POLISI KATAVI YAKANUSHA TAARIFA ZA UZUSHI ZILIZOSAMBAZWA KWENYE MITANDAO ZA KUJERUHIWA KIONGOZI WA CHADEMA KWA SABABU ZA KISIASA .

 

Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Katavi Kaster Ngonyani.

Na Walter Mguluchuma,Katavi.

Jeshi la  Polisi Mkoa wa Katavi  limekanusha  taarifa  ambazo  zimesambazwa  katika   mitandao mbalimbali  ya  kijamii   zikieleza  kuwa  Pambano  Kamaka (40) Mkazi wa  Mtaa wa Makanyagio  Manispaa ya Mpanda  ambae alijeruhiwa kwa  kupigwa  na kitu  kizito  kichwani  kuwa  alifanyiziwa kitendo hicho kwa sababu za kisiasa  sio za kweli na wananchi wanatakiwa wapuuze  uvumi huo wa uongo.

Jeshi la  Polisi Mkoa wa Katavi  limekanusha  taarifa  ambazo  zimesambazwa  katika   mitandao mbalimbali  ya  kijamii   zikieleza  kuwa  Pambano  Kamaka (40) Mkazi wa  Mtaa wa Makanyagio  Manispaa ya Mpanda  ambae alijeruhiwa kwa  kupigwa  na kitu  kizito  kichwani  kuwa  alifanyiziwa kitendo hicho kwa sababu za kisiasa  sio za kweli na wananchi wanatakiwa wapuuze  uvumi huo wa uongo.

Kamanda wa P olisi wa Mkoa wa Katavi Kaster  Ngonyani  amewaambia wandishi wa Habari kuwa Pambano  Kamaka  ambae ni   Katibu   Mwenezi wa    Kata ya Makanyagio  Chama    Cha  Demokrasia  na  Maendeleo  ( CHADEMA) alipigwa na kitu  kizito  kichwani na kupoteza  fahamu .

Alisema  uchunguzi uliofanywa na jeshi la Polisi  baada ya kumkamata  mtuhumiwa   mmoja  aitwaye  Gilibalt Jaluo   mkazi wa Mtaa wa Makanyagio  ambae alihusika kwenye tukio la kumpiga  Kamaka  umeonyesha kuwa  alipigwa kutokana deni alilokuwa akidaiwa la Tshs 50,000 na  mtuhumiwa  mwingine .

Kamanda  Ngonyani  alisema  mtuhumiwa huyo mwingine  aliyekuwa akimdai kiasi hicho cha fedha  alikimbia mara   baada ya kuwa  wametenda kosa hilo  la kumpiga na kitu kizito  kichwani   mhanga huyo.

Amesisitiza kuwa   tukio hilo  halina ukweli  wowote  kama ambavyo limeripotiwa na  mitandao ya kijamii kuwa  linahusiana na  maswala ya kiasiasa  tukio hilo  halihusiani na   maswala ya kiasiasa  hivyo wananchi  wapuuze  uvumi huo wa uongo na wanamtafuta mtu  huyo  aliyeeneza   habari hizo za uongo kwenye mitandao ya kijamii .

 Jeshi la  polisi  Mkoa wa Katavi  linaendelea na  msako  mkali wa kusaka  mtuhumiwa  huyo  aliyekimbia  ili  waweze kumkamata  ili  hatua  kali  za kisheria  zichukuliwe  dhidi   yao waliohusika kutenda kitendo hicho cha kikatili .

Aidha  Kamanda  Ngonyani  amewaomba wananchi  kuendelea kutowa taarifa  za uhalifu  kwenye   mamlaka  husika  na kisha kuziachia  mamlaka hizo  kufanya uchunguzi  ili kubaini   ukweli wa taarifa hizo  na sio kusambaza  taarifa   zisizo rasmi  kwenye  mitandao  ya kijamii na sehemu nyingine  kwani  zinaleta  taharuki  kwenye jamii .

 Hari ya  Pambano  Kamaka  ambae  amelazwa  katika  Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Katavi bado haiendelei    vizuri na  taratibu  zinafanywa za  kumpeleka  katika Hospitali ya Kanda  Mbeya  zinaendelea  kwa ajiri ya  matibabu zaidi .

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages