Na Alex Ngereza,Nsimbo
Kanisa la Pentekoste
Motomoto Kijiji cha Kaburonge Kata ya Katumba Jimbo la Nsimbo Mkoa wa Katavi limememshukuru Mbunge wa Jimbo la Nsimbo Anna Lupembe kwa kuwachangia kiasi cha
Shilingi Milioni Moja kwaajili ya Maendeleo ya Kanisa hilo.
Kanisa la Pentekoste Motomoto Kijiji cha Kaburonge Kata ya Katumba Jimbo la Nsimbo Mkoa wa Katavi limememshukuru Mbunge wa Jimbo la Nsimbo Anna Lupembe kwa kuwachangia kiasi cha Shilingi Milioni Moja kwaajili ya Maendeleo ya Kanisa hilo.Mbunge wa Jimbo la Nsimbo Anna Lupembe [kulia] akikabidhi shilingi Milioni Moja kwa Mchungaji kiongozi wa Kanisa hilo Beteria Beny
Pongezi hizo zimetolewa na
Mchungaji kiongozi wa Kanisa hilo Beteria Beny wakati wa ibaada ya jumapili
iliyofanyika Kanisani hapo amesema kuwa wanamshukuru Mbunge huyo kwa kuwasaidia
kiwango hicho cha fedha kwani zitawasidia katika maendeleo ya kanisa.
Mchungaji huyo amewaomba viongozi
mbalimbali kuwa na moyo wa kusaidia jamii ikiwemo makanisa kama hazina ya
kujiwekea mbinguni kupitia sadaka wanazo zitoa kwenye Jamii.
Aidha ametoa rai kwa wazazi na
walezi kutumia fursa ya miundombinu ya serikali hususani elimu kuwapeleka
watoto wao shule ili kuwa na Taifa lenye maarifa na ujuzi kupitia elimu.
Wakati huo mbunge Anna Lupembe
akiwa katika ibaada ya Misa ya Jumapili katika kanisa la Roman Catholic Kigango
cha Stalike Parokia ya Ilembo amewakabidhi wanakwaya wa kanisa hilo Kiasi cha
Shilingi Laki Tano ili kufanikisha ununuzi wa kinanda hii inatokana na ziara
aliyowahi kufanya kwenye kata ya stalike alipopokea taarifa ya maombi ya
uhitaji wa ununuzi wa Kinanda.
Waumini wa kanisa hilo na wanakawaya wamemshukuru Mbunge huyo kwa moyo wa upendo kwa kuwasaidia kwaajili ya maendeleo kanisani hapo.
Mbunge huyo anatarajia kuanza
Ziara katika jimbo lake la Nsimbo kuanzia Tarehe 10/7/2023 kwenye kata zote za Jimbo
la Nsimbo kwaajili ya kujionea kazi za maendeleo zinazotekelezwa kwenye Jimbo
hilo na kuibua vipaji vya Wasanii wanyimbo za kizazi kipya na Ngoma za asili.
Katika ziara hiyo atapata fursa ya kukabidhi Pikipiki 12 kwa Makatibu Kata wa Chama cha Mapinduzi ngazi ya Kata zilizopo Jimbo la Nsimbo hii ikiwa ni ahadi aliyotoa wakati akisoma taarifa ya utekelezaji wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi ndani ya miaka Miwili katika Jimbo la Nsimbo.
kwa habari zaidi endelea kutembelea ukurasa wetu wa
kataviclub.blogspot.com