POLISI KATAVI YAONYA UHARIFU EID EL FITRI

 

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Katavi [ACP] Ali Makame Hamadi akizungumnza na waandishi wa habari mkoa wa katavi ofisini kwake kuhusu mipango ya jeshi hilo kuimalisha ulinzi kuelekea sikukuu ya Eid el Fitri

Na Paul Mathias
Katavi
Jeshi la polisi mkoa wa Katavi limewaonya vikali wale wote wameajiandaa kufanya uharifu kuelekee siku kuu ya Eid el Fitri.
Kamanda wa polisi mkoa wa Katavi Ali Hamad akizungumnza na waandishi wa habari ofisini kwake amesema jeshi hilo limejiandaa kuimalisha ulinzi na usalama na kukabiliana na iana yeyote ya uharifu utakao jitokeza.

‘’Sisi kama jeshi la polisi tumeanjiandaa kuimalisha ulinzi wa Rai na mali zao kuelekea kipindi hiki cha Siku Kuu ya Eaid el Fitri niwahakikishie wananchi wa mkoa wa Katavi tutafanya doria za kila aina ili kuhakikisha usalama kwenye siku kuu hii amesema Makame’’

Katika hatua nyingine kamanda Makame amewaonya watumiaji wa vyombo vya moto kuelekea sikukuu ya Eid el Fitri kuendesha vyombo vyao vya moto kwa kuzingatia sheria za usalama barabarani.

‘’tuwaonye tena Madreva wa vyombo vyamoto kutopakia uzito hasa Pikikipiki kutobeba Abiria zaidi ya mmoja hatutasita kuwakamata na kuwapeleka mahakamani wale wote watakao bainika na makosa hayo’’ amesema Makame.

Pamoja na hayo amewaomba wazazi kuwamakini na watoto wao kwa kutowaruhusu kwenda katika Maeneo ya starehe kwa kulinda usalama wao ikiwa ni sehemu ya kukabiliana na matukio yanayoweza kujitokeza yenye sura ya upotevu wa watoto na kufanyiwa ukatili na unyanyasaji.

‘’Nimalufuku kumbi hizi za starehe kuluhusu watoto wenye umri chini ya miaka 18 kuingia tutapita na kujilidhisha kwenye kumbi hizi tukibaini kuna watoto wenye chini ya umri wa miaka 18 tutakukamata na kukupeleka katika vyombo vya sheria’’ amesisitiza Makame

Pamoja na hayo kamanda amewaomba wanachi kuendelea kushirikiana na jeshi la polisi mkoa wa Katavi kwa kutoa taarifa za waharifu na uharifu ili kuendelea kuimalisha ulinzi wa Raia na mali zao.

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages