WANANCHI WAISHUKURU TANROADS KWA KUWAREJESHEA MAWASIANO YA BARABARA.

 

Wananchi wa Kata ya Ilunde wakivuka Daraja la Mto Ipati  baada ya kujaa Maji.

Na Walter Mguluchuma ,Mlele

Wananchi wa Kata yaIlunde katika Wilaya ya Mlele Mkoani Katavi  wamewashukuru wakala wa Barabara  Tanzania  (TANROADS)  Mkoa wa Katavi kwa kuweza kuwarejeshea  mawasiliano  ya barabara kwa  wakati   iliyowaunganisha na makao makuu ya Wilaya yao ya Mlele ambayo  iliyokuwa hapitiki  kutonana na maji kupita juu ya daraja .

Meneja wa Tanroads Mkoa wa Katavi Mwandisi Martin Mwakabende wakati alipokuwa kwenye eneo la daraja la mto  Ipati  akiangalia namna ya kurudisha mawasiliano ya barabara ya kwenda Ilunde kutokana na  maji kupita juu ya daraja la mto huo

Wananchi wa Kata yaIlunde katika Wilaya ya Mlele Mkoani Katavi  wamewashukuru wakala wa Barabara  Tanzania  (TANROADS)  Mkoa wa Katavi kwa kuweza kuwarejeshea  mawasiliano  ya barabara kwa  wakati   iliyowaunganisha na makao makuu ya Wilaya yao ya Mlele ambayo  iliyokuwa hapitiki  kutonana na maji kupita juu ya daraja .

Barabara hiyo ilishindikana kupitika kufuatia  mvua kubwa iliyonyesha  usiku wa kuamkia  Aprili 5 na kusababisha maji kupita juu ya daraja la mto  Ipati  uliko katika eneo la Kijiji cha Mapili  maji kupita juu ya daraja  na kusababisha barabara hiyo kutopita kwa masaa kadhaa.

 Salome Mbaluku     mkazi wa Kijiji cha Ilunde   amesema hari ilikuwa ni mbaya  kwenye eneo hilo kwani magari yalishindwa kupita kabisa kutokana na maji hayo hali ambayo ilifanya baadhi ya watu wavuke kwa kubebwa migongoni na kutozwa kiasi cha kuanzia tshs 2000 hadi  tshs 4000 kutegemeana na uzito wa mtu .

Amesema kuwa tuna  washukuru TANROADS Mkoa wa Katavi  waliokuwa wameongozwa na Meneja wao Mwandisi Martin Mwakabende walioweza kufika kwenye eneo hilo  na kuweza kufanya jitihada kubwa na  kuweza kurudisha kwa wakati  mawasiliano hayo ya barabara hiyo muhimu kwa uchumi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mlele .

Maiko  Kasagula mkazi wa Kijiji cha Ilunde amesema kuwa walikuwa hawaamini kama mawasiliano hayo ya barabara yangeweza kurejeshwa kwa muda huo mfupi kutokana na hari ilivyokuwa imeonyesha ni jinsi gani Serikali inavyowajari wananchi wake mpaka wa pembezoni kama Ilunde .

Meneja wa Tanroads Mkoa wa Katavi  Mwandisi Martin  Mwabande amesema kuwa taarifa ya kukatika kwa mawasiliano hayo walipata  kutoka kwa Diwani wa Kata ya Ilunde  Martin Mgoroka na  baada ya taarifa hizo walifika kwenye eneo la tukio na  kukuta mawasiliano ya barabara yakiwa yamekatika kutokana na maji kupita juu ya  daraja .

Amesema jitihada za haraka za kurejesha  mawasiliano zilifanyika kwa kupeleka  haraka mndarasa aliyekuwa akifanya kazi kwenye barabara ya  Inyonga  kwenda Maji Moto .

Mwakabende amesema kuwa pamoja na kufanyika kwa matengenezo hayo ya dharula bado   Tanroads wataendelea kuwepo kwenye eneo hilo la daraja  ili kuhakikisha wananchi hawakosi mawasiliano licha ya eneo hilo kuwana maji mengi ya mvua yanayotokana na mvua zinazoendelea kunyesha kwa sasa .

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages