Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko akimkabidhi Mwenyekiti wa Kashaulili Amcos Charles Ngonyani Mashine ya kuchakata chakula cha mifugo. |
Na Walter Mguluchuma -Katavi
Serikali ya Mkoa wa Katavi imewahimiza wawekezaji wa ndani na nje wa mkoa huo kufungua viwanda vya kuchakata mazao ya mifungo ambapo vitachangia ukuaji wa uchumi pamoja nakumarisha Lishe kwa wananchi.
Wito huu umetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mwanamvua
Mrindoko wakati alipokuwa akikabidhi vifaa vya uchakataji wa mazao
ya mifugo na vifaa vya kuhifadhia mifugo vilivyotoewa na Rais Dkt
Samia Suluhu Hassani Chama cha ushirika cha Maziwa cha
Kashaulili .Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko akimkabidhi cheti cha usajili wa Kashaulili Amcos Charles Ngonyani.
Amebainisha kuwa Mkoa wa Katavi kutokana na sensa ya
mifugo ya Mwaka 2022 Mkoa huu unamifugo ya kutosha unajumla ya
mifugo zaidi ya laki nane kwamaana hiyo viwanda vya kuchakata mazao
ya mifugo ninahitajika sana kutokana kuongezeka kwa mifugo kwa kasi kubwa
kwani kwa sasa Mkoa unakisiwa kuwa na mifugo zaidi ya milioni moja .
Mrindoko amewataka wananchi wa Mkoa huu na nje ya Mkoa
huu kufungua viwanda vya kuchakata mazao ya mifugo kwani wawekezaji sio
lazima wawe ni wazungu peke yao .
Amebainisha kuwa Mkoa wa Katavi unahitaji zaidi
viwanda vya chakata mazao ya mifugo kuanzia nyama
ngozi na maziwa hivyo chama hicho cha Ushirika wa
maziwa cha Kashaulili wahakikishe wanaanzisha kiwanda cha kuchakata
mifugo .
Kutokana na hali hiyo Serikali ipo tayari kuendelea kuimarisha
sekta ya mifugo kupitia mipango ya Rais Dkt Samia Suluhu Hassan hivyo
wanajitaji viwanda kwenye Mkoa huu
Katibu Tawala wa Mkoa wa Katavi Abbas Rugwa
amesema anaamini kuwa vifaa hivyo walivyokabidhiwa vitawafanya hapo baada
kuwa na vifaa vingi zaidi ya hivyo walivyopewa .
Ameeleza kuwa huo ni mwanzo mzuri ambao utawafanya
watu wengine waweze kuvutika na kuanzisha viwanda vingine vya
kuchakata mazao ya mifugo kwenye Mkoa huu kutokana na mahitaji yalipo .
Mwenyekiti wa ushirika wa maziwa wa chama cha
Kashaulili Charles Ngonyani amesema kuwa vifaa hivyo walivyokabidhiwa
vitawafanya kuweza kuwa na uwakika wa kupata maziwa yenye
ubora na yaliyosalama zaidi .
Pia wanauhakika mifugo yao kuanzia sasa haitakuwa na
shida ya kula chakula ambacho ambacho majani yake ambayo ni magumu
kutoka na kuwepo kwa mashine ya kuchakata chakula waliopewa