CCM MPANDA YARIDHISHWA NA MIRADI YA BOOST

Kamati ya siasa ya Chama cha Mapinduzi CCM Wilaya ya Mpanda ikiwa katika Ziara ya kukagua Majengo ya Madarasa yanayotekelezwa kupitia Mradi wa Boost.

Na Paul Mathias,Mpanda.

Chama cha Mapinduzi CCM Wilaya ya Mpanda kimeridhishwa na Mwenenendo wa ujenzi wa Vyumba vya Madarasa kwenye shule za Msingi wilaya ya Mpanda yanayojengwa  kupitia Mradi wa Boost.


Chama cha Mapinduzi CCM Wilaya ya Mpanda kimeridhishwa na Mwenenendo wa ujenzi wa Vyumba vya Madarasa kwenye shule za Msingi wilaya ya Mpanda yanayojengwa  kupitia Mradi wa Boost.

Kamati ya siasa ya Wilaya ya Mpanda ikiongozwa na Katibu wa chama cha Mapinduzi CCM Wilaya ya Mpanda Sadiki Kibwana Kadulo amesema mwenendo wa miradi hiyo itakwenda kuwa saidia wanafunzi kuyatumia Madarasa hayo pindi shule zitakapofunguliwa Mwezi wa Saba mwakaa huu.

‘’maagizo na maelekezo sisi chama cha Mapinduzi kuhakikisha ifikapo July Madarasa haya yawe yamekamilika na wanafunzi wawe wameingia kwenye Madarasa haya tunaamini kwamba kwa kasi hii watoto watayatumia madarasa haya mwezi wa Saba’’ amesema Kadulo

Amesema katika maeneo aliyotembelea ya halmashauri ya Nsimbo kasi ya ujenzi inaendelea kwa kiwango cha kuridhisha na chama hicho kinridhishwa na mwenendo wa kasi hiyo.‘’tumekwenda kule Nsimbo tumekuta kasi ni kubwa ni hii kwahiyo tunakupongeza sana mkuu wa Mkoa Mwanamvua Mrindoko pamoja na mkuu wa Wilaya na Wakurugenzi kwa usimamizi huu sisi kama Chama tunakitu cha kusema kwa wananchi kupitia Miradi hii’’

Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda Sophia Kumbuli amesema halmashauri hiyo imepatiwa fedha kiasi cha Shilingi Bilion 1.9 kwaajili ya ujenzi wa Madarasa kupitia Mpango huo wa Boost.

‘’kwa halmashauri ya Manispaa ya Mpanda sisi tulipokea kiasi cha shilingi Bilion 1.9 ambayo kwa pamoja inaendelea kujenga miundo mbinu ya madarasa ambayo ipo katika hatua mbalimbali’’ amesema Kumbuli


Kwa upande wake Mkurugenzi wa Halmashauri ya Nsimbo Mohamed Ramadhani amesema hamashauri ya Nsimbo imepokea kiasi cha Shilingi Bilion 1 na milioni 850 kwaajili ya ujenzi wa miundombinu ya Madarasa katika shule nane za Msingi.

‘’katika fedha hizi ninashule mbili mpya zinazojegwa ambavyo ni jumla ya Nyumba 16 ambapo vyumba 14 kwaajili ya Wanafunzi wa Kawaida na  na vyumba Viwili kwaajili ya Madarasa ya awali ya mfano ujenzi unaendelea upo katika hatua ya kupaua’’

Katika ziara hiyo ya kukagua miradi ya Elimu Msingi kupitia Miradi ya Boost chama cha Mapinduzi wilaya ya Mpanda kiweza kutembelea Shule ya Msingi Makanyagio,Shule ya Msingi Shanwe,Shule ya Msingi Itenka na shule ya Msingi Tumaini zilizopo halmashauri ya Nsimbo.

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages