WANNE MBARONI KWA KUTEKA MTOTO WA MIAKA TISA

Kaimu kamanda wa Polisi Mkoa wa Katavi Kaster Ngonyani akitoa taarifa ya Matukio mbalimbali kwa waandishi wa habari ofisini kwake.

Na Walter Mguluchuma,Katavi.

Watu wanne wanashikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa Katavi kwa  kutuhuma  za  kumteka  mtoto mdogo wa kike (9) mwanafunzi wa darasa la nne   katika   shule ya Msingi Mizengo  Pinda katika Manispaa ya Mpanda  na kisha kumfungia ndani ya chumba kwa zaidi ya siku moja na kutishia  kumuua kwa madai vinginevyo walipwe Milioni 50 ili wamwachie .


Watu wanne wanashikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa Katavi kwa  kutuhuma  za  kumteka  mtoto mdogo wa kike (9) mwanafunzi wa darasa la nne   katika   shule ya Msingi Mizengo  Pinda katika Manispaa ya Mpanda  na kisha kumfungia ndani ya chumba kwa zaidi ya siku moja na kutishia  kumuua kwa madai vinginevyo walipwe Milioni 50 ili wamwachie .

Kaimu  Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Katavi  Kaster  Ngonyani  amewataja watuhumiwa hao walikamatwa kuhusika na tukio hili kuwa ni  Joseph  John(24) Yusuph  Sadick  (27) wakazi wa Mtaa wa Milupwa , Abrahamu  Kassim(28)  Mkazi wa Mtaa wa Misunkumilo Manispaa ya Mpanda na   Samwel Nzobe (41) Mkazi wa Mtaa wa Kotasi Manispaa ya Mpanda .

Amesema watuhumiwa hao wote wanne wamekamatwa  kufuatia msako mkali ulifanywa na jeshi la Polisi usiku na   mchana kufatilia jeshi hilo la polisi kuwa limepata taatifa ya kutekwa kwa mtoto huyo mdogo wa kike .

Kaimu  Kamanda wa Polisi Ngonyani amebainisha kuwa  tukio hilo la kikatili la kumteka mtoto huyo lilitokea hapo  June 13 majira ya saa  nane mchana  katika Manispaa ya Mpanda wakati mtoto huyo alipokuwa akitokea shuleni   kwenye shule anayosoma ya Mizengo Pinda alikukuwa amekwenda kufanya usafi shule .

Ameeleza kuwa wakati akiwa njia maeneo ya jirani na Kanisa Katoliki Jimbo la Mpanda   anaelekea nyumbani kwao ndipo watuhumiwa hao wanne walipomteka  mtoto huyo na kumpeleka kusiko julikana   na kumtishia   kumuua     lasivyo walipwe na  mzazi wake kiasi cha shilingi milioni 50 ndipo waweze kumwachia akiwa hai .

Baada ya  taarifa  hizo kuwa zimepokelewa  Jeshi la Polisi lilianza mara moja kufanya msako mkali  wa kuwasaka wahusika wa tukio hilo  msako ambao ulifanyika usiku na mchana katika   maeneo yote ya Mkoa wa Katavi ili kuwahakikisha mtoto huyo anapatikana akiwa salama .

Ngonyani amesema ndipo  mnamo tarehe  14 june  jeshi la polisi walifanikiwa   kumpata  mtoto huyo  akiwa salama  huko  katika maeneo  ya Mtaa wa Milupwa Manispaa ya Mpanda  akiwa amefichwa ndani  ndani ya chumba  cha mtuhumiwa  Joseph John.

Amesema watuhumiwa  wote  wanaendelea  kushikiliwa na jeshi la polisi  kwa mahojiano zaidi    juu ya tukio hili na  mara  baada ya upelelezi  kukamilika watafikishwa  mahakamani  kujibu tuhuma zinazo wakabili.

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages