UJENZI WA BARABARA YA LAMI MPANDA -KAREMA WANUKIA


Naibu katibu  Mkuu wa Wizara ya Ujenzi na uchukuzi anaeshughulikia Sekta ya Ujenzi Ludovick Nduhye [wapili kushoto ] akiwa na Meneja wa Tanroads Mkoa wa Katavi Mhandisi Martin Mwakabende wa [kwanza Kushoto] walipotembelea eneo la Bandari ya Karema itakapoishia Barabara ya lami ambayo ujenzi wake upo mbioni kuanza.
Na  Walter Mguluchuma

   Katavi

Naibu  Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi anae shughulikia Sekta ya Ujenzi  Ludovick  Nduhye  amefanya ziara ya kutembelea barabara ya kutoka Mpanda kwenda  kwenye Bandari ya Karema ambayo inatarajiwa kuanza kujengwa hivi karibuni mwaka huu kwa kiwango cha lami .

Meneja wa Tanroads Mkoa wa Katavi Mhandisi Martin Mwakabende akimwelezea Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi anaeshughulikia Sekta ya Ujenzi Ludovick Nduhye akielezewa baadhi ya changamoto iliyopo kwa sasa Kwenye Barabara ya Mpanda Karema ikiwemo wakulima wa zao la Mpunga kulima pembezoni mwa barabara hiyo na kusabisha uharibifu.
                                                                                                                                                      
Naibu  Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi anae shughulikia Sekta ya Ujenzi  Ludovick  Nduhye  amefanya ziara ya kutembelea barabara ya kutoka Mpanda kwenda  kwenye Bandari ya Karema ambayo inatarajiwa kuanza kujengwa hivi karibuni mwaka huu kwa kiwango cha lami .

Akizungumza wakati akiwa kwenye  Karema wakati wa ziara yake hiyo Nduhye amesemakuwa lengo la ziara hiyo ni kuangalia barabara hiyo inayotarajiwa kujengwa kwa kiwango mahali inapo anzia na inapoishia .

Amebainisha kuwa lengo la Serikali ya awamu ya sita   imepanga  kuboresha miundo mbinu mbailimbali ya    mawasiliano ya barabara katika kuhakikisha inakuza uchumi wa nchi na kwa watanzania kwa ujula .

Amesema    ujenzi wa barabara hiyo ni muhimu kwa Nchi ya Tanzania na Nchi ya Kongo kwani wanategemea  mizigo ya kwenda kwenye Nchi ya Kongo itakuwa inasafirishwa kwa barabara hiyo hadi kwenye bandari ya Karema kwa ajiri ya kusafirishia mizigo na abiria wan chi hizi mbili .

Meneja wa Tanroads Mkoa wa Katavi Mwandisi Martin Mwakabende ameeleza kuwa   taratibu za kuwapata wakandarasi watakao tengeneza barabara hiyo tayari umeisha anza kwa kutangaza tenda  ya kandarasi hiyo .

Amefafanua kuwa  zabuni za kuwapata  wakandasi wa barabara hiyo utafanyika tarehe 30 ya mwezi huu wa tano ambapo  ndio itakuwa siku  ya kufunga  zabini zote za maombi  na  kuruhusu  uchambuzi wa tenda zitakazokuwa zimeombwa na makampuni mbalimbali ya ujenzi wa barabara ambapo ujenzi huo utachukua muda wa miezi 24..

Moja ya maeneo ya barabara ya Kagwira Karema iliyokuwa imeharibiwa na wakulima wa zao la Mpunga wanao lima kandokando ya barabara hiyo na kufungulia maji kuelekea Barabarani hali ambayo hupelekea uharibifu wa Barabara.

Mhandisi Mwakabende amesema kuwa ujenzi wa barabara hiyo umegawanywa katika sehemu mbili ambapo mkandarasi wa kwanza atatengeneza  barabara kuanzia  Kagwira hadi  Kasekese  kwa  umbali wa kilometa 54.144 na  Kasekese Karema yenye umbali wa kilometa  59.15.

Amesema kuwa barabara hiyo imekuwa na changamoto  kwenye baadhi ya maeneo hasa wakati wa kipindi cha masika  kwenye maeneo  wanayolima  mpunga  bembeni mwa barabara wananchi wamekuwa wakifungulia maji  kwenye majaruba ya mpunga na  kuyaelekeza barabarani na kusababisha uharibifu wa barabara .

Nae  Paroko wa Kanisa Katoliki  parokia ya Karema  Padri Nikodems Kiyumana amesema kuwa  kujengwa kwa barabara hiyo kwa kiwango cha lami kutaongeza furusa kwa wananchi za kiuchumi kuanzia kwa mfanya biashara mdogo hadi mkubwa .

Pia kutafanya watu wawe na usafiri wa uhakika wa kusafirisha mizigo yao hadi kwenye Bandari ya Karema na kuisafirisha kwenda Nchi  jirani ya Kongo na pia mizigo ya kutoka Kongo itasafirishwa kwa urahisi hadi kwenda kwenye bandari ya Daress salaam kwa kupitia barabara hiyo .

Padri  Kiyumana ameeleza pia wageni wataongezeka  hivyo itakuwa ni furusa kwa wafanya biashara wa nyumba za kulala wageni na pia tutapata furusa ya kujifunza    mambo mbali mbali  yakuleta maendeleo kutoka kwa wageni hao .

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages