MKOA WA KATAVI WATEKELEZA AGIZO LA MAKAMU WA RAIS KWA VITENDO

 

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko akizungumnza na wanachi juu ya umuhimu wa kutunza mazingira na upandaji miti

Na Walter Mguluchuma

Katavi

Mkoa wa Katavi wametekeleza agizo lililotolewa na Makamu wa Rais  Dkt   Philpo l Mpango  la  kuzitaka kila Halmashauri za hapa nchini kupanda miche ya miti kwa kila Halmashauri zisizopungua milioni  moja  na nusu .

Mkuu wa mkoa wa Katavi, Mwanamvua Mrindoko akipanda mti katika shule ya Sekondari Anna Lupembe

Mkoa wa Katavi wametekeleza agizo lililotolewa na Makamu wa Rais  Dkt   Philpo l Mpango  la  kuzitaka kila Halmashauri za hapa nchini kupanda miche ya miti kwa kila Halmashauri zisizopungua milioni  moja  na nusu .

Mkuu wa Katavi Mwanamvua  Mrindoko   amewambia wananchi wa Halmashauri ya Nsimbo  leo wakati wa zoezi la upandaji miti uliofanyika katika shule ya Msingi Isinde kuwa hadi sasa Mkoa wa Katavi kupitia kwa Halmashauri zake tano za Mkoa huu zimeisha panda zaisi ya miche za miti zaidi ya milioni 6 na laki tisa.

Amebainisha kuwa Mkoa huu bado unaendelea na zoezi hilo la upandaji miti ambapo idadi hiyo ya miti iliyopandwa ni kwenye awamu yao ya kwanza  kwenye  zoezi hilo na sasa wanaingia kwenye awamu ya pili ya upandaji miti hali ambayo inaonyesha kuwa watapanda miti mingi kuliko idadi waliopangiwa .

Kwani  Mkoa wa Katavi umejiwekea  uutaratibu wa kupanda miti na kutunza mazingira kuwa ni utaratibu endelevu ili mkoa huu uendelea kuwa wa kijani zaidi kuliko ulivyosasa licha ya kuwa wakijani .

Ameeleza kuwa zoezi la upandaji miti ulifanywa mwishoni mwa mwezi wa pili mwaka huu kwa awamu ya kwanza  na awamu ya pili itafanyika mwanzoni mwa  mwezi mei kutokana na  msimu wa mvua za masika haribu unakwisha .

Maelekezo ya   Makamu wa Rais na Rais kupitia Wizara ya Mazingira  yanaelekeza kila Halmashauri kufikia lengo kama walivyopangiwa kwa hiyo kwa Mkoa wa Katavi hadi sasa wamebakiza miti michache sana ili  kufikia lengo walikupangiwa  hivyo wataendelea kupanda miti zaidi ya milioni saba walipangiwa  kwa msimu huu.

Amesisitiza kuwa zoezi hili la upandaji miti sio la shoo kwani lazima miti yote iliyopandwa itunzwe na ikuwe na  ilindwe isiharibiwe na binadamu wala wanyama waharibifu  lazima ikuwe na iweze kuleta manufaa yaliyokusudiwa

Mrindoko amezita taasisi za umma kuhakikisha  zinapanda miti na watapita kuzikagua  kila wanapokuwa wanapita kukagua miradi ya maendeleo watakuwa wanakagua na miti iliyopandwa  kwani kamati yake ya kukagua  ipo imara sana

Aidha Rc Mrindoko  alisema kuwa maadhimisho ya Muungano wa Tanzania  Zanzibar na Tanzania Bara yalianza Aprili  17 na yameitimishwa leo  Aprili 29 Nchi nzima  kwa maelekezo yaliyotolewa na Serikali kwamba  maadhimisho yafanyike kwa ngazi ya Mkoa na Wilaya zake  na yaendelee mpaka tarehe 29 kwa  hiyo tarehe ya muungano ina baki ile ile .

 Amewataka wananchi wa Mkoa wa Katavi kuendelea kuulinda na kuutunza  Muungano ili uwendelee kudumu kwani miaka  59 sio michache ni jambo la kujipongeza kwani nchi yetu imeweza kuuwendeleza Muungano na mpaka sasa hivi  hatuja farakana kati ya Tanzania Bara Tanzania Visiwani  .

Mkurugenzi wa  Halmashauri ya Nsimbo Mohamed Ramadhani ameeleza kuwa Halmashauri hiyo mbali ya kupanda miti  kwenye maeneo mbalimbali  wameendelea pia na upandaji miti kwenye maeneo ya  pembeni ya barabara za Halmashauri ya Nsimbo .

Lengo la Halmashauri hiyo pia ni kuhakikisha kila mwananchi anapokuwa anapita barabarani atakuwa anapita kwenye kimvuli  ya miti itakayokuwa pembeni mwa barabara .

Mbunge wa Jimbo la Nsimbo ambae pia ni Makamu mwenyekiti wa Kamati ya Maji na Mazingira Anna Lupembe amesema kuwa Benki ya NMB wameisha towa ahadi ya kutowa kiasi cha shilingi milioni 50 kwa Halmashauri ambayo itafanya vizuri kwenye zoezi la upandaji wa miti .

Hivyo ataendelea kuwahamasisha wananchi wa Nsimbo kuendelea kupanda miti  ili waweze kupata fedha hizo watakazo zitumia kujenga madarasa kwenye shule moja ya msingi .

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages