Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Katavi Martha Mariki [Katikati] akiwa katika kikao na Wanawake wa UWT kata ya Shanwe |
Wanawake, vijana na watu wenye uleamavu Katika mkoa wa Katavi wameaswa kuchangamkia fursa ya Mikopo ya Asilimia Kumi ambayo imekuwa ikitolewa na halmashauri ili waweze kujikwamua kiuchumi kwa kufanya Shughuli mbalimbali za kiuchumi .
Wanawake, vijana na watu wenye uleamavu Katika mkoa wa Katavi wameaswa kuchangamkia fursa ya Mikopo ya Asilimia Kumi ambayo imekuwa ikitolewa na halmashauri ili waweze kujikwamua kiuchumi kwa kufanya Shughuli mbalimbali za kiuchumi .
Wito
huo umetolewa na Mbunge wa Viti maalumu Mkoa wa Katavi wakati akizungumza na
wanawake wa UWT Katika Kata ya Shanwe na Kasokola zilizopo Halmashauri ya
Manispaa ya Mpanda Mkoa wa Katavi katika ziara anayoendelea nayo ya kutembelea
Kata 58 za Mkoa wa Katavi.
Mbunge
huyo amesema kuwa serikali imeanzisha Mfumo huo wa Kutoa fedha za Mikopo kwa
Makundi ya Vijana,Wanawake, na Walemavu kwa la kuhakikisha Makundi hayo
yanajikwamua kiuchumi.
Ameeleza
kuwa baadhi ya wanufaika wa Mikopo hiyo tangu ianze kutolewa na serikali
imewanufaisha kwa kiwango kukubwa kwa kubadilisha maisha yao ya kiuchumi
kupitia Miradi wanayoifanya kupitia fedha hizo za Mikopo ya halmashauri.
Katika
kuhakikisha uchumi wa UWT katika kata hizo unaimalika Mbunge huyo ametoa
shilingi Laki Tano kwa Kata ya Shanwe na Kata ya Kasokola kwa lengo la
kuimalisha uchumi wa Jumuiya ya UWT kwenye Kata hizo pamoja na kutoa Kadi za
UWT ili kuendelea kuongeza wanachama .
Pamoja
na hayo Mbunge Huyo wa Viti Maalumu Ktika mkoa wa Katavi Martha Mariki
amechangia kiasi cha Shilingi Laki Tatu katika kata ya Shanwe kwaajili ya
kusaidia ujenzi katika shule ya Msingi Makanyagio.
‘’Mh
Mbuge sisi tunaishuru sana serikali tumemaliza ujenzi wa Madarasa kumi nan ne katika
kata hii lakini katika miaka yenu miwili hii unaona haya majengo yote haya
tumefanya katika vipindi vyenu wakati ule watoto kuanzia Kidato cha Kwanza
nacha pili walikuwa wanakaa chini leo watoto wanachagua wasomee Darasa gani’’
Diwani huyo amechangia Shilingi Laki Moja kwa wanawake wa UWT Kwenye Kata hiyo kama Sehemu ya Kumuunga Mkono Mbunge Martha kwa Mchango aliowapatia wanawakehao wa UWT kwenye Kata hiyo.
kwa habari zaidi endelea kufatilia ukurasa wetu wa
kataviclub.blogspot.com