VYAMA VYA USHIRIKA VISIMAMIE MALIPO YA WAKULIMA

Mwakilishi wa Mkuu wa Mkoa wa Katavi Jamila Yusuph ambae pia ni Mkuu wa Wilaya ya Mpanda akiwahutubia wajumbe wa Jukwaa la Maendeleo ya  ushirika Mkoa wa Katavi. 
Na Paul Mathias,Katavi

Serikali katika Mkoa wa Katavi imeviagiza vyama vya ushirika kuhakikisha wakulima wa Mazao ya Pamba na Tumbaku na mazao mengine yaliyo chini ya ushirika kuhakikisha wakulima wanalipwa fedha zao pindi wanapopeleka mazao hayo sokoni.

Peter nyakunga kaimu Mlajisi Msaidizi mkoa wa katavi akitoa taarifa ya maendeleo ya ushirika kwa wajumbe wa Jukwaa la Maendeleo na Ushirika mkoa wa katavi 

Serikali katika Mkoa wa Katavi imeviagiza vyama vya ushirika kuhakikisha wakulima wa Mazao ya Pamba na Tumbaku na mazao mengine yaliyo chini ya ushirika kuhakikisha wakulima wanalipwa fedha zao pindi wanapopeleka mazao hayo sokoni.

Kauli hiyo imetolewa na Mwakilishi wa Mkoa wa Katavi Jamila Yusuph ambae ni Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Mkoa wa Katavi.

Akiwa hutubia wadau wa Jukwaa la maendeleo ya ushirika katika mkoa wa Katavi Katika ukumbi wa mikutano wa Mpanda Social Hall Jamila amesema vyama vya ushirika niwajibu wao kuhakikisha wakulima wanalipwa fedha zao kwa wakati ili waweze kujiletea maendeleo kupitia fedha hizo.

Wanaushirika kutoka vyama mbalimbali vya ushirika mkoa wa Katavi wakiwa katika picha ya Pamoja na Mwakilishi wa Mkuu wa mkoa wa Katavi Jamila yusuph ambae ni Mkuu wa Wilaya ya Mpanda [Mwenye Ushungi katikati walio kaa.

‘’nitumie fursa hii kutoa rai kwa viongozi wa vyama vya zao la Tumbaku na Pamba kuhakikisha wakulima wanalipwa Fedha zao kwa wakati mara baada ya kumaliza kuuza mazao yao ili fedha ziweze kuwasaidia kwenye shughuli zao za kijamii’’

Amewataka viongozi wa vyama vya ushrika kufanya kazi kwa bidii kwa kutanguliza weledi uaminifu na uadirifu katika kazi za kila za kuvisimamia vyama vya ushirika.

Jamila anasema ‘’nitoe rai kwa viongozi wa vyama vya ushirika na wakulima mliopo hapa kufanya kazi kwa bidii weledi uaminifu na uadilifu katika utendaji kazi ‘’

Amsema kuwa ushirika ni Mhimili mhimu katika sekta ya uchumi kwa kuchangia vikubwa katika Mapato kwenye halmashauri na mkoa wa Katavi kwa ujumla.

Katika hatua nyingine amewaomba wananchi wa mkoa wa Katavi kuguswa na kujiunga katika Saccos Mbalimbali ili waweze kujiajilia kwa kuanzisha viwanda vidogo ambavyo vitasaidia kuajili watu wenngine kupitia sekta hiyo.

Kaimu Mlajisi Msaidizi Mkoa wa Katavi Peter Nyakunga amesema kuwa mkoa wa Katavi unavyama vya ushirika vipatavyo 50 ambavyo hufanya shughuli mbalimbali ikiwemo kilimo,Ufugaji na Saccos.

‘’katika vyama hivyo Hamsini vya ushirika tunavyama tunavyama Arobaini na Moja vya mazao ,vyama vitano vya kifedha,vyama viwili vya ufugaji,chama kimoja cha uvuvi na chama kikiuu kimoja’’ amesema Nyakunga

Amebainisha kuwa Jukumu kubwa ushirika ni kusimamia utekelezaji wa sheria za ushirika na kutoa elimu kwa wanaushirika kuhusu mambo mbalimbali yanayohusu ushirika na kutatua migogoro ndani ya vyama vya ushirika.

Nyakunga amesema kuwa hadi sasa Vyama vya ushrika vinajumla ya wanachama Elfu Sita na kumi na tatu na kufanya kuwa na hisa zenye thamani shilingi Milioni 316 laki saba na kumi na Tano.

Amos Kaega Mwenyekiti wa Jukwaa la Maendeleo na ushirika mkoa wa Katavi ameishuru serikali ya awamu ya Sita kwa kuendelea bkuboresha mazingira ya sekta ya kilimo hapa nachini na kufanya sekta hiyo kuwa mhimu katika ukuaji wa uchumi.

Mkutano huo wa wa Jukwaa la Maendeleo ya  ushirika mkoa wa Katavi umeenda sambamba na kaulimbiu inayosema ‘’USHIRIKA KWA MAENDELEO ENDELEVU’’ KAZI IENDELEE.

Kwa habari zaidi tembelea ukurasa wetu wa 

kataviclub.blogspot.com

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages