RC KATAVI WAPO TAYARI KUSHIRIKI KWENYE KUELIMISHA MPANGO WA DIRA YA 2050.


Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko akifungua semina ya mpango wavdira ya maendeleo ya Taifa ya 2050 iliyowashirikisha viongozi wa Mkoa na Wilaya zote za Mkoa wa Katavi na wadau mbalimbali iliyofanyika katika ukumbi wa Manispaa ya Mpanda

Na Walter Mguluchuma,Katavi .

Mkoa wa  Katavi uko tayari  kushiriki  kikamilifu kwa moyo  mkunjufu  kuhakikisha mpango wa dira ya  maendeleo wa mwaka 2050 unafanikiwa kwa musitakabari  mzuri na maendeleo ya Taifa la Tanzania.

Viongozi mbalimbali wakiwa na Mkuu wa Mkoa  wa Katavi wakati wa semina ya maandalizi ya uhamasishaji wa mpango wa dira ya maendeleo ya 2050

Hayo yamesemwa na Mkuu wa Mkoa wa Katavi,  Mwanamvua  Mrindoko wakati akifungua  semina   ya  zoezi  la kuelimisha umma kwa  viongozi na wakilishi wa makundi mbalimbali ya wadau  kuhusu dira ya maendeleo na utekelezaji wake  na  mchakato wa maandalizi ya dira ya maendeleo ya 2050 iliyofanyika katika ukumbi wa Manispaa ya Mpanda .

Mwanamvua amebanisha kuwa  tulikuwa   na dira ambayo inaishia mwaka 2025 na sasa tunakwenda kwenye  dira ya 2050 anaamini kuwa semina hiyo  itasaidia kujenga  uwelewa kwa viongozi wote wa  Mkoa na Wilaya  na wadau wote  kuhusu    mchakato  mzima wa  maandalizi  ya dira ya dira ya maendeleo ya 2050.

Amewaomba wananchi na viongozi wote wa   Mkoa wa Katavi kushiriki  kwa pamoja ili kuwa  na uwelewa wa pamoja  na  kwa kutambua kila mtu  majukumu yake ni yapi katika kuandaa mpango huo muhimu kwa Serikali na wananchi wote kwa ujumla .

Amebainisha kuwa  Mkoa wa Katavi wapo tayari  kwa kazi iliyoko mbele  ya kuhakikisha wananchi wote  na makundi mbalimbali wanapata uwelewa  kama  ambao waliopata wao   wa kuhusiana na dira  ya 2025 ambayoinaelekea ukingoni  na   dira  mpya ya 2050 inayokwenda kuandaliwa .

Mrindoko alisema Katavi wapo yatari  wapo  tayari kwa asilimia mia moja kuhakikisha jambo hilo muhimu hapa  nchini   nilifatiwa bila shida wala kikwazo chochote kile  hivyo watashiriki kwa ukamilifu kwenye jambo hilo .

Nae  Victoria  Mariale  kiongozi wa timu ya uhamasishaji  wa  mchakato wa maandalizi  ya dira ya maendeleo ya 2050 kwa  mikoa ya Katavi  Rukwa ,  Kigoma , Tabora na  Singida  amesema lengo kubwa la uhamasishaji ni kuendeleza  dhama kubwa  kwa wananchi kushiriki  kupanga maendeleo yao  ili kupanga Tanzania waitakao wao katika miaka 25 ijayo .

Kwa hiyo   mchakato  wa  kutengeneza  dira ya maendeleo ya  Taifa ulizinduliwa  tarehe 3  mwezi  wa  nne na Makamu wa Rais  Dk  Philipo Mpango  na alisisitiza ushirikishwaji  mpana wa Watanzania  kuamua  Tanzania waitakayo  kwa   hiyo  wao wapo kuhakikisha wanashiriki  kutowa maoni yao kutengeneza dira ya maendeleo .

Amesema mwamko wa washa  hiyo umekuwa ni mkubwa  hivyo wanaamini na wananchi watashiriki kwa wingi  kwa kuwa viongozi wengi wamefikiwa  kwani lengo kubwa ni kuhakikisha kila Mtanzania  anajua kuna  mchakato wa kutengeneza  dira na anatowa maoni yake  .

Padre Anacretus  Bafumkeko wa Kanisa  Katoliki   Jimbo la Mpanda  ameshauri uwepo wa makini kwenye  mchakato huu kwani kunaweza kukawepo watu wachache ambao wanaweza kufanyamambo  kiujanja ujanja  nap engine kukwamisha  mwelekeo wa dira  ambayo tunataka itusaidie  kuendelea na kufikia maendeleo endelevu .

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages