Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Katavi Martha Mariki akimtua ndoo kichwani Mkazi wa Kjiji cha Mwamkulu alipotembelea Mradi wa Maji ambao unawanufaisha Wananchi kwa kujipatia Maji Safi na Salama. |
Na Paul Mathias,Mpanda
Mbunge wa Viti maalumu Mkoa wa Katavi Martha Mariki ameishukuru serikali kwa kuwaletea Huduma ya Maji safi na Salama wa kazi wa Kata ya Mwamkulu Manispaa ya Mpanda Mkoa wa Katavi.
Mbunge wa Viti maalumu Mkoa wa Katavi Martha Mariki ameishukuru serikali kwa kuwaletea Huduma ya Maji safi na Salama wa kazi wa Kata ya Mwamkulu Manispaa ya Mpanda Mkoa wa Katavi.Akiwa katika ziara ya kutembelea Kata zote za Mkoa wa Katavi amefika na kujionea namna mradi huo unavyo wasaidia wananchi kupata huduma ya Maji kwa uhakika tofauti na hapo siku za nyuma ambapo wananchi walikuwa wanatumia Maji ambayo si safi na salama.
‘’tunaishukuru
sana serikali ya awamu ya Sita ya Mama yetu Dk Samia Suluhu Hassan kwa jinsi
alivyo dhamilia kumtua mama ndoo kichwani’’
‘’Sisi
kama wananchi wa Mkoa wa Katavi mimi kama mwakilishi wa kundi la wanawake na
mwakilishi wa wananchi wa mkoa wa Katavi nasema naishukuru sana serikali yetu
kutuletea mradi huu wa Maji wenye thamani ya Milioni 400.73 tunasema asante
sana mama wananchi wa Mwamkulu wanasema asante kwa mradi huu’’.
Katika
hatua nyingine ameipongeza Ruwasa kwa Mkoa wa Katavi kwa usimamizi makini ambao
umewezesha wanachi hao kupata huduma ya maji safi na salama kwa wakati pasipo
na ucheleweshaji wa aina yeyote.
Katika
ziara hiyo Mbunge Huyo amepata fursa ya kuzungumnza na wanawake wa UWT Kata ya
Mwamkulu na kuwapatia kiasi cha shilingi Laki Tano ili waweze kujikwamua
kiuchumi.
Magreth
Robert Mkazi wa Kijiji cha Mwamkulu amesema huduma hiyo ya upatikanaji wa maji
imewaepushia kutumia muda mwingi kutafuta Maji kitendo ambacho kilikuwa
kinaathiri shuhguli za uzalishaji mali kijijini hapo.
Kalipi
Katani Diwani wa Kata ya Mwamkulu amewashukuru wabunge wa mkoa wa Katavi kwa
kuisemea kata ya Mwamkulu kwenye chombo cha uwakilishi wa wananchi Bungeni na
hatimae kupata mradi huo wa Maji.
‘’tunawashukuru
sana Wabunge wetu kwa kusimama kwa kauli moja kwa kuisemea Kata yetu sisi
tunafarijika sana tunaendelea kuwaombea muwesalama pamoja na mama yetu Rais
Wetu Dk Samia Suluhu Hassan’’
Mradi huo utakwenda kunufaisha Mitaa mitatu kwenye Kata hiyo ambayo ni St Maria,Mkwajuni na Mkokwa ambayo ni sawa na Jumla wote ya wakazi 16,735 wa Kata ya mwamkulu wananufaika na Mradi huo wa Maji.