MBUNGE MARTHA MARIKI ATOA MILIONI TANO UKARABATI JENGO LA MAMA NA MTOTO KAJEJE


Mbunge wa Viti maalumu Mkoa wa Katavi,Martha Mariki akizungumnza na wanawake wa UWT Katika Kijiji cha Kajeje Kata ya Kanoge.

Na Paul Mathia,Nsimbo

Mbunge wa Viti maalumu mkoa wa Katavi ,Martha Mariki amekabidhi hundi ya Shilingi Milioni Tano kwaajili ya kusaidia ukarabati wa Jengo la mama na Mtoto katika Kijiji  Cha  Kajeje iliyopo Kata ya Kanoge Halmashauri ya Nsimbo Mkoa wa Katavi.

Mbunge wa Viti Maalumu Martha Mariki [alieshika Maiki] akiwa katika picha na viongozi wa Kata ya Kanoge na uongozi wa Kijiji cha Kajeje akikabidhi hundi ya Shilingi Milioni Tano

Mbunge wa Viti maalumu mkoa wa Katavi, Martha Mariki amekabidhi hundi ya Shilingi Milioni Tano kwaajili ya kusaidia ukarabati wa Jengo la Mama na Mtoto  Katika Kijiji  Cha  Kajeje  Kata ya Kanoge Halmashauri ya Nsimbo Mkoa wa Katavi.

Akiwa katika kikao katika Kijiji cha Kajeje Mbunge Martha Mariki amesema kwa kutambua Juhudi zinazofanywa na serikali katika kuimalisha miundombinu ya Afya katika Mkoa wa Katavi na Halmashauri ya Nsimbo  kwa ujumla na kuchangia Milioni Tano ili kuharakisha ukarabati Jengo la Mama na Mtoto.

 ‘’ndugu zangu wana Kajeje Mimi Mbunge wenu wa Mkoa wa Katavi nimeguswa na Risala yenu nawachangia Milioni Tano ili kusaidia ukarabati huu wa Jengo la mama na Mtoto ili wanawake wenzangu wapate huduma bora wakija kujifungua hapa’’amesema Mbunge Martha.

zahanati ya Kijiji cha Kajeje ambayo Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Katavi,Martha Mariki ametoa shilingi Milioni Tano ili kusaidia ukarabati wa Jengo la Mama na Mtoto.

Ameeleza kuwa miongoni mwa Mambo ambayo serikali imekuwa ikiyafanya katika mkoa wa Katavi nikuendelea kujenga Zahanati,Vituo vya Afya ,Hospitali za Wilaya pamoja na uwekezaji mkubwa wa ujenzi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Katavi ambayo imeanza kufanya kazi na kuwaepushia adha wananchi kwenda kutibiwa katika Mikoa mingine.

‘’Niwaambie ndungu zangu mkoa wetu unahalmashauri Tano Tayari serikali imesha Jenga Vituo vya afya,na kujengwa kwa Hospitali ya Rufaa Mkoa wa Katavi Eneo la Kazima hii ni hatua kubwa ya mapinduzi ya utoaji wa huduma za afya kwa wananchi wetu tunaishukuru sana serikali kwa hili’’amesema Mbunge Martha Mariki.

Salehe Mrisho Diwani wa Kata ya Kanoge amemshukuru Mbunge huyo kwakuwaonea Huruma akina mama wa Kijiji cha Kajeje kwa Kuguswa na kuchangia Milioni Tano katika ukarabati wa Jengo la mama na Mtoto..

Wananchi wa Kijiji cha Kajeje wakimsikiliza Mbunge wa Viti maalumu mkoa wa Katavi Martha Mariki
Katika hatua nyingine amempongeza Mbunge wa Jimbo la Nsimbo kwa kuendelea kulipigania Jimbo la Nsimbo kwa kuhakikisha wananchi wanapata Maendeleo kupitia miradi Mbalimbali ya Serikali.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Nsimbo Charles Halawa amesema kuwa wanamshukuru sana Mbunge Martha Mariki na kwa Mchango wake na wao kama halmshauri tayari wametenga Milioni Hamsini kwaaajili ya ukarabati wa wa Jengo hilo la mama na Mtoto katika Kijiji cha Kajeje

‘’Mh Mbunge kazi uliyoifanya ya kutoa milioni Tano ni kazi kubwa sana katika jengo hili la mama na Mtoto  niukweli usiopingika kijiji hiki cha Kajeje wananchi wamekuwa wakipata adha katika eneo hili la afya lakini naamini sasa kutoa kwa hiii Milioni Tano itasaidia ukarabati huu’Amesema mwenyekiti Halawa

Ziara ya ya Mbunge Viti maalumu katika Mkoa wa Katavi Martha Mariki inaendelea ka Katika Wilaya ya Mpanda Hususani Jimbo la Nsimbo ambapo ametembea Kata ya Kanoge na Katumba na kutoa shilingi laki Tano kwa kila kata kama sehemu ya kuimarisha Jumuiya ya UWT Kwenye Kata hizo pamoja na kutoa Kadi za UWT ili jumuiya hiyo iendelee kuingiza wanachama wengi zaidi wa UWT.

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages