MIKOA MITANO YASHIRIKI BONANZA LA MH LUPEMBE

 

Mkuu wa mkoa wa Kaavi Mwanamvua Mrindoko akipata maelezo kuhusu Mpira wa Pete kwenye bonanza lililoandaliwa na Mbunge wa Jimbo la Nsimbo Anna Lupembe.

Na Walter Mguluchuma.

      Katavi .

Timu tano za mpira wa Kikapu  kutoka mikoa mitano ya Dodoma , Rukwa , Kigoma,Tabora na   Katavi zimeshiriki bonanza la  mchezo wa mpira wa kikapu  kwenye uzinduzi wa viwanja vya michezo ya mpira wa kikapu na mpira wa pete  Bonanza ambalo liliandaliwa na Mbunge wa  Jimbo la Nsimbo Anna Lupembe .

 
Moja ya Muonekano wa Kiwanja cha Mpira wa Kikapu kilicho zinduliwa kwenye Bonanza hilo
Timu tano za mpira wa Kikapu  kutoka mikoa mitano ya Dodoma , Rukwa , Kigoma,Tabora na   Katavi zimeshiriki bonanza la  mchezo wa mpira wa kikapu  kwenye uzinduzi wa viwanja vya michezo ya mpira wa kikapu na mpira wa pete  Bonanza ambalo liliandaliwa na Mbunge wa  Jimbo la Nsimbo Anna Lupembe .

Bonanza hilo lililohudhuriwa na mamia ya wanamichezo na wananchi wa Mkoa wa Katavi  ambapo  mgeni rasmi  alikuwa  Mkuu wa   wa Katavi  Mwanmvua Mrindoko  pia  bonanza hili  lime hudhuriwa na Rais wa  shirikisho la mpira wa kikapu Tanzamia Michael Kadebe

Akinzumza kabla ya  uzinduzi wa  viwanja hivyo viwili vilivyojengwa  katika  shule  ya Sekondari Nsimbo  Mbunge wa Jimbo hilo Anna Lupembe ameeleza kuwa viwanja hivyo viwili   vya mpira wa pete na vikapu  amevijenga kwa gharama ya zaidi ya shilling  Milioni 50  zilizotokana na fedha za mfuko wa jimbo .

Aliamua kuwekeza kwenye sekta ya michezo kwa kujenga viwanja hivyo viwili na kimoja cha mpira wa miguu kwa kutambua kuwa michezo ni afya na ajira kwa vijana kwa sasa michezo ni ajira nzuri kwa vijana  na ndio maana ameamua kujenga viwanja vya aina mbalimbali kwa ajiri ya kuinua vipaji na afya pia kwa watu wazima kwa kuwa watu wengi wanaandamwa na magonjwa mengi .

 Lupembe amesema  kwa wao  kama viongozi wanaiga  wanaiga  mfano wa Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kwa  kuendelea kutowa hamasa kwenye sekta ya michezo  hapa nchini   ili vijana  wapate ajira kwa kupitia michezo .

Amebainisha kuwa   kwa kutambua umuhimu wa michezo  ameanzisha  mashindano ya  mpira  wa miguu yanayoitwa Lupembe Cup na kwa mwaka jana timu 140 zilishiriki mashindano hayo  ameona ameona bi vema kuibua vipaji vya michezo mingine mbali ya mpira wa miguu  na ndio maana ameamua kufanya bonanza la mpira wa vikapu na pete ili kuinua vipaji kwa vijana .

Rais wa shirikisho wa shirikisho la mpira wa vikapu Tanzania Michael Kadebe  amesema kuwa kupitia kwa bonanza hilo kutasaidia sana kuleta chachu na hamasa kwa wanamichezo  kupenda  kuchezo michezo ya mpira wa vikapu na pete kwani bado kuna furusa kwa vijana .

Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko amewaagiza wakurugenzi wote wa Halmashauri kuhakikisha miundo mbinu ya michezo inaboreshwa na michezo inachezwa mashuleni kuanzia shule za msingi .

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages