Kamanda wa polisi mkoa wa Katavi,Ali Hamad Makame akizungumnza na waandishi wa habari ofisi kwake kuhusu Matukio mbalimbali katika mkoa wa katavi. |
Na Walter Mguluchuma .
Katavi .
Jeshi la Polisi
Mkoa wa Katavi limewakamata watu wawili kwa tuhuma za matukio
mbalimbali ya kujihusishs na wizi wa pipiki kwenye maeneo
mbali mbali ya wizi wa pikipiki uliokuwa unatokea kwenye Mkoa wa Katavi .
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Katavi Ali Makame Hamad amewambia wandishi wa Habari kuwa watuhumiwa hao wamekamatwa kufutia msako mkali uliofanywa na jeshi la polisi baada ya kuwa wamepata taarifa ya watu hao kujihusisha na matukio hayo ya wizi .
Kamanda amewataja
watuhumiwa hao walio kamatwa na jeshi la polisi kuwa ni Benedict
Gasper(32) mkazi wa Mtaa wa Majengo Manispaa ya Mpanda na
Fideris Ruben boda boda Mtaa wa mtaa wa Airtel Manispaa
ya Mpanda .
Amesema kuwa
katika msako huo watuhumiwa hao wamekamatwa kwa kujihusisha na wizi wa
pikipiki mbili zenye Namba za usajiri MC 520 CCK na
pikipiki yenye Nambza za usajiri MC128DFU mali
ya Robbert Ismail .
Watuhumiwa hao baada ya kuwa wamekamatwa walihojiwa na jeshi la polisi na baada ya mahojiano na upelelezi kukamilika watuhumiwa hao wote wawili wamefikishwa Mahakamani na wameisha somewa mashitaka .