MICHEZO NI AJIRA ''ASEMA ANNA LUPEMBE''

 

Mbunge wa Jimbo la Nsimbo Anna Lupembe akiwahutubia wanamichezo waliojitokeza katika Bonanza la michezo kwenye Viwanja vya Shule ya Sekondari Nsimbo Mapema leo.
Na Paul Mathias-Nsimbo

Wakazi wa Mkoa wa katavi wameaswa kulichukulia suala la michezo kamasehemu ya ajira na Upendo na mshikamano katika kwenye jamii.

Viongozi mbalimbali wa mkoa wa Katavi wakiongozwa na mkuu wa mkoa wa katavi Mwanamvua Mrindoko [mwenyekilemba Cheupe katikati] akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya viongozi wa serikali na chama walioshiriki katika bonanza hilo

Wakazi wa Mkoa wa katavi wameaswa kulichukulia suala la michezo kamasehemu ya ajira na Upendo na mshikamano katika kwenye jamii.

Akizungumnza katika Bonanza la Michezo lililofanyika katika viwanja vya Shule ya Sekondari Nsimbo Mbunge wa Jimbo Hilo Anna Lupembe amesema kuwa michezo imekuwa ni sehemu ya Ajira kwa vijana kwa kujipatia kipato kupitia michezo ya aina mbalimbali.

‘’sisi kama halmashauri yetu ya Nsimbo tumeamua fedha za Jimbo tutumie kujenga viwanja vya hivi vya Mpira wa Pete na Mpira kikapu ili kufanya maendeleo ya Michezo tukitambua kuwa michezo ni Ajira, michezo ni furaha,michezo ni amani’’

Mkuu wa mkoa wa Katavi mwanamvua Mrindoko akipata maelezo kuhusu Mchezo wa Mpira wa Pete kwenye bonanza la michezo lililofanyika katika halmashauri ya nsimbo lililoandaliwa na Mbunge wa jimbo la Nsimbo Anna Lupembe

Lupembe amsema kuwa yeye kwa kushirikiana na Mkurugenzi wa halamsahari pamoja na Madiwani wote wa 16 wa Halmshauri ya Nsimbo kutumia fedha za mfuko wa Jimbo kuhakikisha kumejengwa viwanja Viwili vya michezo ya Mpira wa Pete na Kikapu ili wanachi wa halamsahuri ya Nsimbo wawe na sehemu ya kufanya Mazoezi kwa kuwa michezo ni afya.

Ameeleza kuwa bonanza hilo limefanyika kwa kujumiusha Mikoa ya Dodoma,Rukwa,Tabora,Kigoma na Katavi kwa lengo la kuutangaza mkoa wa Katavi hasa halmashauri ya Nsimbo katika sekta ya Michezo .

Katika hatua nyingine amesema kuwa tangu aanzishe Mashindano Mbalimbali kama Lupembe Cup kumekuwa na mafanikio makubwa kwa baadhi ya vijana kupata fursa ya kujiunga na timu zenye uwezo katika michezo na wengine kupata fursa ya kwenda nchi za nje kupitia Mpira wa Kikapu.

Anna Lupembe anasema ‘’Ndugu Mgeni Rasimi hapa tunakijana amepata fursa ya kupata nafasi ya Kwenda Marekani kucheza Mpira wa kikapu haya ninamafakio makubwa sana katika sekta ya michezo katika halmashauri ya nsimbo ndio maana nimekuwa muumini wa Suala la michezo kwa vitendo ‘’

Michael Kadebe Rais wa shirikisho la Mpira wa Kikapu Tanzania TBF akitoa neno kuhusu umuhimu wa Mpira wa Kikapu kwa vijana

Kwa upande wake mkuu wa mkoa wa katavi Mwanamvua Mrindoko ambae alikuwa Mgeni Rasimi katika Bonanza hilo la michezo katika halmashauri ya Nsimbo amesema kuwa Mmbunge wa jimbo la Nsimbo la Nsimbo Anna Lupembe ni mfano wa kuigwa katika sekta ya michezo katika mkoa wa katavi

‘’Mbunge huyu amekuwa amfano wa kuigwa katika sekta ya Michezo utasikia ametoa Mipira,ametoa majezi,ametoa amagoli hiii inaonyesha nikwa namna gani wanansimbo mmepata Mbunge wa vitendo hongereni sana’’

Mkuu huyo wa mkoa ametumia fursa hiyo kuwaagiza wakurugenzi wa halmashauri kulipa kipaombele suala la michezo kwa kuhakikisha mazingira na miundombinu ya michezo iunajengwa kwa kujenga viwanja vya kisasa.

Mkuu wa mkoa wa Katavi mwanamvua mrindoko akizungumnza na wanamichezo kwenye bonanza la michezo lililofanyika viwanja vya shule ya sekondari Nsimbo

Michael Kadebe  Rais wa shirikisho la Mpira wa kikapu Tanzania amesema kuwa mpira wa kikapu kwa sasa umekuwa na fursa kubwa kwa vijana hasa wanao maliza kidato cha nne kwa kupata udhamini wa kucheza Michezo hiyo nje ya nchi

Ametoa wito kwa wazazi kuwaachia watoto wao kujifunza michezo hii kwakuwa bado inaonekana kuwa na fursa kubwa katika mataifa mengine.

Katika bonanza hilo michezo mbambali ya Mpira wa Miguu kikapu na pete limefanyika kwa kuchezwa michezo kwa kushirikisha wanamichezo kutoka mikoa ya Dodoma,Kigoma,Rukwa,Tabora na Katavi.

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages