WANANCHI NSIMBO WAMPONGEZA MBUNGE NA MKURUGEZI UJENZI WA SHULE.

 

Mbunge wa Jimbo la Nsimbo,Wilaya ya Mpanda Mkoa wa Katavi,Anna Lupembe akiweka tope kwa ajili ya kujengea moja ya darasa katika shule ya msingi Makomelo ambalo linajengwa chini ya mradi wa Boost katika kitongoji cha Songambele kijiji cha Tumaini Kata ya Itenka.

Na George Mwigulu,Nsimbo.

Wananchi wa kitongoji cha Songambele Kijiji cha Tumaini Kata ya Itenka halmashauri ya wilaya ya Nsimbo Mkoa wa Katavi wamekiri kuwa matatizo ya utolo shuleni na mimba za utotoni zitakoma baada ya kukamilika kwa mradi wa ujenzi wa shule ya msingi Makomelo.

Mbunge wa jimbo la Nsimbo,Anna Lupembe akikangua leo ujenzi wa shule ya msingi Makomelo.

Ujenzi wa shule hiyo unatekelezwa chini ya mradi wa Boost ambapo fedha Mil 561 zinatumika kwenye ujenzi wa vyumba vya madarasa 16 sambamba na vifaa vya samani kama vile madawati.

Masolwa Malubalo,Mkazi wa kitongoji cha Songambele ameeleza wamekuwa na matatizo ya watoto wao kwenda shule umbali wa zaidi ya km tisa jambo ambalo licha ya juhudi kubwa za kuchangia chakula mahala pakusomea lakini bado watoto wao walishindwa kumudu umbali hao.

Malubalo amesema kuwa umbali huo umekuwa ni chanzo cha watoto wao kushindwa kufika shule na kuwa watolo sugu sambamba na baadhi ya watoto wao wakike kupata vishawishi kwa wanaume waovu na kupatiwa ujauzito na kushindwa kuendelea na masomo.



“mtoto anaondoka akimwaga mzazi wake kuwa anakwenda shule lakini anaishia kujificha machakani (Maporini) muda wa jioni ukifika anarudi nyumbani na kusema baba nimesoma kumbe la!” amesema  Malubalo.

Pili Deus anasema walichoshwa na matatizo hayo ambapo waliweza kuchanga fedha ambazo ziliwawezesha kupata eneo lenye thamani ya Mil 4.8 na kuanza kubeba mawe ili kuanza ujenzi wa shule.

Anafafanua kuwa Mbunge wa Jimbo la Nsimbo,Anna Lupembe ndio aliwaambia kuwa kwa kuwa ameona juhudi zao atawapigania ili hakikisha wanapatiwa fedha ambazo zitawezesha ujenzi wa shule hiyo.

“hatukutarajia baada ya kuambiwa Mil 561 zimeletwa kwa ajili ya ujenzi wa shule yetu,Tunamshukuru Mbunge Anna na serikali ya halmashauri ya wilaya ya Nsimbo  chini ya Mkurugenzi Mohamed kwa kufanikisha hili” amesema Pili.

Kwa upande wa Mbunge wa Jimbo la Nsimbo,Anna Lupembe amesema kuwa serikali ya awamu ya sita  lengo lake ni kutengeneza mazingira bora na rafiki ya wanafunzi kusomea ili kujenga taifa la watu wasomi.

Ambapo amesema ujenzi wa shule hiyo utakwenda kuondoa adha ambayo wanafunzi wa maeneo hayo wamekuwa wa kipata kwa muda mrefu ikiwa nia yake ya kujenga shule mpya ya sekondari akiiweka wazi kwenye kitongoji hicho.

Lupembe amesema kuwa mradi wa boost umekuja ukiwa umejitosheleza,hivyo ametoa maagizo kuwa hata furahishwa kuona wananchi wanachangishwa fedha kwa ajili ya madawati.

Naye Diwani wa Kata ya Iteka,Joseph Laurent amesema ujenzi wa shule katika eneo hilo umelenga kuwapunguzia watoto umbali wa kwenda masomoni ikiwa pamoja na kupunguza idadi kubwa ya wanafunzi katika shule ya msingi Iteka A ambapo zaidi ya wanafunzi 3600 wako hapo.





Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages