KATAVI YAPANDA MITI MILIONI 6

 

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko akipanda Mti kwa pamoja na moja ya Mkazi wa kijiji cha Isinde katika shule ya Msingi Isinde Halmashauri ya Nsimbo Mkoa wa Katavi.

Na Paul Mathias-Katavi

Serikali ya katika mkoa wa Katavi imesema zoezi la upandaji miti ambalo limeanza toka Mwezi wa February Mwaka huu katika halmashauri za mkoa wa Katavi limeeweza kufanikiwa kwa kwa kiasi kikubwa ambapo hadi sasa Miti Milioni Sita imewezwa kupandwa katika maeneo Mbalimbali ya Taasisi za Umma na kwenye makazi ya Watu.

Wananchi na wadau mbalimbali wa mazingira wakishiriki zoezi la upandaji miti katika eneo la shule ya Msingi Isinde Halmashauri ya Nsimbo mkoa wa Katavi.

Serikali ya katika mkoa wa Katavi imesema zoezi la upandaji miti ambalo limeanza toka Mwezi wa February Mwaka huu katika halmashauri za mkoa wa Katavi limeeweza kufanikiwa kwa kwa kiasi kikubwa ambapo hadi sasa Miti Milioni Sita imewezwa kupandwa katika maeneo Mbalimbali ya Taasisi za Umma na kwenye makazi ya Watu.

Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko amebainisha hayo wakati akizungumnza na wananchi wa Kijiji Cha Isinde Halmashauri ya Nsimbo mkoa wa Katavi ikiwa ni Sehemu ya maadhimisho ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar kwa kufanya shughuli za upandaji miti katika Shule ya Msingi Isinde.

amesema kuwa tangu Shughuli Mbalimbali za upandaji wa miti zianze katika maeneo mbalimbali ya mkoa wa Katavi hadi sasa kuna miti zaidi ya Milioni 6 imepandwa katika mkoa wa Katavi ikiwa ni sehemu ya kutekeleza Maagizo ya viongozi wa juu ya suala la utunzaji wa Mazingira

Mohamed Ramadhan mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Nsimbo akieleza utekelezaji wa zoezi la upandaji miti katika halmashauri ya Nsimbo

‘’Mrindoko hapa anasema kwa takwimu ambazo tunazo mkoani na tumefatilia mkoa mzima kwa maana ya halmashauri zote Tano miti iliyopandwa ni zaidi ya million 6 na laki 9 lakini maelekezo ya Makamu wa Rais wetu na Rais kupitia wizara ya Mazingira nilazima kila halmashauri ipande miti Milioni 1 na laki Tano’’

Amesema zoezi hilo la upandaji miti niendelevu na wiki ijayo litaanza kwa awamu ya pili ikiwa ni sehemu ya kufikisha lengo la kupanda miti Milioni Saba na laki Tano kwa mkoa wa Katavi.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Nsimbo Mohamed Ramadhani amsema kuwa halmashauri hiyo imekuwa ikitekeleza agizo la Upandaji miti kwa kupanda miti katika sehemu mbalmbali za halmashauri ya Nsimbo

‘’kwaajili ya kupendezesha mji wetu kata hii ya Mtapenda nimiongoni mwa maeneo ambayo yamepagwa ukitoka manispaa ya Mpanda mpaka kufika hapa hapa katikati pote panaendelea kupimmwa na kupangwa barabara hii kutoka Nsimbo sekondari mpaka hapa Isinde hadi makao makuu ya kata ni karibu kilomita Sita na barabara hii inayopitia Mtapenda kwenda Manispaa tumepanda miti hivyo baada ya muda tutakuwa tunapita kwenye kivuli kupitia miti tuliyoipanda’’ amsema Mohamed.

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua     Mrindoko akimwagilizia Maji Mbunge wa Jimbo la Nsimbo Anna Lupembe Baada ya kushiriki zoezi la kupanda Mti Katika shule ya Sekondari Anna Lupembe iliyopo halmashauri ya Nsimbo mkoa wa Katavi.

Kwa upande wake Mbunge wa Jimbo la Nsimbo Anna Lupembe ambae pia ni Makamu mwenyekiti wa kamati ya Bunge ya mazingira na Maji amesema kuwa kamati hiyo imekuwa ikisistiza suala la uhifafadhi wa mazingira ikiwa nipamoja na Upandaji wa Miti.

Mimi kama makamu mwenyekiti wa kamati ya bunge ya Maji na Mazingira nimeona tuanze hapa leo Isinde kwa kupanda miti ili kutunza Mazingira amesma Anna Lupembe Mbunge wa jimbo la Nsimbo kwenye zoezi Hilo.

Zoezi la upandaji miti limefanyika katika shule ya Msingi Isinde na Shule ya Sekondari Anna Lupembe ambapo zaidi ya Miti 800 imeweza kupadwa kwenye zoezi hilo.

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages