UWT MPANDA YAPIGA HESABU UCHAGUZI SERIKALI ZA MITAA 2024

 

Mwenyekiti wa Umoja wa wanawake wa chama Cha Mapinduzi CCM Wilaya ya Mpanda Tausi Ramadhani akizungumza na wanawake wa UWT kwenye Mkutano wa Baraza la UWT  wilaya ya Mpanda. 

Na Paul Mathias,Mpanda

Wanawake wa Jumuiya ya UWT wilaya ya Mpanda wameaswa kuendelea kuhamasisha wanawake kujiunga na jumuiya hiyo ili kuongeza nguvu ya pamoja katika kuelekea uchaguzi wa Serikali za Mitaa.

Mwakilishi wa Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Leah Gawaza akiwahutubia wanawake wa UWT Wilaya ya Mpanda katika baraza la UWT lililofanyika katika ukumbi wa Mikutano wa Chama cha Mapinduzi Wilaya ya Mpanda

Jumuiya ya wanawake ya Chama cha Mapinduzi CCM UWT wilaya ya Mpanda wameaswa kuendelea kuhamasisha wanawake kujiunga na jumuiya hiyo ili kuongeza nguvu ya pamoja katika kuelekea uchaguzi wa Serikali za Mitaa.

Akiwa hutubia wanawake wa Jumuiya hiyo Katika Baraza la UWT Wilaya ya Mpanda Mwakilishi wa Mkuu wa hilo Leah Gawaza ambae ni Afisa Tarafa ya Misunkumilo amesema kuwa wanawake kupitia UWT wanao wajibu wa kuhakikisha wanaongeza idadi ya wanachama ili kutengeneza mazingira mazuri katika uchaguzi ujao wa serikali za mitaa.

‘’muda siorafiki tunakimbizana sana na uchaguzi wa Mwakani tusimwache mtu hata mmoja nyuma kila kura moja inathamani ndunguzangu sasa hivi tunaenda kwenye Boksi la kura kwenye Boksi tunahitaji watu ili kuhakikisha tunapata ushindi hivyo akina mama tuhakikishe tunawaingiza watu wengi zaidi’’

Katika hatua nyingine amewapongeza UWT kwa kuwa na mikakati mbalimbali ya kujiinua kiuchumi kupitia vikundi mbalimbali hali ambayo inasaidia jumuiya hiyo kujitegemea kiuchumi

Awali akisoma taarifa ya UWT Wilaya Kwaniaba ya Katibu wa Jumuiya hiyo Grace Abisai amesema kuwa chama hicho kimendelea kuongeza wanachama kupitia usajili mtandaoni.

‘’kwa kipindi cha January 2023 hadi June 2023 kumekuwa na ongezeko la wanachama ni 4199 na mpaka sasa waliosajiliwa kwenye mfumo wa Tehama ni wanachama 2354’’

Amesema jumuiya hiyo inamipango mbalimbali ikiwemo kujenga nyumba ya Mtumishi wa UWT Wilaya ya Mpanda kuandaa semina na mafunzo kwa wanachama na kuanzisha miradi ya kiuchumi kuanzia ngazi ya Kata hadi wilaya na kuendelea kuongeza wanachama kupitia mfumo wa Tehama.

Mwenyekiti wa UWT Wilaya ya Mpanda Tausi Ramadhani amesema ajenda yao kubwa kwa sasa ni kushinda katika uchaguzi wa Serikali za mitaa Mwakani pamoja na uchaguzi mkuu 2025

Kwa upande wake Mbunge wa Viti maalumu Mkoa wa Katavi Martha Mariki amewaasa wanawake wa UWT Wilaya ya Mpanda kuendeleza umoja nan a mshikamano ili kuhakikisha Chama cha Mapinduzi kupitia UWT wanakuwa chachu ya ushindi katika chaguzi Mbalimbali.

Sebastiani Kapufi Mbunge wa Mpanda Mjini Akitoa salamu kwa wanawake wa Jumuiya hiyo amesema  UWT ni nguzo mhimu katika Wilaya ya Mpanda kwakuwa mara nyingi Jumuiya hiyo imekuwa imara katika kufanikisha Mambo mbalimbali ndani ya chama na Jumuiya hiyo kwa ujumla.

Jumuiya ya wanawake ya Chama cha Mapinduzi UWT inajumla ya wanachama 14,898 .

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages