CHADEMA YAPIGA HESABU UCHAGUZI SERIKALI ZA MITAA


Masanja Katambi Makamu mwenyekiti wa Chama cha Democrasia na Maendeleo CHADEMA kanda ya Magharibi akiwahutubia wanachama na wanacnchi wa chama Hicho katika kata ya Kawajense Manispaa ya Mpanda Mkoa wa Katavi.

Na Paul Mathias

Katavi,

Makamu mwenyekiti wa Chama cha Democrasia na maendeleo CHADEMA Kanda ya Magharibi Masanja Katambi amesema chama hicho kimeanza mikakati ya kujianda na uchaguzi wa Serikali za Mitaa mwakani.

Katibu wa chama cha Democrasia na maendeleo CHADEMA Mkoa wa Katavi Almasi Ntije akihutubia  mkuatano wa hadhara kata ya Kawajense Manispaa ya Mpanda mkoa wa Katavi

Makamu mwenyekiti wa Chama cha Democrasia na maendeleo CHADEMA Kanda ya Magharibi Masanja Katambi amesema chama hicho kimeanza mikakati ya kujianda na uchaguzi wa Serikali za Mitaa mwakani.

Akiwa hutubia wanachama wa Chama hicho katika Mkutano wa hadhara ulioandaliwa na Chama hicho katika kata ya Kawajense Manispaa ya Mpanda mkoa wa Katavi.

Masanja amesema tayari mikakati imeanza ya kuhakikisha Chama hicho Mkoa wa Katavi kinaenda kufanya vizuri katika uchaguzi huo wa Serikali za mitaa .

‘’Kama Chama tunaomba mtuunge mkono mwakani tunauchaguzi wa Vitongoji na Vijiji jiandikisheni kama wanachama wa Chadema ili mgombee kwenye mitaa,Mgombee kama wajumbe hii itaweka Msingi mzuri katika kuelekea uchaguzi mkuu mwaka 2025 ‘’amesema Masanja 

Kupitia mkutano huo Masanja ametangaza nia yake ya Kugombea Ubunge wa Jimbo la Mpanda mjini na kuwaomba wanachi na wanachama wa chama hicho kukiunga mkono katika kuelekea chaguzi zinazokuja katika siku za usoni.

‘’ningependa niwatangazie wana Kawajense moja ya wanachama wa CHADEMA waliotangaza nia ya kulitaka Jimbo hili la Mpanda Mjini katika uchaguzi ujao ni pamoja na mimi ila chama kitachuja ‘’

Kuhusu katiba mpya amesema kuwa Chama hicho kitaendelea kudai katiba mpya kupitia falsafa ya 255 ambayo Viongozi wajuu wa chama hicho wameendelea kuitambulisha kwa Watanzania kwa kuzunguka katika maeneo mbalimbali hapa nchini

Almasi Ntije Katibu wa Chama cha Democrasia na Maendeleo Chadema Mkoa wa Katavi amesikitishwa na baadhi ya Watendaji wa Kata na Mitaa kwa kutosoma Mapato na matumizi kwa wananchi  takwa ambalo nilakisheria

‘’mapato na matumizi yanayotokana na ushuru mbalimbali vyanzo mbalimbali wanatakiwa wawasomee mapato na matumizi kila baada ya miezi mitatu sasa kama hawafanyi hivyo niviongozi gani wasiotambua majukumu yao ya kisheria wangapi huwa wanawasomea mapato na matumizi ‘’amehoji Ntije  

Amesema watakuwa na mwendelezo wa mikutano ya hadhara kwa wananchi kwa lengo la kukijenga chama na kuwaamusha wananchi juu ya mambo Mbalimbali na kuwaasa kuendelea kujiandikisha na kupatiwa kadi za chama hicho kwenye Mfumo wa kisasa yaani electronic Systeam maalufu kama Chadema Digital zoezi ambalo linaendelea kwa sasa.

Mkutano huo umehudhuliwa na Viongozi mbalimbali wa chama hicho katika ngazi ya Mkoawa Katavi.

kwa habari zaidi tembelea ukuerasa wetu wa 

kataviclub.blogspot.com

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages