WAANDISHI KATAVI WAASWA KUANDIKA HABARI ZINAZO GUSA JAMII.



        Rais wa Umoja wa Klabu za waandishi wa habari Tanzania [UTPC] Deogratius Nsokolo akikabidhiwa cheti cha shukurani  kwa niaba ya UTPC kwa kuendelea kuwa wadau mhimu katika kazi mbalimbali za Katavi Press club.

Na Paul Mathia 

Katavi

Waandishi wa Habari katika Mkoa wa Katavi wameaswa kuendelea kuuhabarisha wa Mkoa wa Katavi kwa Mambo yanayofanywa na serikali katika sekta Mbalimbali ili wananchi wafahamu namna serikali inanyo sogeza huduma hizo kwa Wananchi.

Waandishi wa Habari katika Mkoa wa Katavi wameaswa kuendelea kuuhabarisha wa Mkoa wa Katavi kwa Mambo yanayofanywa na serikali katika sekta Mbalimbali ili wananchi wafahamu namna serikali inanyo sogeza huduma hizo kwa Wananchi.

Kauli hiyo imetolewa na Deodatus Kangu Afisa utumishi wa Manispaa ya Mpanda aliye Mwakilisha Msitahiki meya wa Manispaa ya Mpanda Haidary Sumry kwenye Maadhimisho ya uhuru wa vyombo vya habari yaliyofanyika katika ukumbi wa Katavi Resort Mpanda Mjini.

Kangu amesema kuwa Waandishi wa Habari ni vipasa sauti kwa umma kwa kuwafikia wananchi kwa ukubwa nakwa haraka zaidi kwa kuandika na kutangaza Mambo mbalimbali ambayo yamekuwa yakifanywa na serikali.

‘’nitoe shukurani sana kwenu waandishi wa Habari mmekuwa Vipasa sauti vya kuwafikia wananchi kwa ukubwa kwa mambo mengi sana ambayo serikali imekuwa ikiyafanya kwani siyo kila mmoja anaweza akayaona lakini huwatunaamini kwamba tukiwashirisha masuala yote hayo yanawafikia wananchi’’ amesema Kangu.

Amesema kazi ya uandishi wa habari huleta usitawi wa Jamii kupitia Habari zinazoandikwa na kuleta Mtizamo chanya kwenye Jamii ili kuongeza uwajibikaji kwa Mamlaka zilizopo ili wananchi waweze kupata huduma mbalimbali.

Katika hatua nyingine amewaomba waandishi wa Habari kupaza sauti zao kupitia Kalamu zao kujijkita kuandika habari zinazo husu tatizo la  unyanyasaji wa Kijinsia ikiwemo Ulawiti,Ushoga na Usagaji ambayo yamekuwa yanazungunmzwa sana katika jamii kwa sasa.

Mwenyekiti wa Klabu ya wandishi wa habari mkoa wa Katavi walter Mguluchuma amewaasa waandishi wa habari kufanya kazi zao kwa kuzingatia miiko ya uandishi wa habari

Kwa upande wake Rais wa Umoja wa Klabu za waandishi wa habari Tanzania Deogratius Nsokolo amesema kuwa anaishuru serikali ya awamu ya Sita kwa kukubali kuanza mchakato wa Ulekebishaji wa sheria za habari ambazo zilikuwa zinaoneka kuwa kandamizi kwa waanndishi wa habari hapa nchini.

‘’tunashuru sana awamu ya Sita ya Uongozi wa Rais Dk Samia Suluhu Hassan umekuja na Mabadiliko Makubwa sana sababu Mh Rais ameonyesha nia ya kuleta Maridhiano kwenye Sekta ya Habari ametuita tumekaa nae tumezungumnza nae tumejadiliana ni wapi ambapo sisi tunalalamika tumemweleza amaeneo ambayo tunayalalamikia ambayo tunaona yatatukandamiza’’ ameeleza Nsokolo

Nsonkolo amewakumbusha waandishi wa Habari kuendelea kuwa sauti ya watu wasio kuwa na sauti kwa kuibua changamoto zao ili serikali iweze kuwajibika kwa kupeleka huduma kwenye maeneo yenye changamoto za Maji,Elimu Afya na miundombinu.

‘’Sisi tunapaswa kuwa katikati kuwasemea wasiokuwa na sauti ili waheshimiwa wasikie waweze kukaa na kupanga Bajeti ii wanachi wenye uhitaji na huduma hizo wapatiwe huduma’’

Katika maadhimisho hayo ya Uhuru wa vyombo vya Habari waandishi wa Habari katika mkoa wa Katavi wamepata fursa ya kupatiwa elimu kuhusu habari zinazo husu Masuala ya kipolisi yaliyotolewa na maafisa kutoka jeshi la polisi mkoa wa katavi pamoja na Elimu kuhusu Madhara ya Rushwa yaliyotolewa na maafisa kutoka Taasisi ya kuzuia na kupambana na Rushwa Takukuru mkoa wa katavi.

Maadhimisho ya uhuru wa Vyombo vya habari kwa mwaka 2023 yamebebwa na kaulimbiu inayosema kuunda Mstakabali wa haki uhuru wa kujieleza kamakichocheo cha haki nyingine zote za Kibinadamu.

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages