waombolezaji wa Msiba katika Mtaa wa Kigoma kata ya Makanyagio Manispaa ya Mpanda Nyumbani kwa mama yake Mzazi Marehemu Kijana Charles Elias alifariki dunia kwa kuchomwa kisu. |
Kijana mmoja mkazi wa Mtaa wa Kigoma Kata ya Makanyagio Manispaa ya Mpanda mkoa wa Katavi amefariki dunia baada ya kuchomwa kisu na watu wasiojulikana majira usiku eneo la Mtaa wa kawajense Mpanda Manispaa.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Katavi Ali Hamad Makame akizungumnzia tukio hilo ofisini kwake na waandishi wa Habari |
Mama
Mzazi wa marehemu Easter Herman amebainisha kuwa asubuhi aliamka na kwenda
kazini kwakwe lakini ilipofika majira ya saa nne asubuhi alipata taarifa za
mwanawe kufariki Dunia.
Ameeleza
kuwa mtoto wake alikuwa anajishughulisha na kazi ya kuuza Barafu na alikuwa
amepanga maeneo ya kawajense ambapo alikuwa anafanya shughuli zake huko.
‘’Ilikuwa
mda wa saa nne asubuhi nilipigiwa simu na Mdogo wangu nikiwa kazini akaniambia
dada una taarifa gani nikamwambia sina taarifa yeyote akaniambia Mtoto wako Charles
amechomwa kisu huko kawajense,, amesema
Easter.
Vumilia
swila mkazi wa Makanyagio na jirani Nyumbani kwa Marehemu amewaasa wazazi
wenzake kuwa na tabia ya kujua mienendo ya kazi za watoto wao wanazo zifanya
ili kukabiliana na wimbi la Mmonyoko wa Maadili katika jamii.
Waombolezaji wakiwa katika msiba huo nyumbani kwa mama mzazi wa marehemu Charles Elias Makanyagio Manispaa ya Mpanda. |
Kwa
upande wake Josephat Katabi mkazi wa Makanyagio amesema kuwa analiomba jeshi la
polisi kuimalisha Doria hasa nyakati za usiku ili kukabiliana na uharifu
unaoweza kujitokeza.
‘’Niiombe
serikali kupitia jeshi la polisi kuimalisha Doria hasa usiku wa manane amabapo
matukio haya hutokea ili kuwe na usalama muda wote,, amesema katabi.
Kamanda
wa polisi mkoa wa Katavi Ali Hamad Makame amekili kutokea kwa tukio hilo na
uchunguzi unaendelea pindi utakapo kamilika jeshi hilo litatoa taarifa kwa wananchi.
Tukio
hili la kufariki kwa Kijana Elias Charles linajiri ikiwa ni Takribani wiki moja
kwa kijana Michael Chapa mkazi wa Shanwe kuuawa na watu wenye hasila kali kwa
kile kilichodaiwa kujihusisha na vikundi vya uharifu maalufu kama damu Chafu.