Na Walter Mguluchuma,Mpanda.
Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Jamila Yusuph amewataka wananchi wa Wilaya hiyo kuhamasisha jamii kupeleka watoto shule kwani kwa sasa miundombini ipo ya kutosha ya madarasa ya shule za msingi na Sekondari na vyuo kwa wanaomaliza kidato cha nne na darasa la saba vipo hivyo wawasimamie watoto waweze kwenda shule miundombinu hiyo itumuke kwa watoto wa wana Mpanda mwisho wa siku wawe wapate kuwa viongozi wanchi hii na kuwaongoza watu wengine wa nchii hii.
Mkurugenzi Mtendaji wa Manispaa ya Mpanda,Sophia Kumbuli akizungumza jambo na Katibu Tawala wa Wilaya ya Mpanda Mwashitete( Picha na George Mwigulu)
Wito huo ameutowa wakati wa kikao cha wadau wa maendeleo wa Wilaya ya Mpanda kilichofanyika katika ukumbi wa Manispaa ya Mpanda kwa ajiri ya kujadili maswala ya maendeleo ya Wilaya hiyo .
Aliwasisitiza wajumbe wa kikao hicho kuwa mabalozi
wa kuwahasisha jamii kupeleka watoto shule kwani Serikali imeisha weka
miundombinu ya kutosha kwenye shule za msingi na Sekondari na pia kwenye
Wilaya ya Mpanda vipo vyuo mbalimbali kama vile chuo cha afya, Veta na
chuo cha Wananchi Msaginya .
Amebainisha kuwa kwenye vyuo hivyo wanaweza kwenda watoto
waliomaliza elimu ya kidato cha nne na pia waliomaliza darasa la saba
wanaweza kwenda kwenye chuo cha wananchi Msaginya na veta Mpanda .
Dc Jamila aliwataka kutumia vizuri
miundombinu hiyo vizuri kwa manufaa ya watu wa Mpanda ili na
wao watoto mwisho wa siku waweze na wao kuwa viongozi katika nchi
hii na kuweza kuwaongoza wengine hivyo miundombinu hiyo iliyojengwa
isibaki bila watoto kwenda kuitumia .
Amewaomba wananchi wananchi kuhakikisha miundombinu
yote inayoletwa katika Wilaya ya Mpanda kama vile ya
elimu maji barabarana mingineyo kuhakikisha wanaitunza
vizuri ili iwezekudumu muda mrefu zaidi kwa manufaa ya sasa
na hapo baadae .
Swala jingine amewaomba wadau wa maendeleo kusimama
kwa pamoja kuupinga ukatili wa aina yoyote
ile pamoja na kukataa mmonyoko wa maadili
kama vitendo vya ubakaji ,usagaji vitendo vya ushoga mimba za
utotoni wote wasimamame kwa pamoja na Mungu atawabaliki kwa kupinga
vitendo hivyo .
Alisema kwa sasa watoto wamekosa malezi mazuri hali ambayo imesababisha kuwa wanafanyiwa vitendo vya ukatili sana hasa watoto wa kiume na wamakuwa wakifanyiwa na wengine ndugu zao wa karibu hata wakuzaliwa anachokizungumza wameisha kifanyia uchunguzi wamebaini hayo.
Wajumbe wakiwa kwenye mkutano leo katika ukumbi wa manispaa ya Mpanda (Picha na George Mwigulu) |
Jamila alisema ni vema kuwa watu wanafanya mazungumzo na watoto wao wasiseme tuu wapo na ndugu zao wanalala pamoja wawe na utaratibu wa kuzungumza nao na ikibidi kuwakagua kwasababu watoto wetu wanaumizwa sana na walezi kwa sababu wazazi tumekuwa tujishughulisha sana na mambo mengine na kusahau kuwaangalia watoto.
Mkurugenzi wa Manispaa ya Mpanda Sofia Kumbuli amesema kuwa
Rais Dkta Samia Suluhu sana amesema Manispaa ya Mpanda
wametendewa haki sana kwa kuboreshewa Hospitali ya Manispaa ya
Mpanda ambapo ukifika pale kwa sasa ni kama vile umefika
kwenye Hospitali ya kubwa za Rufaa kwa jinsi ilivyokarabatiwa
na inavyoendelea kujengwa .
Amesema katika kuunga jitihada hizo za
Rais samia Manispaa hiyo inatajia kujenga madarasa ya
shule za msingi mia moja ili kwa kupitia frdha za mapato ya ndani ya
Halmashari hiyo ili kuondoa tatizo la upungufu wa vyumba vya madarasa .
Mzee maarufu wa Mji wa Mpanda Vicent Nkana alisema
kuwa hali ya ulinzi na usalama katika mkoa wa Katavi anaiona
imeimarika sana tofauti na hali ilivyokuwa katika miaka ya hapo nyuma wananchi
walikuwa hawaishi kwa amani.