Hii ni picha ya siku ya uzinduziI wa makoso ya Tumbaku uliofanywa na Kampuni ya Mkwawa Leaf. Meneja wa Bodi ya Tumbaku Mkoa wa Katavii,Genwin Swai alipokuwa akitoa maelezo kwa Mkuu wa Mkoa wa Katavi,Mwanamvua Mrindoko.(Picha na Makitaba). |
Na Mwandishi
wetu,Katavi .
Wakulima wa vyama vya AMCOS vya Nsimbo na Kasekese wameilalamikia Kampuni ya ununuzi wa Tumbaku ya Mkwawa Leaf Tobacco Limeted kwa kukiuka mkataba wa ununuzi wa Tumbaku kwa kushindwa kuwalipa malipo yao ya ununuzi wa Tumbaku ya msimu wa 2022/2023 na kuwasababishia wakulima kuishi kwa shida.
Mkurugenzi wa Kampuni ya Mkwawa Leaf Tobbaco,Ahmed Mansoor akizungumza katika Mkoa wa Katavi wakati wa uzinduzi wa masoko ya zao la tumbaku (Picha Na Makitava) |
Baadhi ya wakulima hao wamedai kuwa baada ya kuingia mkataba na vyama vyao walitegemea kuwa Kampuni hiyo ingekuwa msaada mkubwa kwa wakulima wa zao la Tumbaku katika Mkoa wa Katavi .
Mmoja wa wakulima
wa Amcos ya Nsimbo Gedson Simon amesema kuwa toka walipofanya
soko la ufunguzi mnamo tarehe 3 Mei 2023
walipo uza tumbaku yao kwa mara ya kwanza hadi sasa wakulima
wa kwenye chama hicho hawalipwa fedha zao licha ya wao mara kwa
mara kuwa wanafatilia kwenye Amcos yao wamekuwa wakijibiwa kuwa kuna shida ya
Dolla.
Amebainisha kuwa
kabla ya kuanza msimu wa ununuzi wa Tumbaku uongozi wa
Kampuni hiyo waliwaaminisha wakulima kwa kuwaeleza kampuni hiyo
ikisha nunua Tumbaku watakuwa wanalipa kwa wakati jambo ambalo limekuwa
tofauti .
Amebainisha kuwa kitendo
cha kutolipwa kwa wakati kimewasababishia wakulima kupa adha kubwa
kutoka kwa watu ambao walikuwa wamewaajiri kwa ajiri ya shughuli za kilimo
hicho ambao wameshindwa kuwalipa haovibarua wao hali inayofanya
waendelee kuwahudumia hadi sasa kwa chakula na matibabu pindi wanapokuwa
wamepata maradhi .
Alisema wao kama
wakulima wanategema walime tumbaku na kuiuza ili waweze
kuhudumia familia za lakini kwa wakulima wa Nsimbo hali imekuwa tofauti
na matarajio yao hivyo wanaiomba Serikali iweze kuangalia namna ya kuwasaidia
waweze kulipwa fedha zao .
Juma
Mwiga Mkulima wa Amcos ya Kasekese Juma Mwiga
ameeleza kuwa wao kama wakulima wameweza kuuza tumbaku yao kwa
wakati ila malipo yao ndio yamechelewa na kila wakiwauliza viongozi
wanaambiwa Dolla zimeisha hali ambayo inawafanya wakulima kutojua
watalipwa lini kwani ni mda mrefu toka walipo uza tumbaku yao .
Wanaiomba Serikali
iwasaidie kama changamoto ni Dolla ili walipo yao yafanyike mapema kwani
kazi ya kilimo cha Tumbaku ni kubwa sana wanachukua muda muda
mrefu wa maandalizi ya kilimo mpaka leo hii fedha
inapochelewa wanashindwa wafanye nini matokeo yake wamejiingiza kuchukua
mikopo ya fedha za riba hivyo hata kama watalipwa fedha kwa
hali iliyopo sasa zitaichia kwenye kulipia madeni hayo ya liba .
Amesema
anachofahamu kwenye Mabenki ambako vyama vyao vya AMCOS
waliko kopa fedha za pembejeo huwa fedha zikichelewa kulipwa
huwa kuna liba sasa kwa chelewa huku ili liba atalipa nani
wakati mkulima yeye sio kosa lake .
Mwenyekiti wa
Nsimbo Amcos Gredo Kasokola amesema malalamiko ya
wakulima ni haki kwani masoko licha ya kuanza
mwezi wa tano na kumaliza june 22 kwenye
chama hicho kwa mujibu wa mkataba wao na Kampuni ya Mkwawa
wanatakiwa kila wanapokuwa wamenunua tumbaku wanatakiwa walipe
ndani ya siku 14.
Amebainisha kuwa hadi
sasa wanadai kwenye Kampuni hiyo zaidi ya Dolla milioni moja wamekuwa
wakifanya mawasiliano na kampuni hiyo juu ya madai
yao kuwa kwa sasa hawana dolla za kuwalipa.
Amesema kuwa wakati
wa maadhimisho ya sikuuu ya Ushirika Waziri wa Kilimo
Hussein Bashe alisema swala la wakulima kutolipwa fedha
zao Wizara inalishughulikia na
ifikapo tarehe 30 Julai swala lilo litakuwa
limeshughulikiwa.
Mrajisi msaidizi
wa vyama vya ushirika Mkoa wa Katavi Perer Nyakunga amasema
kuwa ni kweli vyama hivyo hawaja lipwa fedha fedha zao
la kampuni ya Mkwawa licha ya masoko ya ununuzi kwa Mkoa
wa Katavi msimu wake kuwa umemalizika pia toka tarehe 13
julai .
Amefafanua kuwa kwa mujibu wa mikataba ya ununuzi na uuzaji wa tumbaku Makampuni yanatakiwa kulipa fedha ndani ya siku kumi nan ne baada ya kufanya ununuzi wa soko la tumbaku na wakulima huwa wanalipa kwa mikopo ya fedha za kutoka kwenye mabenki lakini kwa sasa kilichokwamisha ni Kampuni hiyo kutokuwa na dolla.