SERIKALI YAPONGEZWA UBORESHAJI MIUNDOMBINU YA AFYA KATAVI

Mbunge wa Viti Maalumu mkoa wa Katavi Martha Mariki akizungumza na wanawake wa UWT na Wanachama wa chama Cha Mapinduzi CCM katika Kata ya Majengo na Mpanda hotel

Na Paul Mathis,Mpanda.

Mbunge wa Viti maalumu Mkoa wa Katavi Martha Mariki amesema serikali ya awamu ya Sita ya Rais Dk Samia Suluhu Hassan inania ya dhati ya kuimalisha Huduma za afya kwa mkoa wa Katavi .

Mbunge wa Viti maalumu Mkoa wa Katavi Martha Mariki amesema serikali ya awamu ya Sita ya Rais Dk Samia Suluhu Hassan inania ya dhati ya kuimalisha Huduma za afya kwa mkoa wa Katavi .

Akizungumza na wanawake wa umoja wa Chama cha Mapinduzi CCM [UWT]Katika kata za Mpanda hotel na Kata ya Majengo zilizopo halmashauri ya Manispaa ya Mpanda mkoa wa Katavi.

Amesema kuwa Kujengwa kwa hospitali ya Rufaa ya mkoa wa Katavi pamoja na hospitali za Wilaya katika mkoa wa Katavi unaonyesha namna serikali imedhamiria kuimalisha huduma za afya katika mkoa wa Katavi.

‘’Sote nimashahidi akinana mama wenzangu Hospitali ya Rufaa mkoa wa Katavi imekamilika na inafanya kazi hospitali za wilaya kwenye mkoa wetu zipo na zingine zinaendelea kujegwa hii itakwenda kuwasaidia wananchi kupata huduma za matibabu kwa urahisi’’

Amewaomba wanachama hao kuendelea kuiunga mkono serikali ya Rais Dk Samia Suluhu na chama cha Mapinduzi CCM kwakuwa Chama na serikali yake chini ya Chama hicho kinania ya dhati ya kuwatumikia watanzania kwa vitendokwa kuleta maendeleo kwa wananchi.

Amewakumbusha wanachama hao kuendelea kuyasema mazuri yanayofanywa na serikali kwa  wananchi ambao wanabeza Jitihada za serikali katika kuwatumikia wananchi.

Pamoja na hayo Martha ameendelea kuikumusha jamii kuzingatia malezi ya watoto wao na kupinga vitendo vya ukatili wa kijinsia ambavyo vimekuwa vikilipotiwa katika baadhi ya maeneo ya mkoa wa Katavi na Tanzania kwa ujumla.

Katika ziara hiyo Mbunge huyo ametoa shilimgi Laki Tano kwa umoja wa wanawake wa Chama cha Mapinduzi CCM [UWT] katika Kata za Mpanda hotel na Majengo ili kujiinua kiuchumi.

Mwenyekiti wa Umoja wa wanawake UWT Wilaya ya Mpanda Tausi Ramadhani amewaomba wanawake hao kutumia fursa hiyo kukopeshana kupitia shuguli ndogo za kiuchumi.

''niwaombe sana wanawake wenzangu tuka tumia fedha hizi kukopeshana kwenye biashara ndogondogo na siyo kugawana na kuzifanyia matumizi yasiyo faa''

Diwani wa Kata ya Majengo William Mbogo amesema kuwa anaridhishwa na kazi zinazofanywa na wabunge wote wa mkoa wa Katavi kwa lengo la kuhakikisha mkoa wa Katavi unapiga hatua kimaendeleo.

Ziara ya Mbunge wa Viti maalumu mkoa wa Katavi Martha Mariki imeanza leo katika Wilaya ya Mpanda kwa kuanza kufanya ziara katika kata zilizopo Manispaa ya Mpanda 

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages