MKUU WA MKOA AONYA DISKO TOTO SHEREHE ZA PASAKA

 

Mkuu wa Mkoa wa Katavi,Mwanamvua Mrindoko akizungumnza na waandishi wa Habari ofisini kwake na kutuma salamu za Pasaka kwa wananchi wa mkoa wa Katavi.
Na Paul Mathias- Katavi
Wananchi katika mkoa wa Katavi wameaswa kuchukua tahadhari ya ulinzi katika familia katika kipindi hiki cha kuelekea Sikukuu ya Pasaka.
Waandishi wa habari mkoa wa katavi wakiwa katika majukumu yao wakati mkuu wa mkoa wa katavi akitoa salamu za Pasaka kwa wananchi wa mkoa wa katavi.

Wananchi katika mkoa wa Katavi wameaswa kuchukua tahadhari ya ulinzi katika familia katika kipindi hiki cha kuelekea Sikukuu ya Pasaka.

Akizungumnza na waandishi wa habari ofisini kwake wakati akitoa salamu za Pasaka Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko amesema wananchi wasiondoke Majumbani kwao na kuacha nyumba ikiwa haina watu ili kuepusha mwanya wa Matendo ya uharifu ambayo hufanywa katika vipindi vya sikukuu.

‘’tusiondoke kwenda kusherekea na kuacha Nyumba zetu zikiwa hazina aina yeyote ya ulinzi kwakuwa kuna baadhi ya watu hutumia mwanya wa sikukuu hizi kufanya vitendo vya wizi’’amesema Mrindoko.

Amesema kuwa wazazi na walezi wawe walinzi kwa watoto wao ili kuepusha watoto hao kupotea.

Katika hatua nyingine amepiga marufuku watoto kwenda katika Maeneo ya Starehe kwenye Mziki wa watoto maalufu kama [Disko toto ] kwa ni katika vipindi mbambali kulisha wahi kutokea maafa yanayotokana na Mziki kwa watoto [Disko toto ]kwenye baadhi ya maeneo hapa nchini hivyo nilazima kuchukua tahadhari.

‘’tulishawahi kushuhudia Maafa kutokana na Mziki wa watoto, watoto wetu washerekee siku kuu hii katika maeneo ya wazi ambayo yanatambulika ili kuepusha maafa yanayoweza kujitokeza’’

Ametoa tahadhari kwa watumiaji wa vyombo vya  moto  kuzingatia sheria za usalama barabarani ili kuepusha ajali amabazo zinaweza kujitokeza katika kipindi hiki cha siku kuu ya Pasaka.

Amewahakikishia wananchi kuwa mkoa umejipanga kuimalisha ulinzi katika maaeneo ya Ibaada wakati wa sikukuu ya Pasaka

Amewatakia wananchi wote wa mkoa wa Katavi kusherekea siku kuu ya Pasaka kwa amani na utulivu na mkoa wa Katavi upo salama

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages