MANISPAA YA MPANDA HAIKO TAYARI KUMWANGUSHA RAIS KWENYE KUTELEZA MIRADI


Meya wa Manispaa ya Mpanda Haidar Sumry amewahakikishia Watanzania Mbele ya Baraza la Madiwani kuwa Manispaa ya Mpanda haita mwangusha Rais Dkt Samia Suluhu Hassan katika kusimamia miradi ya maendeleo inayotekelezwa kwenye Manispaa ili kuwafanya wananchi wapate huduma bora kwa wakati

Na Walter Mguluchuma,Katavi.

Manispaa ya Mpanda  Mkoani  Katavi  wanahakikisha wanaendelea  kusimamia kwa nguvu zote  miradi ya  maendeleo yote inayotekelezwa kwenye Manispaa ya Mpanda  kwa ukaribu  zaidi  na  kwa kuzingatia    thamani ya fedha ili  kutomwangusha Rais kwenye utekelezaji wa miradi ya Maendeleo.

Mkurugenzi wa Manispaa ya Mpanda Sofia Kumbuli akiwaelezea madiwani wa Baraza la Madiwani namna ambavyo Manispaa hiyo ilivyopanga kutengeneza madawati 4000 kwa ajiri ya Shule za Msingi ili kuondokana na upungufu wa dawati katika shule za Msingi za Manispaa

Kauli hiyo ya Manispaa ya Mpanda  imetolewa na  Meya wa  Manispaa ya Mpanda  Haidary  Sumry wakati aliipokuwa akifunga  kikao cha robo ya   nne cha  Baraza la Madiwani la Manispaa hiyo kilichofanyika kwenye ukumbi wa Manispaa kilichojadili taarifa mbalimbali  za utendaji kazi wa Kata za Manispaa ya Mpanda .

Alisema  wanaendelea  kusimamia  miradi yote inayotekelezwa kwa ukaribu zaidi  ili kuhakikisha  miradi hiyo inatekelezwa kwa  ubora na kiwango kinachotakiwa kulingana na thamani ya  pesa ambazo   zinazokuwa  zimetolewa kwa ajiri ya utekeleza wa miradi husika .

Sumry ameeleza kuwa miradi yote ambayo wameitekeleza na inayoendelea  kwenye Manispaa ya Mpanda  inaonekana  jinsi ilivyotekelezwa  na ilivyosimamiwa  kwa ufanisi mkubwa   na kwa kuzingatia ubora unao lingana na thamani ya fedha  .

Amesisitiza kuwa hawako    tayari  kumwangusha Rais  Dkt  Samia  Suluhu  Hassan kwenye utekelezaji wa miradi ya maendeleo kwani   katika  kipindi cha  miaka  miwili  yapo mengi yamefanyika kwenye Manispaa hii ya maendeleo .

Hivyo  wataendelea  kusimamia  miradi yoye inayoletwa  na Serikali ya awamu ya sita  ili   kuhakikisha  wananchi waote wanapata  huduma nzuri na bora kama ambavyo Rais  Samia  alivyokusudia.

Madiwani wa Manispaa ya Mpanda Mkoani Katavi wakiwa kwenye Kikao cha Baraza la Madiwani wakipotea taarifa za utendaji kazi wa Kata mbalimbali

Mkurugenzi wa Manispaa ya Mpanda  Sofia Kumbuli amesema katika mwaka huu wa fedha wametenga  fedha kwa ajiri ya kutengeneza    madawati 4000  kwa ajiri ya wanafunzi wa shule za msingi ikiwa ni   katika   sehemu ya kuondokana na tatizo la upungufu wa madawati .

Amesema kuhusu vituo vya afya  vilivyojengwa hivi karibu vituo vyote wameisha weka umeme isipo kuwa vituo   viwili tuu    hata  havyo  Mkuu wa Mkoa wa Katavi ameisha  liagiza shirika la umeme Tanesco kuweza kufikisha umeme kwenye vituo hivyo vya afya   ifikapo    tarehe 30 ya mwezi huu .

Diwani wa  Kata ya   Mwamkulu Kalipi  Katani  amesema kuwa  miradi mbalimbali inayotekelezwa kwenye Manispaa ya Mpanda imekuwa na ubora  mkubwa na aliomba kwenye Kata yake waongeze walimu wa kike kwenye shule ya Msingi  Mkokwa ambayo inaupungufu wa walimu wa kike.

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages