MNEC KATAVI ''JUMUIYA ZA WAZAZI WAJIBIKENI KWENYE MALEZI''

Mjumbe wa Halmashauri kuu ya Chama cha Mapinduzi CCM Taifa Mkoa wa Katavi Girbert Samnpa akizungunza na wanachama wa chama hicho katika Wiki ya jumuiya ya wazazi ya chama hicho iliyofanyika katika Kata ya Itenka Halmashauri ya Nsimbo Mkoa wa Katavi

Na Paul Mathias 

Katavi.

Chama cha Mapinduzi CCM Katika Mkoa wa Katavi kupitia Kwa Mjumbe wa Halmashauri kuu ya Chama cha Mapinduzi CCM Taifa Girbert Samnpa katika Mkoa wa Katavi ametoa Wito kwa Jumuiya ya wa wazazi ya  Chama hicho kuungana na serikali katika kukemea Mmomonyoko wa Maadili katika Jamii.

Mjumbe wa Halmashauri kuu ya Chama cha Mapinduzi CCM Taifa Mkoa wa Katavi Girbert Samnpa akimkabidhi Mahitaji mmoja ya Mkazi wa Itenka aliekuja kupata huduma katika Kituo cha Afya itenka ikiwa ni sehemu ya Wiki ya Jumuiya ya wazazi ya chama cha Mapinduzi.

Chama cha Mapinduzi CCM  Mkoa wa Katavi kupitia Kwa Mjumbe wa Halmashauri kuu ya Chama cha Mapinduzi CCM Taifa kutoka Mkoa wa Katavi Girbert Samnpa  ametoa Wito kwa Jumuiya ya wa wazazi ya Chama hicho Mkoa wa Katavi kuungana na serikali katika kukemea Mmomonyoko wa Maadili katika Jamii.

Ametoa wito huo wakati akifungua maazimisho ya Wiki ya Jumuiya ya Umoja wa wawazi ya Chama cha Mapinduzi CCM Mkoa wa Katavi yaliyofanyika katika Shule ya Msingi Itenka Halmashauri ya Nsimbo Mkoa wa Katavi.

Baadhi ya wanachi na wanachama wa Chama cha Mapinduzi CCM kata ya Itenka walivyojitokeza katika uzinduzi wa Wiki ya Jumuiya ya wazazi iliyofanyika kimkoa katika kata Hiyo.
Samnpa amesema kuwa Jumuiya hiyo ya umoja wa wazazi inao wajibu wa kukemea vitendo vya Mmomonyoko wa Maadili kwa kuwa Jumuiya hiyo ndiyo Mlezi wa Viongozi katika kusimamia Maadili kwa viongozi wa Jumuiya ndani ya Chama hicho.

‘’Anasema kwa hali ya sasa hii Jumuiya kama chama cha Mapinduzi kinaitazama sana Jumuiya ya wazazi mmomonyoko wa maadili ambao umekuwa Janga kwa sasa kitaifa na Kidunia’’

Mwenyekiti wa jumuiya ya Umoja wa wazazi Mkoa wa Katavi Evarist Mnyere akitoa neno kwa wanachama wa chama cha Mapinduzi CCM mkoa wa Katavi waliohudhuria kwenye uzinduzi wa Wiki ya jumuiya hiyo iliyofanyika katika Kata ya Itenka Halmashauri ya Nsimbo Mkoa wa Katavi.

Ameeleza kuwa Chama cha Mapinduzi CCM kinaitizama Jumuiya hiyo kama Kitengo Maalumu kwa kuwandaa viongozi wanaochipukia kwenye Ungozi ndani ya chama na Jumuiya kuwa katika maadili na kukemea vitendo vya Mmomonyoko wa maadili katika Jamii.

Katika hatua nyingine amesema Jumuiya ya wazazi imekuwa mlezi kwakuwa imekuwa ijajihusisha Moja kwa moja katika Malezi na Elimu kwa Vitendo zaidi ndani ya chama.

‘’sisi kama chama cha Mapinduzi ndio walezi wetu kupitia jumuiya hii inadili na malezi jumuiya imejikita kwenye Elimu kwa vitendo ndio Jumuiya yenye shule nchi nzima zilizopo chini ya Jumuiya ya wazazi’’amesema Samnpa.

Ameeleza kwa sasa chama hicho kimekuja na sera ya kuimalisha uchumi kuanzia ngazi ya jumuiya za chama ili kukisaidia chama katika mambo mbalimbali yanayo hitaji uchumi kiuendeshaji katika Shughuli mbalimbali.

Wanachama wa Chama cha Mapinduzi CCM mkoa wa katavi wakiwa katika maandamano wakitokea kituo cha afya Itenka wakielekea Viwanja vya Shule ya Msingi Itenka ambako kumefanyika uzinduzi wa wiki ya Jumuiya ya wazazi katika mkoa wa Katavi.

amewaomba wananchi na wanachama wa chama hicho kuendelea kukiamini chama cha Mapinduzi kwakuwa kinatekeleza ilani kwa Vitendo kwenye Miradi ya Maji,Afya,Elimu na miundombinu Chini ya Mwenyekiti wa Chama hicho Rais Dk Samia Suluhu Hassan

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Jumuiya Wazazi Mkoa wa Katavi Evarist Mnyere amesema Moja ya Majukumu ya Jumuiya hiyo ni Kusimamia Mazingira Malezi na Elimu na ndio maana zoezi la upandaji miti limefanyika katika Kiwanja cha CCM Kata ya Itenka na Kituo cha afya Itenka.

Mnyere ‘’anasema Jumuiya hii inasimamamia Mazingira,Elimu na Malezi hivyo jumuiya hii ni Jumuiya mama katika chama chetu,,

Mjumbe wa Halmashauri kuu ya chama cha Mapinduzi CCM Mkoa wa Katavi Girbert Samnpa akipanda mti katika kiwanja kinachomilikiwa na chama cha Mpainduzi CCM Kata ya Itenka.

Uzinduzi huo wa Wiki ya Jumuiya ya wazazi ya Chama Cha Mapinduzi CCM katika mkoa wa Katavi imeenda sambamba na Upandaji wa miti katika Kiwanja Kinachomilikiwa na Chama cha Mapinduzi CCM Kata ya Itenka,Kufanya Matendo ya Huruma kwa kuwajulia hali wagojwa katika Kituo cha Afya Itenka pamoja na kupanda miti kwenye Kituo hicho.

Sherehe hizo za Maadhimisho ya Wiki ya Jumuiya ya Wazazi ya Chama cha Mapinduzi CCM itahitimishwa kitaifa katika mkoa wa Manyara.

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages