SERIKALI YASHUSHA NEEMA VIFAA TIBA HOSPITALI YA NKASI

 

Vifaa Tiba vilivyo tolewa na serikali katika Hospitali ya Wilaya ya Nkasi Mkoa wa Rukwa nye Thamani ya Shilingi Bilion 1.8


Na Israel Mwaisaka,Nkasi

Wilaya ya Nkasi imepokea vifaa tiba na dawa vyenye thamani ya shilingi Bilioni 1.8 kwa ajili ya Hospitalii ya Wilaya, Vituo vya afya Vinne na zahanati kumi.

Vifaa tiba vilivyotolewa na Serikali katika hospitali ya Wilaya Nkasi Mkoa wa Rukwa

Wilaya ya Nkasi imepokea vifaa tiba na dawa vyenye thamani ya shilingi Bilioni 1.8, kwa ajili ya Hospitalii ya Wilaya, Vituo vya afya Vinne na zahanati kumi.

Mkuu wa wilaya ya Nkasi Peter Lijualikali amesema wamepokea mashine za kisasa za Mionzi, CT SCAN mashine pamoja na vifaa vya vipimo mbalimba vya magonjwa

amesema kuwa baada ya serikali kukamilisha ujenzi wa hospitali ya wilaya na vituo vya afya sambamba na zahanati serikali sasa imetimiza ahadi yake ya ununuzi wa vifaa tiba na dawa katika wilaya Nkasi

Mkuu huyo wa wilaya alisisitiza kuwa serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Dkt,Samia Suluhu Hassan iliahidi kuboresha huduma za afya na sasa hayo ndiyo matokeo yake na kubwa ni hjili la kupatikana kwa vifaa tiba vya kisasa.

Mkurugenzi mtendaji wa wilaya Nkasi Williamu Mwakalambile kwa upande wake alidai kuwa ujio wa vifaa tiba hivyo vya kisasa unamfanya yeye kuwapeleka wataalamu kwenye mafunzo zaidi juu ya matumizi ya vifaa hivyo na kwa kuanzia ataanza na wataalamu wawili.

Alisema kuwa lengo lake ni kuwa na wataalamu 8 waliopata mafunzo kwa kipindi cha miaka 3 na kuwa ana uhakika kuwa kama kama wataalamu wa vifaa hivyo watakuwepo kuna uwezekano mkubwa wa jamii kupata huduma bora ukilinganisha na siku za nyuma.

"vifaa hivi vya kisasa vinaendana na utaalamu wa kutosha hivyo halmashauri itahakikisha inawapeleka wataalamu wetu kwenye mafunzo na ndani ya miaka mitatu tutahakikisha wataalamu wanapatikana na kubwa ni tija katika huduma za afya kwa jamii" alisema

Awali mganga mkuu wa wilaya Nkasi Benjamini Chota alianisha vifaa vilivyopokelewa kuwa ni vifaa vya mionzi,CT Scan,Ex-Ray,kifaa cha tiba ya meno,kifaa cha kupima damu (Blood test machine) vifaa vya tiba ya macho na vipimo vingine vya kisasa vya magonjwa mbalimbali.

Alisema kuwa hospita ya wilaya pekee ilipokea Mil.900 na baadae serikali ilipeleka milioni 900  kwa ajili ya kununua vifaa vingine na katika mgawanyo wa hiyo fedha vituo 4 vya afya navyo vimenunuliwa vifaa vya afya pamoja na zahanati 10.

katibu wa CCM wilaya Nkasi Robert Mwega alidai kuwa ujio wa vifaa tiba hivyo vya kisasa ni sehemu ya ilani ya CCM ya kuhakikisha huduma bora za afya zinapatikana na jamii inakuwa salama.

Hospitali ya wilaya Nkasi imekamilika kwa gharama ya ujenzi wa zaidi ya shilingi Bil.1.8 na kuifanya jamii kuwa na uhakika wa huduma za kiafya.

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages