VIJANA WAASWA KUCHANGAMKIA FURSA YA MIRADI TANRODS

Mkurugenzi wa Jukwa la kuwakomboa vijana Mkoa wa Katavi Saimon Jonh akimkabidhi cheti cha Shukurani Meneja wa Tanrods Mkoa wa Katavi Mhandisi Martin Mwakabende ikiwa ni sehemu ya kutambua ushirikiano unaotolewa na Tanrods kwa jukwaa la Vijana.

Vijana katika mkoa wa Katavi wameaswa kuchangamkia Fursa za Vijana zinazo tolewa na serikali kwa kuunda umoja na kusajiliwa kisheria  na Bodi ya wakandarasi ili waweze kupata kazi ndogo ndogo zinazotolewa na serikali kupitia wakala wa Barabara Tanrods Katika mkoa wa Katavi.

Viongozi wa Jukwa la Kuwakomboa Vinaja mkoa wa Katavi,Saimon Jonh [Kulia] na Paul Mathias[Kushoto] wakiwa katika mazungumzo na Meneja wa Tanrods Mkoa wa Katavi Martin Mwakabende kuhusu fursa za vijana.

Vijana katika mkoa wa Katavi wameaswa kuchangamkia Fursa za Vijana zinazo tolewa na serikali kwa kuunda umoja na kusajiliwa kisheria  na Bodi ya wakandarasi ili waweze kupata kazi ndogo ndogo zinazotolewa na serikali kupitia wakala wa Barabara Tanrods Katika mkoa wa Katavi.

Ushauri huo umetolewa na Meneja wa Tanrods Mkoa wa Katavi Mhandisi Martin Mwakabende alipotembelewa na Viongozi wa Jukwaa la Vijana Mkoa wa Katavi Ofisini kwake leo

Mwakabende amesema katika sera ya Wizara ya Ujenzi kwenye Bajeti za Mkoa Asilmia 30 Hutegwa kwaajili ya Makundi Maalamu ambayo ni Wazee,Wanawake ,walemavu na Vijana ambapo makundi haya huyalazimu kusajiliwa katika Bodi ya Wakandarasi na baadae hatua zingine za kuomba miradi hiyo hufuata.

‘’hii ni Sera ya wizara ya Ujenzi katika Bajeti inayopangwa na mkoa Asilimia 30 inabidi zitengwe kwaajili ya makundi maalumu kuna kundi la wazee,kundi la Vijana,kundi la akina mama na kundi la wenye ulemavu makundi haya yote yanaweza kuunda umoja wao na Kusajiliwa katika Bodi ya Wakandarasi hapo sasa wanakuwa na kazi ya kuomba kazi za kufanya’’amesema Mwakabende

Amesema katika Mwaka wa fedha  ujao Tanroads katika mkoa wa Katavi wanatalajia kuwa na kazi ndogo ndogo 16 ambapo zitahusisha makundi hayo kwa kuangalia Mahitaji ya kazi kulingana na uhitaji katika miradi husika.

‘’katika mwaka wa Fedha ujao tunategemea kuwa na kazi ndogo ndogo 16 nahizi tumejaribu kuziweka katika maeneo tofautitofauti tumetenga kazi Fulani zitafanywa na kundi la vijana kwa mfano mwaka huu tumetenga aina tatu za kazi zitakazofanywa na Makundi ya Vijana hii ni fursa kwa Vikundi vilivyosajiliwa na bodi ya wakandarasi katika mkoa wa Katavi kuingia katika Mifumo hususani Taneps kuangalia kazi zilizotangwa na Tanroads mkoa wa Katavi’’

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Jukwaa la kuwakomboa vijana Mkoa wa Katavi Saimon Jonh amesema kuwa adhima ujio wa viongozi wa Jukwaa la vijana katika ofisi za Tanrods Katavi ni kutambua mchango wa Tanrods namna inavyoshrikiana na na jukwaa la vijana katika kushirki kazi ndogo ndogo za uelimishaji wa jamii unaofaywa  na jukwaa la vijana kwa wananchi kwenye maeneo ambayo miradi hiyo ya Tanrods inapojengwa.

‘’sisi kama jukwaa la Vijana mkoa wa Katavi tunashukuru namna ofisi yako imekuwa ikitupa ushirikiano katika majukumu yetu hasa kwenye miradi hii midogo midogo ambayo tumekuwa tukiipata kwa kutoa elimu ya maambukizi ya Virusi vya ukimwi kwenye baadhi ya Miradi hapa mkoani kwetu’’amesema Saimon

Katika hatua nyingine Jukwaa la kuwakomboa vijana mkoa wa Katavi limetoa cheti cha Shukurani Kwa ofisi ya Tanrods Mkoa wa Katavi kwa kutambua mchango unaotolewa na ofisi hiyo katika kwenye uelimishaji wa jamii kuhusu VVU na Ukimwi kwenye baadhi ya maeneo ambayo miradi mbalimbali ya ujenzi wa Barabara hufanyika.

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages