LUPEMBE KUWAKUTANISHA NSIMBO WACHIMBAJI NA WAZIRI WA MADINI.


Mbunge wa Jimbo la Nsimbo,Wilaya ya Mpanda Mkoa wa Katavi,Anna Lupembe akizungumza leo na wananchi  wa kata ya Ibindi  ambapo ameeleza nia yake ya kuwauganisha wachimbaji wa madini na waziri  wa madini Dkt Doto Biteko.

Na George Mwigulu,Nsimbo.

Wachimbaji wa madini wa Kata ya Ibindi halmashauri ya wilaya ya Nsimbo Mkoa wa Katavi wameahidiwa na mbunge wa Jimbo la Nsimbo,Anna Lupembe kuwa atamwalika waziri wa Madini Dkt Doto Biteko kwenye halmashauri hiyo ili kuweza kuzungumza na wachimbaji hao kwa ajili ya kutatua kero zao na kupewa elimu ya fursa za uwekezaji.

Amesema hayo leo Mbunge huyo wakati akiwahutubia wananchi wa kata ya Ibindi kwenye ziara yake ya kikazi jimboni humo ambapo amefafanua kuwa anatambua  changamoto mbalimbali ambazo zinawakabili wachimbaji wa madini hasa wadogo wadogo.

Lupembe ameeleza kuwa serikali ya awamu ya sita inadhamira njema kwa wananchi wake ya kuhakikisha wanapata maendeleo ya kiuchumi kwa sababu hiyo imekuwa ikitengeneza mazingira rafiki ya miundombinu bora ili kurahisisha upatikanaji wa fursa za kiuchumi.

Mbunge huyo amesema kuwa Waziri wa Madini, Dkt Doto Biteko atafika ndani ya halmashauri ya Nsimbo na kuonana moja kwa moja wa wachimbaji wa madini kwani licha ya kutatua kero zao bali ziko fursa nyingi za kiuwekezaji kwenye sekta za madini ambazo wachimbaji wanapaswa kuzifahamu.

Aidha anafahamu kuwa katika Kata ya Ibindi wako wawekezaji mbalimbali wa madini ambao wamekuwa wakifanya shughuri zao za kiuchimbaji hivyo ataendelea kuzungumza naoi li waweze kuendelea kushiriki kwenye kazi za maendeleo ya kata hiyo kama vile kuchangia fedha kwenye ujenzi wa miradi mbalimbali.

Wananchi wa Kata ya Ibindi waliohudhuria kwenye mkutano wa Mbunge wa Jimbo la Nsimbo,Anna Lupembe leo ambapo ameweza kuzungumza na wachimbaji wa madini pia.

Katika huta nyingine amemshukuru rais Samia Suluhu Hassain kwa kazi nzuri ya kuwezesha upatikanaji wa umeme na maji katika kata ya Ibindi kwani kwenye bajeti mpya miundombinu ya maji itaimarishwa zaidi.

Nao baadhi ya wananchi wa kata ya Ibindi wamemshukuru mbunge huyo kwa kuonesha nia ya dhati ya kuwasaidia wachimbaji wadogo wadogo wa madini ya kuwakutanisha na waziri wa madini.

Amesema hayo Masaja Daudi ambaye ni mchimbaji wa madini katika kata ya Ibindi ambapo ameeleza kuwa kama wachimbaji wa madini wazawa watapewa fursa zaidi ya elimu ya uchimbaji wataweza kupata tija kubwa kwenye uchimbaji.

Maulid Rashidi,Mchimbaji wa madini amesema kuwa wanataka kuona rasirimali za taifa kama madini yanawanufaisha zaidi wazawa na sio wageni pekee kwani itakuwa aibu kubwa kuachiwa mashimo pekee na umasikini huku madini yakiwanufaisha watu wanje.

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages