TUPO TAYARI KUPIMWA USHOGA ASEMA ''SHEKHE MASHAKA''

 

Shekhe Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mashaka Nassoro Kakulukulu akiwa hutubia waumini wa dini ya kiislamu katika swala ya Eid el Fitri iliyoswaliwa katika viwanja vya shule ya Msingi Kashato Wilaya ya Mpanda Mkoa wa katavi

Na Paul Mathias-  Katavi.

Jamii ya Watanzania imeobwa kuungana na serikali katika Mapambano ya Wimbi la ushoga ulawiti na usagaji ambalo limeonekana kushamili kwenye baadhi ya Jamii za Kitanzania ili kulinda maadili na utu wa Mwafrika.

waumini wa dini ya kiislamu katika mkoa wa katavi wakiwa katika swala ya Eid el fitri katika viwanja vya shule ya msingi Kashato.

Jamii ya Watanzania imeobwa kuungana na serikali katika Mapambano ya Wimbi la ushoga ulawiti na usagaji ambalo limeonekana kushamili kwenye baadhi ya Jamii za Kitanzania ili kulinda maadili na utu wa Mwafrika.

Akiwa hutubia waumini wa Dini ya kiislamu katika Uwanja wa Shule ya Msingi Kashato Shekhe Mkuu wa Mkoa wa Katavi Shekhe Mashaka Nassoro Kakulukulu amesema wao kama viongozi wa Dini ya kiislamu katika mkoa wa Katavi wanaungamkono juhudi mbalimbali zilizoonyeshwa na wabunge kukemea suala hilo la ushoga ulawiti na usagaji.

‘’Ikiwa wanawake wataona wao kwa wao wanasagana na wanaume kuoana wao kwa wao kizazi kitaongezeka vipi nilazima kilammoja wetu tukemee jambo hili kwa nguvu zetu zote watu wawa fichue mashoga popote pale walipo ukimjua huyu ni shoga mwambie mwenzako jamaa ni shoga,,amesema Shekhe Mashaka.

Amesema kuwa wao kama viongozi wa Dini wanayasema hayo kwakuwa wanaoahtirika na vitendo hivyo ni pamoja na watoto wadogo kufanyiwa vitendo vya ulawiti hivyo kila mwanajamii lazima kuchukua tahadhari juu ya matendo hayo maovu.

Waumini wa Dini ya kiislamu katika mkoa wa Katavi wakiwa katika swala ya Eid el fitri iliyoswaliwa katika viwanja vya shule ya Msingi Kashato

‘’Wapo watoto wa miaka kumi miaka Mitano miaka kumi ambao tayari watoto hao wameshaharibika kwa hiyo tusipo yasema haya watoto hawa tunawaweka katika mazingira magumu watoto wapo mashuleni wamekwisha haribika na sisi wazazi tuhakikishe watoto wetu waliopo mashuleni tuhakikishe tunawafatilia vilivyo wale wanaosoma shuele binafsi na kawaida je tunawafatilia vizuri ’’amesisitiza Shekhe Mashaka.

Aidha katika hatua nyingine ameeleza kuwa ikiwa kutakuwa na Mpango maalumu wa kupima ili kuwabaini Mashoga viongozi wa Dini ya kiislamu katika mkoa wa Katavi watakuwa wa kwanza kupima ikiwa ni sehemu ya Mapambano juu ya swala hilo.

,,kwahiyo likija suala la kupimwa ili kuwabaini wanaojihusisha na masula ya ushoga sisi viongozi wa Dini wa kiislamu viongozi wa Dini ya kikirsto tujitokeze twende tukapime ili pumba na mchele ujulikane tunaweza tukachanganyikana kwa kupinga ushoga kumbe wewe mwenyewe ni shoga’’amenena Shekhe Mashaka

Hamisa Saburi moja ya waumini walishiriki katika swala hiyo amesema Hotuba ya Shekhe imegusa uhalisia wa namna mambo yalivyo katika kupambana na ushoga na kuiomba serikali kuendelea kulipinga jambo hilo na kuongeza ufatiliaji wa mienendo ya watoto waliopo majumbani na Mashuleni.

‘’Kama mimi mzazazi hotuba ya shekhe nimeilewa nilikuwa naishauri serikali ifatilie hasa katika watoto wa kike nawakiume pia hata sisi wazazi tunapokuwa nyumbani inatakiwa tuwape Darasa watoto wetu tukiwa kama wazazi kuhusiana na haya mambo ya ukatili’’amesema Hamisa

Nae Idrisa Kapena moja ya waumini walio hudhuria swala hiyo amesema changamoto kubwa ya kujitokeza kwa mambo ya ushoga ulawiti usagaji na ulawiti ni mmomonyoko wa maadili na maendele ya sayansi na technolojia hasa utandawazi hivyo jamii lazima iwe makini kwa mafundisho ya watoto na watu wazima.

Sikukuu ya Eid el Fitri huadhimishwa kila mwaka duniani kote ikiwa ni Sherehe  ya kumalizika kwa mfungo mtukufu wa mwezi wa Ramadhani ikiwa ni nguzo ya nne katika Dini ya kiislamu.   

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages