UDESO KUONGEZA UWAJIBIKAJI KWENYE FEDHA ZA UMMA

 



Mkurugenzi Mtendaji wa wa Taasisi ya Usevya Development [UDESO] Eden Wanyimba akielezea utekezaji wa Mradi kwa washiriki wa kikao hicho.

Na Walter Mguluchuma,Tanganyika

Taasisi   isiyo ya Kiserikali ya   Usevya  Development Sociaty(UDESO ) ya  Mkoani  Katavi  wamefanya  tathimi ya  mradi wa  AUDIT ACCOUNTABILILITY unatekelezwa katika  Wilaya ya Tanganyika wenye lengo la  kuangalia  miundo mbinu  inayotokana na taarifa za Mkaguzi Mkuu wa  Hesabu za  Serikali(CAG) zilizotolewa mwaka 2017 na kuangalia vitu ambavyo  vilivyofanyika hadi 2023

Washiriki mbalimbali wa kikao hicho wakifatilia kwa makini maelezo ya utekelezaji wa Mradi
Taasisi   isiyo ya Kiserikali ya   Usevya  Development Sociaty(UDESO ) ya  Mkoani  Katavi  wamefanya  tathimi ya  mradi wa  AUDIT ACCOUNTABILILITY unatekelezwa katika  Wilaya ya Tanganyika wenye lengo la  kuangalia  miundo mbinu  inayotokana na taarifa za Mkaguzi Mkuu wa  Hesabu za  Serikali(CAG) zilizotolewa mwaka 2017 na kuangalia vitu ambavyo  vilivyofanyika hadi 2023

Mkurugenzi  Mtendaji wa Taasisi ya Usevya  Development(UDESO)  E deni  Wanyimba amesema  mradi huu unatekelezwa katika  Kata mbili za  Kasekese   na Mwese katika Wilaya ya Tanganyika kwa ufadhili wa  shirika la  Instute of   Public A cconntabilility(WAJIBU).

Mkutano huu wa  umefanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika  na  umewashiirikisha wajumbe wa kamati ya PETS kutoka katika  Vijiji  vya Lugonesi,  Kasekese.

Waratibu  Elimu   Kata ,  Maafisa watendaji wa Kata hizo Maafisa  Mipango wa  Halmashauri,na mwakilishi wa Takukuru wa Wilaya ya Tanganyika walikuwa sehemu ya kikao hicho cha kufanya tathimini ya mradi huo unaotekelezwa katika Wilaya ya Tanganyika.

Wanyimba amebainisha kuwa  mradi huu unafanyika katika shule mbili za  Lugonesi  Kata ya Mwese na Kasekase ambao unatekelezwa katika  mambo makuu mawili  ambayo ni  ni ufatiliaji wa mali za   umma  na  mfumo wa kuangallia miundo mbinu  kufatia taalifa iliyotolewa na CAG .

Na ndio maana kwenye mradi huu wakaona wafatilia  vitu  vingine ambavyo vimefanyika hadi mwaka 2023 ambapo wameona ni vitu  vingi   vizuri ambavyo  Serikali wamevifanya  miradi   mingi imefanyika  kwenye maeneo mbalimbali  lakini kwenye mradi huu wanakamati za PETS  hivyo iliviweze kufanya kazi vizuri  lazima washirikiane na mifumo ya Serikali .

Kamati hizo za Pets zinachaguliwa na kijiji husika unapotekelezwa mradi  na Kijiji kina mamla ya kuwa na  kamati hiyo na ndio maana wanatakiwa kufanya kazi karibu  ili zile changamoto zinazopatikana kwenye miundo mbinu  wazilipoti mapema sana ili kuzuia changamoto   za miradi zisiweze kutokea  mfano kama fundi anajenga   kitu ambacho ni   kinyume cha utaratibu wa ujenzi wakiripoti mapema ili hatua  zichukuliwe mapema za  kurekebisha .

Wanyimba amesema  wakati huo huo  kamati za Pets wanaweza wakawa wameona jambo sio zuri  linafanywa na walimu au wanafunzi  kama utoro wa  mwanafunzi au mwalimu kushindwa kufanya kazi zake kwa mujibu wa sheria  wanaweza  kutowa taarifa kwenye vyombo ambavyo vinaweza kuchukua hatua   ambayo  Serikali inaona inafaa .

Amefafanua kuwa toka wameanza kutekeleza mradi huu mwezi wa tatu mwaka huu wameweza kuonyesha  ushirikiano mkubwa  na viongozi wa Vijiji na  wameweza kubaini baadhi ya changamoto  ya  baadhi ya wanafunzi  kushindwa kufika  shuleni kipindi cha masika  kutoka na mto katika kijiji cha Lugonesi kujaa maji  hivyo kuvuka wao inakuwa ni tatizo na kusababisha utoro wa reja reja .

Meneja wa mradi wa  kutoka Taasisi ya  WAJIBU  Moses  Kimaro  amesema   lengo  la mradi huu  unaotekelezwa na UDESO Ni kuisaidia Serikali  ili kuleta maendeleo yanayotakiwa kuletwa kwa wananchi .

Amesema wao  kama Wajibu uwajibikaji wanao utaka  ni kuangalia  ni uwajibikaji wa fedha na rasilimali za umma  kwa ajiri ya maendeleo ya Watanzania  kwani kama hili likifanyika vizuri  kwa fedha kusimamiwa vizuri hata  uwajibikaji wa kijamii utakwenda  vizuri  kwa sababu  rasilimali fedha inasimamiwa vizuri na matumizi yatatumika  ipasavyo .

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages