wa Maadili kwa watoto na kukua katika mwenendo mwema ili kuwa na jamii yenye Tabia njema.

Katika taarifa hiyo jeshi lapolisi mkoa wa katavi limeweza kuwakamata watuhumiwa 214 wa makosa ya mali za wizi na watuhumiwa 14 wakijihusisha na uharifu wa wa makossa ya uvunjaji na kuiba vitu mbalimbali kama Redio,Jogofu,Tv tatu,Mageti ya chuma ya milango 40.

Wananchi wameobwa kufika kituo cha Polisi Mpanda kwaajili ya utambuzi wa vitu vyao wakiwa na vielelezo vya uhalali wa ununuzi wa vifaa hivyo kabla ya kuibiwa.

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages