MAHAKAMA YA MWANZO MPANDA YAUNGUA MOTO

 

Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Shanwe Mustapha Mkimasa akiwa katika jengo la mahakama ya Mwanzo Shanwe Manispaa ya Mpanda lililoungua moto.

Na Paul Mathias.

Katavi.

Mahakama ya Mwanzo Shanwe iliyopo Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda mkoa wa Katavi imeungua moto usiku wa kuamkia leo.

Sehemu ya jengo la mahakama ya Mwanzo Shanwe lilivyo ungua moto

Mahakama ya Mwanzo Shanwe iliyopo Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda mkoa wa Katavi imeungua moto usiku wa kuamkia leo.

Mwenyekiti wa Serikali mtaa wa Shanwe Mustapha Mkimasa amesema kuwa amepata taarifa ya kuungua kwa jingo hilo kutoka kwa Mtoto wake.

‘’Mimi nimeambiwa tu mtoto wangu akitoka kwenda uani akaniambia Baba mahakamani pale kuna moto mkubwa unawaka pale nikasogea hadi eneo hilo kukuta moto unaendelea kuwaka  ’’ amesema Mkimasa

Ameeleza kuwa baada ya kufika eneo hilo alichukua jukumu la kutoa taarifa kwenye jeshi la zimamoto na uokoaji wakati huo wananchi walikuwa wanaendelea kuuzima moto huo.

‘’hatua ya kwanza niliyochukua mimi ni kuwapa taarifa watu wa zima moto na jeshi la polisi zimamoto walifika na wananchi walifika hapa kwa wingi tumefanya jitihada sana za kuzima moto huu kwenye hili’’

Amebainisha jeshi la zimamoto na uokoaji walipofika katika eneo la tukio walianza mara moja kuuzima moto huo kwa ushirikiano mkubwa na wananchi walifika kwenye eneo la tukio hilo.

Mustapha amesema kwa namna ya moto huo ulio ugunza jingo hilo kuna nyaraka nyingi za serikali zitakuwa zimeungua.

‘’Kwanguvu yetu tumewajibika akina baba akina mama tumesaidia sana hili jengo lakini inaonekana nyaraka nyingi za serikali zimeungua amesema ‘’Mustapha

Kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa wa Katavi ikiongozwa na mkuu wa mkoa wa Katavi mwanamvua Mrindoko imefika eneo la tukio na uchunguzi wa tukio hilo ukiwa unaendelea.

Kwa habari zaidi endelea kutembelea ukurasa wetu wa 

kataviclub.blogspot.com.

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages