UDESO WAKAMIRISHA MAFUNZO YA UFATILIAJI MIRADI VIJIJINI


Halima Kitumba Msajili Msaidizi wa Mashirika yasiyo kuwa ya Kiserikali Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika mkoa wa Katavi akitoa neno wakati akifunga mafunzo ya Siku Tano kwa viongozi wa kamati za Pets Kutoka Vijiji vya Lugonesi na Kasekese yaliyoandaliwa na Taasisi ya UDESO.

Na Walter Mguluchuma

   Katavi .

Wajumbe wa  Kamati  za PETS  za kutoka kwenye Vijiji  vya Kasekese na Lugonesi  vilivyopo katika Wilaya ya Tanganyika Mkoani Katavi wamepatiwa  mafunzo ya siku tano yaliyoandaliwa na Shirika lisilo la Kiserikali la Usevya Development Society [UDESO]  mafunzo hayo kwaajili  ya kuwajengea uwezo ili kusimamia  rasilimali na miradi ya Maendeleo .

Mkurugenzi wa Taasisi ya Usevya Development Society[ UDESO] Eden Wayimba akitoa neno kwa washiriki wa Mafunzo.

Wajumbe wa  Kamati  za PETS  za kutoka kwenye Vijiji  vya Kasekese na Lugonesi  vilivyopo katika Wilaya ya Tanganyika Mkoani Katavi wamepatiwa  mafunzo ya siku tano yaliyoandaliwa na Shirika lisilo la Kiserikali la Usevya Development Society [UDESO]  mafunzo hayo kwaajili  ya kuwajengea uwezo ili kusimamia  rasilimali na miradi ya Maendeleo .

Mafunzo hayo ya siku tano yaliyowashirikisha wajumbe wa PETS  wa kutoka kwenye  vijiji  vya Logonesi na Kasekese yamefanyika katika ukumbi wa Mikutano wa Kichangani uliopo Manispaa ya Mpanda Mafunzo hayo yamefungwa na  Msajiri  Msaidizi wa  Mashirika  yasiyo ya Kiserikali  (TDC) wa  Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika  Halima Kitumba .

Kitumba akifunga mafunzo hayo amesema   washiriki wa mafunzo hayo yamewafanya wawe wa mfano  kwenye maeneo  mengine katika Halmashauri hiyo  kwa kuweza kuisaidia kupeleka mgao  wa  shughuli zote zinazo  husiana na miradi    na rasilimali kwenda kwa uswa.

  Amebainisha kuwa kabla ya kupatiwa mafunzo hayo  hapo nyuma ilikuwa ni tofauti  kwa kuwa wasahivi tayari wametambua haki zao na watakuwa na uwezo wa kwenda katika Halmashauri na  kuhoji haki za mgawanyo kwenye Kata  kuhusu mikopo   na miradi.

Kitumba amewasisitiza watihimu hao kutumia vizuri mafunzo hayo kwa kuhakikisha wanakwenda kwenye vijiji vingine na kuwapatia elimu kama ambayo wamepewa wao na mwisho wa siku  kamati zitakapokuwa hai kwenye vijiji vyote  kwani watakuwa pia na uwezo wa kuandaa mikutano ambayo itakuwa haija   fanyika kwenye vijiji vyao na kuhoji  bajeti za miradi mbalimbali ya maendeleo ingawa kwa sasa  wanaanza na miradi ya elimu .

Washiriki wa Mafunzo wakiwa katika picha ya Pamoja na Mkurugenzi wa UDESO na Msajili Msaidizi wa Mashirika yasiyo kuwa ya KiserikaliWilaya ya Tanganyika  Halima Kitumba .
Mwezeshaji wa mafunzo hayo wa kutoka   Jijini Arusha  Evance  Mvamila ameishukuru Halmashauri ya Tanganyika kwa kukubali  na  kupokea  programu ya uwajibikaji wa ngazi ya jamii ili jamii iweze kukuza  na kuendeleza  ushiriki wao  katika  shughuli za  maendeleo  katika swala zima  la kusimamia   rasilimali zote za umma zile ambazo zinatengwa  na kuelekezwa kwenye maeneo yao .

Amesema kuwa mafunzo   hayo yalikuwa yamejikita  kwenye maeneo makuu yafuatayo  wameangalia  dhama nzima ya  madaraka ya Serikali  ili  kumezesha mwananchi katika  ushiriki  nakusimamia  rasilimali zote za umma zinazopelekwa kwenye maeneo yao

Vilevile  wameangalia   dhana nzima ya utawala bora ni namna gani ambavyo wananchi   anapaswa kuwa sehemu ya  ushiriki wa sehemu  uhimizaji wa utawala  bora  kwa  kutambua  umuhimu wa ihimizaji wa utawala bora

Mkurugenz Mtendaji i wa  shirika lisilo la kiserikali la  Usevya  Development Sociaety(UDESO) Eden Wanyimba  amesema kuwa  mradi huu  katika Wilaya ya Tanganyika  unatekelezwa  kwa  kushirikiana UDESO  na Taasisi ya  WAJIBU .

Mradi huu  unatekelezwa  katika  vijiji hivyo  viwili katika Wilaya ya Tanganyika ulianza  mwezi machi 2023 na  unajikita zaidi katika kuangalia  utekelezaji  wa mapendekezo  yaliyotolewa  katika sekta ya elimu  ya awali   kupitia ripoti ya  mdhibiti  na mkaguzi Mkuu wa hesabu za Serikali CAG  Mwaka 2017.

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages