MAAFISA TARAFA NA WATENDAJI WA KATA WAPIGWA MSASA

 

Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Jamila Yusuph akizungumnza na maafisa tarafa na watendaji wa kata za Mkoa wa Katavi kwa niaba ya Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko katika ukumbi wa mikutano wa Mpanda Manispaa

Na Walter Mguluchuma

Katavi,

Maafisa Tarafa na Watendaji wote wa Kata wa Mkoa wa Katavi wamepatiwa mafunzo ya kuwajengea uwezo  wa utendaji wao wa kazi wa kila siku  na  kukumbushwa mahusiano yao baina ya Serikali kuu na Serikali za Mitaa ili kuhakikisha utawala Bora unafanyika .

Maafisa Tarafa na watendaji wa Kata Mkoa wa Katavi wakiwa wakisiliza uwasilishwaji wa Mada mbalimbali katika semina ya kuwajengea uwezo katika kazi zao.

Maafisa Tarafa na Watendaji wote wa Kata wa Mkoa wa Katavi wamepatiwa mafunzo ya kuwajengea uwezo  wa utendaji wao wa kazi wa kila siku  na  kukumbushwa mahusiano yao baina ya Serikali kuu na Serikali za Mitaa ili kuhakikisha utawala Bora unafanyika .

Mafunzo hayo   hayo  yaliondaliwa na TAMISEMI yamefunguliwa na Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Jamira Yusuph aliyemwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko kwenye ufunguzi wa mafunzo hayo yaliofanyika katika ukumbi wa Manispaa ya Mpanda .

Katika hotuba yake hiyo ya ufunguzi  Jamila  Yusuph   amesema  mafunzo hayo ni muhimu kwa viongozi hao wa Tarafa na Kata  kwani yatawaongezea uwezo wa utendaji wao wa kazi zao za kila siku  kwani uzowefu umeonyesha  umeonyesha uwepo wa   uchangamoto  zinazokuwepo  za utekelezaji wa  huduma  kwa wananchi  katika ngazi ya Kata  na Tarafa  na Halmashauri zinazotokana na sababu mbalimbali  ikiwemo kutozingatia sheria  na kanunu katika utekelezaji wa kazi  za kila siku .

Amezitaja baadhi ya changamoto  hizo ni migogoro ya kiutendaji  kati ya viongozi na wataalamu wa kwenye ngazi hizo  pili usimamizi usio ridhisha  wa miradi ya maendeleo inayotekelezwa  kwenye maeneo yao  kutotatuliwa kelo za wananchi kwa wakati .

Kutokuwa na uwelewa kwa sheria  sera na miongozo  wanayotakiwa kuisimamia  na kuitekeleza ,kukosa ubunifu  wa  kiongozi  katika kujua furusa za kiuchumi  na  kijamii zinazopatikana kwenye ngazi ya msingi  pamoja na ushirikishwaji wa wananchi na wadau  kulingana na rasilamali zinazokuwepo .

Jamila  amesema kuwa ni matumaini  na matarajio  ya TAMISEMI   ya  baada ya mafunzo hayo maafisa hao wa ngazi ya Tarafa na Kata  watakwenda kutatua kelo za wananchi na watazingatia sheria za utumishi wa umma  na kutotowa siri za Serikali .

Ummy  Wayayu  Mkurugenzi  Msaidizi  idara  ya  Serikali  za Mitaa  fedha kutoka TAMISEMI  ameeleza kuwa  mafunzo hayo kwa maafisa wa ngazi hiyo yatafanyika kwa  mikoa yote na  yalizinduliwa huko Mkoani    Songwe .

Amebainisha kuwa  Tamisemi wameona umuhimu  wa kuwapatia mafunzo hayo maafisa hao kwa kuwa wao ndio viunganishi   baina ya Serikali kuu na Serikali za Mitaa na pia  kuwakumbusha wao ndio mzizi wa utendaji kazi kuanzia huko chini   ambao wanatakiwa kutatua changamoto zinazokuwa zimetokea kwa wananchi na kuzitatua  kwenye maeneo yao .

Kwa upande wake  Naibu  Mkuu wa cguo  cha Serikali  za   Mitaa  Dr  Michael  Msendekwa  ameeleza kuwa  anaimani kuwa  baada ya mafunzo hayo  watabadilika katika utendaji wao wa kazi za kila siku na yatasaidia si kwa Katavi tuu mbali kwa nchi nzima .

Wanaamini kuwa wao  maafisa hao wa ngazi ya Tarafa na Kata    wako karibu  na wananchi  katika  kazi zao  za kila siku  hivyo watahakikisha utawala bora unafanyika na kazi za  serikali zinatekelezwa .

Mmmoja wa  washiriki wa mafunzo hayo  Afisa Tarafa  wa  Tarafa ya Kabungu  Alson Uisso  amesema kuwa mafunzo hayo yatawasaidia sana kuwakumbusha majukumu  yao ya utendaji wao wa kazi  na baada ya   hapo wataenda kuwa viongozi bora zaidi kwenye maeneo yao ya kazi .

kwa habari zaidi tembelea ukkurasa wetu wa 

kataviclub.blogspot.com

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages