MANISPAA YA MPANDA LAWAMANI KUSHIDWA KUSIMAMIA USAFI

 

Muonekano wa Nyasi Ndefu ambazo hazijafyekwa  katika eneo la ukumbi wa Mikutano  wa Idara ya Maji Manispaa ya Mpanda Mkoa wa Katavi

Na Walter Mguluchuma

   Mpanda .

Baadhi ya Wananchi wa Manispaa  Mkoani Katavi  wameilalamikia Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda kwa kushindwa kusimamia usafi wa mji hali ambayo imewafanya kuhofia hali ya usalama wao kwa kushindwa kusimamia usafi na Kuluhusu kuwepo kwa nyasi ndefu iliwepo eneo la nyuma ya ukumbi wa mikutano wa Idara ya Maji unao milikiwa na Halmashauri ya  Wilaya ya Tanganyika .

Muonekano wa Nyasi Eneo la Nyuma ya ukumbi wa Mikutano wa Idara ya Maji Mpanda Mjini

Baadhi ya Wananchi wa Manispaa  Mkoani Katavi  wameilalamikia Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda kwa kushindwa kusimamia usafi wa mji hali ambayo imewafanya kuhofia hali ya usalama wao kwa kushindwa kusimamia usafi na Kuluhusu kuwepo kwa nyasi ndefu iliwepo eneo la nyuma ya ukumbi wa mikutano wa Idara ya Maji unao milikiwa na Halmashauri ya  Wilaya ya Tanganyika .

Mmmoja wa wananchi hao  Peter Michael amesema kuwa  wamekuwa wakipita kwenye eneo hilo nyuma ya ukumbi huu hata mchana huku akiwa na hofu ya usalama wake kutokana na kichaka kikubwa cha  nyasi kilichopo maana mpaka kinaziba barabara .

Amesema  licha  ya kuwa eneo hilo lipo katika  kati ya  Manispaa ya Mpanda  lakini mtu unaweza  ukakabwa hata mchana kama muda huu unaopita hakutakuwa na mtu mwingine anae pita  kwenye eneo .

Maiko Msanja amesema kuwa  yeye huwa anashangaa kila anappopita kwenye eneo hilo na kuona  likiwa na kichaka tena kati kati ya mji  utadhani hakuna mamlaka ambazo zina wajibu wa kusimamia mazingira ya usafi .

Amebainisha kuwa mbaya zaidi ikitokea umepita usiku kwenye eneo hilo  linakuwa linatisha sana utadhani kama vile umefika eneo la msitu wa Ntongwe  Magharibi au kwenye Hifadhi ya Taifa ya Katavi .

Doto Siveseter Mkazi wa Mtaa wa  Nyerere Kata ya Kawajense amesema kuwa wao wananchi wamekuwa wakitozwa faini pindi maeneo yao yanapokuwa ni machafu  sasa inakuaje kwenye maeneo kama hayo ya ukumbi wa maji yapo kati kati ya mji  halafu yanakuwa  yanatishia usalama wa watu na wahusika wanaona .

Alitowa mfano  wa  kuwepo na tabia ya kwenye  maeneo yanayomilikiwa kiwa  na Serikali kuwa kama  yametelekezwa ni kama siku za nyuma aliwahi kupita kwenye nyumba aliyokuwa akiishi     Mkuu wa Wilaya ya Tanganyika  Salehe Mhando  iko katikati maeneo ya  Kotazi alivyoiona  ni kama imetekelezwa kutoka na  mazingira  yalipo kwenye eneo hilo.

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages