TAKUKURU KATAVI KUIMARISHA MAPAMBANO YA RUSHWA

Mkuu wa Takukuru Mkoa wa Katavi Faustine Maijo akitoa taarifa kwa waandishi wa Habari ya utendaji kazi wa taasisi hiyo kwa kipindi cha Mwezi January March

Na Walter Mguluchuma 

Katavi

Katavi Taasisi ya  Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Katavi  kwa kipindi cha robo   mwaka  ya  Aprili  hadi june 2023  inatarajia  kuimarisha juhudi  za kuzuia  Rushwa  kwa kukagua miradi  ya maendeleo  kwa kuwahamasisha  wananchi  na kutoa elumu  ya ushiriki  wa wananchi kuzuia Rushwa 

Waandishi wa habari mkoa wa Katavi wakiendelea na Majukumu yao wakati mkuu wa Takukuru Mkoa wa Katavi Faustine Maijo alipotoa taarifa ya utendaji kazi kwa mwezi January hadi March.

Katavi Taasisi ya  Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Katavi  kwa kipindi cha robo   mwaka  ya  Aprili  hadi june 2023  inatarajia  kuimarisha juhudi  za kuzuia  Rushwa  kwa kukagua miradi  ya maendeleo  kwa kuwahamasisha  wananchi  na kutoa elumu  ya ushiriki  wa wananchi kuzuia Rushwa 

Hayo yamebainishwa  na Mkuu wa Takukuru Mkoa wa Katavi  Faustine  Maijo  wakati akitowa taarifa   ya utekelezaji wa Taasisi hiyo kwa kipindi cha miezi mitatu ya kuanzia    mwezi  Machi hadi   mwezi june 2023.

Amesema  Takukuru Mkoa wa Katavi  inatarajia  katika kipindi  hicho  kuimaimarisha  juhudi za Kuzuia  Rushwa  kwa kukagua miradi  ya maendeleo ,kuimarisha  na kutoa  elimu  ya kushiriki  wananchi  katika kuzuia  Rushwa  kupitia   nyenzo  mbalimbali .

Pia  watatumia  uelimishaji  katika  mikusanyiko   mbalimbali kwa kutumia  mwongozo  wa TAKUKURU  RAFIKI  na pia wataendelea  kufatilia  kwa karibu  fedha zote  zinazotolewa na Serikali  zikiwepo  fedha  za  mradi  wa Boost ili  kuhakikisha  zinatumika  kama  ilivyokusudiwa  na kuonyesha  thamani ya fedha .

Vilevile wataendelea  kufatilia  makusanyo  na  uwasilishaji  wa mapato  yanayotokana  na mashine  za POS  na kuchukua  hatua  stahiki  kwa wale  watakaobainika  kufuja  mali za umma  ikiwemo wanao tumia fedha mbichi .

Maijo  ameeleza kuwa  Takukuru  kwenye kipindi hicho  watafanya  warsha  na wadau  kujadili  matokeo  ya uchambuzi  za mifumo  zilizokamilika  ili  kuweka  maazimio  ya namna bora  ya kuziba  mapungufu  yaliyobainishwa  katika uchambuzi  hizo .

Aidha watafanya  uchunguzi  wa  haraka  kwa taarifa zote  zitakazopokelewa  na ambazo  uchunguzi  wake  unaendelea  ili ziweze kukamilika  mapema .

Kuhusu   malalamiko ya Rushwa    Takukuru Mkoa wa Katavi wameendelea  kupokea  malalamiko  yanayohusiana na  vitendo vya Rushwa  ambapo katika kipindi   hicho  wameweza kupokea  malalamiko  51 kati ya malalamiko hayo  malalamiko  35 yalikuwa yanahusu Rushwa  na malalamiko 16 hayakuwa yanahusiana na Rushwa .

Maijo ametowa wito  kwa wananchi  wote wa Mkoa wa Katavi  kutowa  taarifa  za  vitendo vya Rushwa pindi  vinapokuwa  vimetokea .

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages