''WAUGUZI NI KADA MHIMU'' ASEMA RC MRINDOKO

Mkuu wa Mkoa wa Katavi,Mwanamvua Mrindoko akiwahutubia wananchi katika kilele cha Siku ya wauguzi duniani yaliyofanyika kimkoa katika viwanja vya Shule ya Msingi Kashaulili

Na Paul Mathias

Katavi,

Wauguzi katika Mkoa wa Katavi wameobwa kuendelea kufanya kazi kwa Weledi kwa kuzingatia miiko ya Taaluma kwani wao ni Sehemu mhimu kwa kuokoa Uhai kwa Binadamu katika kazi zao.

Baadhi ya Wauguzi katika halmashauri ya Manispaa ya Mpanda wakiwa katika kilele cha Maadhimisho ya siku ya Wauguzi Duniani

Akiwahutubia wananchi wa Mkoa wa Katavi kwenye kilele cha siku ya Wauguzi Duniani yaliyofanyika kimkoa katika viwanja vya Shule ya Msingi Kashaulili Manispaa ya  Mpanda , Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko amesema kada ya wauguzi ina umuhimu Mkubwa jamii kwakuwa wao wamekuwa sehemu ya kuponya maradhi kwa mwanadamu yanapo Mpata.

 ‘’baada ya Daktari kumaliza kazi yake ya kuandika ni namna gani apate Matibabu anaendelea nae kwenye hatua za mbele kule ni Muuguzi kwa maana hiyo Sekta hii kada hii ya Wauguzi wa aina zote ni mhimu sana katika sekta ya Afya’’ amesema Mrindoko

Amesema kazi kubwa inayofanywa na wauguzi kwa kuwaangali wagojwa kwa upole ni sehemu kuhakikisha wanafanya kazi yao kwa kuzingatia maadili na weledi kwa Wagojwa wanaowahudumia kwenye Zahanati,Vituo vya afya,Pamoja na hospitali ambapo kwa mwaka wa fedha wa 2022/2023 Mkoa wa Katavi ulipatiwa wafanya kazi 290 kwa mkoa wa katavi.

Katibu tawala Mkoa wa Katavi Abas Rugwa akipata huduma kwenye moja ya Banda la kutolea huduma za afya kwenye kilele cha siku ya wauguzi Duniani yaliyofanyika kimkoa katika viwanja vya Shule ya Msingi Kashaulili.

‘’niwapongeze sana tuendelee kuthamini kazi inayofanywa na wauguzi kwakuzingatia kuwa kundi hili ni kundi kubwa kwenye sekta ya utoaji wa huduma za afya kwenye hospitali zetu’’

Katika hatua nyingine Mkuu huyo wa Mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko amsema kumekuwa na ongezeko la Vituo vya kutoa huduma za upasuaji kwa  mama wajawazito kutoka 3 mwaka 2017 na kufikia 12 kwa mwaka 2023.

Awali akisoma Risala kwa Mkuu wa Mkoa Mratibu wa TANNA Mkoa wa Katavi Augusta Thomas amesema kuwa kwa sasa mkoa wa Katavi unawauguzi wapatao 403 waliosajiliwa idadi ambayo haiendani na uhalisia wa Miundombinu ya afya iliyopo na kuimba serikali kuendelea kuwekeza nguvu kazi katika Rasilimali watu hususani waauguzi.

Mkuu wa Mkoa wa Katavi,Mwanamvua Mrindoko akimkabidhi Cheti cha Pongezi Mganga Mfawidhi wa Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda Paul Swakala kwenye maadhimisho ya kilele cha siku ya wauguzi Duniani yaliyofanyika kimkoa katika viwanja vya shule ya Msingi kashaulili.

Augusta ameipongeza Serikali kwa kuendelea kuwaboreshea Miundombinu ya kufanyia kazi ikiwemo hospitali,pamoja n vituo vya afya.

Kwa upande wake Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Manispaa ya Mpanda Paul Swakala amesema kuwa pamoja uchache wa watumishi waliopo katika hospitali hiyo wafanyakazi hao wamekuwa wakifanya kazi zao kwa kujituma nakwa weledi wa hali ya juu.

Maadhimisho ya kilele cha siku ya wauguzi Duniani  2023  yamebebwa na kaulimbiu inayosema WAUGUZI WETU MSTAKABALI WA MAISHA YETU.

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages