WANANCHI WAASWA KUUNGA MKONO JUHUDI ZA SERIKALI

Shekhe Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mashaka Nassoro Kakulukulu akizungumnza na waumini wa Dini ya Kiislamu wa Mkoa wa Katavi wakati wa Sikuu kuu ya Eid El Adha 

Na Paul Mathias

Balaza la waislamu Tanzania Bakwata Mkoa wa Katavi limesema kuwa linaunga mkono juhudi mbalimbali za kimaendeleo zinazo fanywa na serikali kupitia uwekezaji na ubinafsishaji wenye lengo  kuleta maendeleo kwa wananchi na Taifa kwa ujumla.

Balaza la waislamu Tanzania Bakwata Mkoa wa Katavi limesema kuwa linaunga mkono juhudi mbalimbali za kimaendeleo zinazo fanywa na serikali kupitia uwekezaji na ubinafsishaji wenye lengo  kuleta maendeleo kwa wananchi na Taifa kwa ujumla.

Hayo yamebainishwa na shekhe mkuu wa mkoa wa Katavi Mashaka Nassoro Kakulukulu wakati akiongoza swala ya Eiad El Adha iliyoswaliwa katika viwanja vya Shule ya Msingi Kashato Mpanda

Kakulukulu amsema ‘’Kuna mambo mbalimbali ambayo serikali inatuletea katika mikakati yake na mipango yake nilazima na niwajibu wetu kuiamini na kutii yale ambayo yanayoletwa letwa kwetu ‘’

‘’yapo mambo mbalimbali ambayo serikali inayafanya katika nchiyetu yapo mambo mbalimbali ambayo yanaelekezo la serikali katika nchi yetu kwa mujibu wa aya hii twatakiwa sisi kuwa tii na na kuelekea katika maelekezo ambayo wanayatoa’’amesema Kakulukulu

Katibu tawala mkoa wa Katavi Abas Hassan Rugwa akitoa salamu za serikali katika sikukuu ya Eid El Adha viwanja vya shule ya Msingi Kashato

Amesema serikali haiwezi kuleta jambo ambalo linamadhara kwa wananchi wake kwa mfano kwenye maswala ya ubinafsi shaji kwenye masuala ya uwekezaji.

‘’Serikali haiwezi kutuletea jambo ambalo linamadhara kwetu mfano katika mambo ya uwekezaji serikali haiwezi kuleta jambo ambalo jambo hilo inafahamu kwamba litaleta madhara kwa wananchi wake ikiwa serikali italeta jambo lenye madhara hiyo serikali itawaongoza akinanani‘’

Katika taua nyingine amewaasa waumini wa Dini ya kiislamu na wananchi wa ujumla kuishi katika utii,Umoja na mshikamano pamoja

‘’Ibaada yetu hija inatufundisha kuwa na umoja kuwa na mshikamano kuwa na umoja wa Umma watazame waloko hija leo hauwezi ukamtambua mfalme hauwezi ukamtambua waziri hauwezi ukamtambua rais wote wapo kwenye vazi moja hakika umati huu ni umma mmoja’’

Awali akitoa salamu za serikali kwa mkoa wakati wa swala hiyo Katibu Tawala mkoa wa katavi Abas Hassan Rugwa ameiomba jamii na wananchi wa mkoa wa katavi kuendelea kudumisha maadili ya kumcha mungu pamoja na tamaduni za kitanzania.

‘’niwaombe sana tuendelee kuzingatia mila na tamaduni na maadili yetu yote ya kiimani nay ale mengine ya kijamii ili kuifanya jamii yetu iwe salama zaidi’’

Baadhi ya waumini walioshiriki swala hiyo wamesema kuwa niwajibu wa jamii kuendelea kusisitiza malezi bora kwa watoto na kuwalea katika misingi ya kumcha mungu ili kuwa na kizazi chenye hofu ya mungu.

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages