MBUNGE NSIMBO KUWAUGANISHA WASANII NA MFUKO WA TAIFA WA UTAMADUNI.

Mbunge wa Jimbo la Nsimbo,Wilaya ya Mpanda Mkoa wa Katavi,Anna Lupembe akiwahutubia wananchi wa kijijicha Tumaini leo wakati akihamasisha michenzo ndani jimbo hilo.

Na George Mwigulu,Nsimbo.

Mbunge wa Jimbo la Nsimbo,Wilaya ya Mpanda Mkoa wa Katavi,Anna Lupembe amedhamiria kuwaunganisha wasanii wa mziki wa kizazi kipya na muziki wa ngoma asili wa Jimbo hilo kwenye mfuko wa taifa wa utamaduni ili waweze kunufaika na mikopo ya fedha itakayowasaidia kujikwamua kiuchumi.

Vijana wa kikundi cha ngoma asili maarufu kwa jina la Sumu ya Mamba wakitubuhinza kwenye bonaza la nyimbo za asili na kizazi kipya.Kikundi hicho kimefanikiwa kushika nafasi ya kwanza kwenye mchuano huo.

Amesema hayo leo wakati wa hafla ya bonaza la kuibua vipaji vya Sanaa ya musiki katika kijiji cha Tumaini Kata ya Itenka Halmashauri ya Nsimbo mkoa hapa ambapo ameeleza nia yake ya kukuza sio mchezo wa mpira wa miguu pakee bali hata michezo mingine hususani pia sanaa.

Lupembe amesema kuwa kupitia bonaza hilo ameona vipaji mbalimbali jinsi ambavyo vijana wanaiba na kucheza jambo ambalo limemvutia sana na kuona namna bora ya kuwasapoti waweze kukua zaidi kwenye sanaa hiyo.

‘’… tumechenza ngoma na tumeona vipaji vya kwaya mbalimbali hapa,Ndugu zangu vikundi vyote vya ngoma mliojiandikisha mlioimba hapa ninawaingiza kwenye kundi la mfuko wa utamaduni wa taifa tutakuja kufanya uwasajili na BASATA itakuja kuwasajili na kuanza kupewa mikopo’’ amesema Lupembe.

Mbunge huyo ametoa rai ya kuacha tabia ya baadhi ya vikundi vya ngoma kuanzishwa na kupotea,Hivyo kuvitaka vikundi vyenye tabia hiyo kuacha sambamba na kutokujiandikisha kwa sababu fedha za mkopo watakazopewa lengo lake ni kunufaisha kundi,jamii ya Itenka na taifa vilevile mrejesho  utatolewa kwa mfuko wa utamaduni wa taifa.

Aidha kwa mwaka huu ameweza kuhamasisha Sanaa ya utamaduni maarufu kama ‘‘mbina’’ au ‘’ matanda’’ ambayo yatafanyika mwenzi wa tisa na kujumuisha makundi ya Sanaa ya jimbo lote la Nsimbo.

Aidha katika bonaza hilo mbunge huyo ameweza kutoa fedha Jumla Tshs 2,340,000/= kama zaidi kwa washindi wa vikundi vya ngoma za asili ,kwaya na waibaji binafsi wa mziki wa kizazi kipya ambapo mshindi wa kwanza amepewa fedha Tshs 300,000/-,Mshindi wa Pili Tshs200,000/- watatu Tshs 100,000/-na wa mwisho Tshs 50,000/- kwa kila makundi husika shindaniwa.

Naye kiongozi wa kundi la ngoma asili Sumu ya Mamba,Maria Nyango amemshukuru mbunge wa Jimbo la Nsimbo Anna Lupembe kwa kuweza kuona kuwa Sanaa ya uimbaji inanafasi ya kuwakomboa kiuchumi.

Ameeleza kuwa Sanaa ni ajira ambayo kama itathaminiwa na wadau mbalimbali itaweza kukua zaidi katika Mkoa wa Katavi.

Vilevile Zengo Tuma,Mkazi wa kijiji cha Itenka A amesema kuwa kuingizwa kwenye mfuko wa taifa wa utamaduni sio tuutawawezesha wasanii kupata mikopo ya kifedha bali ni lango la wasanii kutambulika kitaifa.

Hivyo akawaasa wasanii wa jimbo Nsimbo kuchangamkia fursa hiyo kwa kuhakikisha wanafanya kazi nyingi za Sanaa huku wakindumisha umoja na mshikamo. 

Tizama hapa chini moja ya ngoma ya Sumu ya Mamba wakicheza.



Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages