SERIKALI KUIMARISHA HUDUMA YA MAWASILIANO YA SIMU KATAVI.

 

Naibu Waziri wa wizara wa wizara ya Habari,Mawasiliano na Teknolojia, Mhadisi Kundo Mathew  akizungumza na wananchi wa Kata ya Nsekwa,Halmashauri ya wilaya ya Mlele juu ya mpango wa serikali ya kuimarisha sekta ya mawasiliano.

Na Walter Mguluchuma,Katavi.

Serikali chini ya Wizara ya Habari,Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Kupitia mradi wa Tanzania ya Kidigitali inatarajia kujenga minara ya mawasiliano katika Mkoa wa Katavi ili kuimarisha mawasiliano kwa wananchi na kuchochea ukuaji wa uchumi mkoani humo.

Hayo amesema leo Naibu Waziri wa wizara hiyo, Mhadisi Kundo Mathew katika ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Katavi akiwa kwenye ziara ya kikazi ambapo alisema kuwa maeneo ambayo itajengwa minara hiyo ni katika  kata za Kasasa,Majimoto,Bulamata,Ipwaga,Kasekese,Katumba na Uruwila.

Mhadisi Kundo ameeleza kuwa kujenga mnara wa mawasiliano moja gharama yake ni wastani wa  fedha Mil 350 ikiwa ni sawa na ujenzi wa kituo kimoja cha afya lakini serikali imeamua kuwekeza fedha zote hizo kwenye kujenga minara kwa sababu inatija.

Amesema kuwa tija inayopatikana kupitia mawasiliano ni pamoja na wananchi wataweza kuwasiliana   na vyombo vya ulinzi na usalama kwa kutoa taarifa za kiharifu

Vilevile mawasiliano ni afya kwani mtu anapopata changamoto yoyote ya kiafya anauwezo wa kuita gari la wagonjwa sambamba na kurahisisha taarifa kwa jeshi la zimamoto pale majanga ya moto yanapojitokeza.

Naibu Waziri huyo amesema kuwa katika kuhakikisha Tanzania inakuwa chini ya uchumi wa kidigitali (Digital Economy) serikali ilianzisha sheria namba 11 ya mwaka 2006 ya mfuko wa mawasiliano kwa wote.

Mfuko wa mawasiliano kwa wote lengo lake ni kutoa fedha za ruzuku kwa makapuni ya mitandao ya simu pale ambapo wakiona kama wakiwekeza watapata hasara kwa kukosa faida basi serikali itasaidia ili wasipate hasara na huduma ya mawasiliano kupatikana kwa wananchi wote.

“…mwenzi uliopita kunautiaji saini wa mikataba ya kupeleka huduma ya mawasiliano katika nchi nzima ambapo minara 758 inaenda kujengwa ambapo serikali inakwenda kutoa fedha za ruzuku Bilioni 126 ni sawa na asilimia 40 inakwenda kujenga minara hiyo “ Alisema Kundo.

Ameeleza lengo ni kuhakikisha maeneo yote ambayo hayana mvuto wa kibiashara,maporini yenye uhitaji wa mawasiliano na maeneo ya pakani serikali itahakikisha wananchi wanawasiliano kupitia mitandao husika ya nchini ili kuepuka kutumia mitandao ya nchi jirani.

Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Katavi,Onesmo Buswelu amemwomba Naibu Waziri huyo uharakishwaji wa ujenzi minara ya mitandao ya simu mkoni humo kwani wamezindua huduma ya M-Mama kwa lengo la kusaidia wanawake wajawazito wanaopata changamoto pindi ya kujifungua kwa kukosa mtandao ya simu pindi wanapotaka kutoa taarifa kwa gari la wagonjwa.

Buswelu amesema kuwa huduma ya M-Mama itakuwa na ufanisi mkubwa kwani hakuna atakaye kosa huduma ya afya kutokana na changamoto ya mtandao wa simu.

Mkuu wa Wilaya ya Mpanda,Jamila Yusuph amesema kuwa maisha kwa sasa yanategemea sana mawasiliano ya kimtandao kutokana na kuwa hurahisisha namna ya kutoa na kupokea taarifa za kijami.

Aidha ameishukuru serikali kwa mpango wake wa ujenzi wa minara ambayo itakwenda kuimarisha zaidi usalama wa watu kutokana na jiografia ya mkoa huo kuwa mpakani nan chi jirani.

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages