WAFANYA BIASHARA WA MAHINDI KATAVI WAIPA TANO SERIKALI


Wafanya biashara wa Mazao katika soko la Mahindi Mpanda hotel wakiwa katika shughuli zao za kila siku sokoni hapo

Na Paul Mathias 

Katavi.

Wafanya biasahara wa Mazao katika mkoa wa Katavi wamesema hatua ya Serikali ya mkoa wa katavi kupiga Marufuku wafanyabiashara kutoka nje ya nchi kwenda kununua Mazao vijijini itapunguza mfumko wa bei ya mazao.

shuhguli za kila siku za wafanyabiashara wa Mahindi Mpanda hotel Manispaa ya Mpanda mkoa wa Katavi

Wafanya biasahara wa Mazao katika mkoa wa Katavi wamesema hatua ya Serikali ya mkoa wa katavi kupiga Marufuku wafanyabiashara kutoka Nje ya nchi kwenda kununua Mazao vijijini itapunguza mfumko wa bei ya mazao.

Wafanya biashahara hao wamesema kuwa  Kitendo cha serikali ya mkoa wa Katavi kupiga marufuku wafanyabiashara kutoka nje ya nchi kwenda mojakwamoja vijijini kununua mazao itasaidia kupunguza ongezeko la bei mara dufu kwa mazao hususani Mpunga na mahindi.

Antony Chula mfanya biashara wa Mahindi katika soko la Mpanda hotel Manispaa ya Mpanda mkoa wa Katavi amesema wafanyabiashara wa kigeni wakienda kijijini wamekuwa wakijali kujaza mzigo na kuondoka bila kujali kuwa wanaathiri watumiaji wa bidhaa hiyo kwa kupandisha bei hiyo ya mazao.

Moja ya mfanyabishara wa Mahindi katika soko la Mpanda hotel akizungumnza na chombo hiki kuhusu mwenendo wa biashara ya mahindi sokoni hapo

‘’Ilikuwa ni changamoto sana kwa mfanyabiashara kutoka nje kupitiliza moja kwa moja kijijini imetuathiri pakubwa kwa maana mfano bei ya gunia la mahindi kwa hapa mjini kwa kule kijijini mfano tunanunua elfu Tisini mfanya biashara akifike kule kijijini anapandisha bei moja kwa moja’’ amesema Chula

Amempongeza mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua mrindoko kwa hatua hiyo ya kupiga marufuku wafanya biashara wa kigeni  kwenda vijijini moja kwa moja kununua mazao na badala yake wafanyabiashara hao wa Kigeni wanunulie Mahindi hayo Sokoni na itakuwa na tija kwa uchumi wa Mkoa wa Katavi.

‘’mkuu wa mkoa tunampongeza kwa hayo maono ni wakuuwa mikoa wachache ambao wanaliangalia suala hilo la kutujali sisi wafanya biashara wa ndani katika mkoa wetu’’ amesema Antony

Khadija Rashid mfanya biashara wa wa Mahindi katika soko la Mpanda hotel wakati akizungumnza na chombo hiki amesema hatua ya serikali ya Mkoa wa Katavi kuchukua maamuzi hayo yatakwenda kuwanufaisha wafanyabiashara na serikali kupata mapato kwakuwa wafanya biashara hao watakuwa wananunulia mazao hayo kutoka sokoni hapo.

‘’Wafanya biashara wanaotoka Kenya waje kununulia mahandi haya sikoni sio kwenda moja kwa moja kwenda huko kijijini tunaishuru serikali kwa kuliona hilo’’ amesema Khadija

Antony Chula Mfanyabiashara wa Mahindi soko la Mpanda Hotel Manispaa ya Mpanda Mkoa wa Katavi amepongeza hatua ya mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko kupiga marufuku wafanyabiashara wa Kigeni kwenda kununua mazao vijijini.

Amesema wafanyabiashara hao wa ndani ya mkoa wa Katavi walikuwa wanaathirika kwa kushidwa kupata mzunguko wa kifedha sababu mkenya anaingia kijijini badala ya kupita sokoni kununua mazao hayo.

‘’kwa maoni yangu mimi mkuu wa mkoa yupo sawa hata sisi lilikuwa linatupa utata sana maana tulikuwa hatupati faida kutokana na mfumko huo wa bei unaletwa na hao wafanya biashara wa kigeni’’

Hivi karibuni mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua mrindoko alikutana na wafanyabishara wa mkoa wa Katavi alipiga Marufuku wafanyabiashara wa kigeni kwenda kununua mazao vijijini moja kwa moja badala yake wafanya biashara wa mkoa wa Katavi wanunue mahindi hayo vijijini na kuyaleta sokoni ili wafanya baishara wa kigeni wanunulie mazao hayo sokoni.

‘’wafanyabiashara wanaotoka nje ya nchi hawaluhusiwi kununua mazao moja kwa moja shambani au moja kwa moja kwa wakulima badala yake wafanya biashara wetu ndani ya mkoa changamkieni fursa hiyo ya kununua mazao hayo vijijini na kuwauzia wafanyabiashara wa kigeni sokoni ‘’amesema Mrindoko

kwa habari zaidi Tembelea ukurasa wetu wa 

kataviclub.blogspot.com

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages